Mwakyembe: Sikusinzia...

mimi naona watz hawana umuhimu wa kujua wazir gani yuko wizara gani au anafanya nini, hii ni kujionesha tu muhimu ni kutengeneza system yako hata kama umejifungia chumbani kila kitu kinaweza kwenda sawa.
 
Haters ni weeeengiiii kwa jambo jema. Ni lazima ujue matatizo ndo ufanye maamuzi, siyo unakula kiyoyozi, na kukiurupuka kufanya maamuzi bila utafiti. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Hongera jembe Mwakyembe!
 
Waziri wa Uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe amesema kuwa hakupata kusinzia njia nzima, wakati akisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa treni, kwakuwa anafanya utafiti wake.

Waziri Mwakyembe amesema kuwa hakuweza kusinzia kwakuwa alihitaji kujiridhisha na hali ya usafiri wa treni na pia kujionea hali halisi ya wananchi wa Tanzania sehemu ambapo treni linapita.

'Nimejifunza mengi sana;ya Wizara yangu na Wizara nyinginezo' alisema Dr.Mwakyembe. 'Nitatumia niliyoyaona kwa maslahi ya Taifa' aliongeza.

Chanzo: Mimi mwenyewe niliyeambatana naye kwenda Dodoma kwa treni...

Aende zake na Undumilakuwili wake. Yale aliyoyaficha wakati wa EPA/ RICH-MONDULI ndiyo yalikuwa na maslahi kwa Taifa. Aliudanganya umma kwa kubakiza mengine kifuani mwake kwa kuogopa serikali yake ya SISIEMU kuanguka. Leo anakuja na maslahi ya Taifa......tangu lini????? F*&%#~.... maslahi ya Taifa in my A.S.S
 
Nakushukuru, nasubiri kuona matokeo. Ila kumbuka ninasukumwa na uzoefu wa vijisafari kama hivi kutokuwa na tija yoyote hasa katika kada ya viongozi wetu wa sasa, kuanzia kwa mheshimiwa Rais. Huyu amekuwa akizunguka wizara na idara nyingi za serikali matokeo yake amesababisha inefficience kubwa zaidi katika usimamizi wa serikali yetu.

Alikuwapo Lowasa, alifanya ziara nyingi na kutoa maelekezo na maamuzi ya papo kwa papo ambayo hatuoni mwangwi wake ukirindima mpaka sasa. Lowasa alikuwa akifuta leseni za mainginia kutokana na ujenzi mbovu wa maghorofa akiwa site, ujenzi wa maghorofa yenye viwangu vya chini ndio umeshamiri mara dufu sasa.

Huyu Mwakyembe huyu, majuzi kasema hajaenda Bandarini sababu bado anawapa muda wa kujipanga, how many times mr president went there? not less than three times since 2005, nini kimetokea? Nini Mwakyembe Jamani.

Both,Mwakyembe and CCM have to go kama kweli tunataka kuanza kuamini mategemeo ya ufanisi baada ya vijisafari vya namna hii kufanyika.

Nitasubiri Matokeo. Nashukuru.



Nani kakwambia kua CCM ikiondoka madarakani chama kitakachokuja kitaleta neema, acha ulimbuken wewe, bado CCM ipo imara na wachapa kazi wameanza kuonyesha muelekeo, tuwape ushirikiano.
 
Sijaona ubaya wa Mwakyembe kusafiri kwa treni.
Hivi utawezaje kuhubiri ubaya wa pombe wakati hujawahi hata kuionja? tusubiri matokeo ya utafiti wake ndipo tuje na kejeri za namna hii.

utasuluhishaje migogoro ya ndoa wakati hujawahi kuoa ?kweli tusubiri
 
Achana na Mwakyembe, wewe binafsi hauelewi matatizo wanayokabiriana nayo wasifiri wanaotumia treni? haya, ufahamu wa matatizo hayo unaweza kukusaidi vipi kulikwamua shirika la reli kutoka kwenye mning'inio lililokuwa nao.

Kwa mfano, kuna tatizo la wafanyakazi kutokulipwa mishahara yao, unatatuaje tatizo hili kwa kusafiri kwa treni? miundombinu ya reli imezeeka na haiwezi kuimili safari za mara kwa mara na shehena nzito, unatatuaje na hili kwa kusafiri? kuna tatizo la wafanyakazi kurusha ticketi, unalitatuaje hili kwa kusafiri na treni?

hiyo ni moja kati ya mbinu ama njia kabla ya kufikia maamuzi mazuri ya kutoa maamuzi.ingekuwa amefanya hivyo dr slaa ama mbowe angeitwa majina kibao mara kamanda mara jembe mara mpiganaji lakini tumewazoea kamanda shibuda anawaita watu pingapinga
 
Hapa ndipo nashindwa kuwaelewa watu. Hivi hata mtu akifanya jambo jema kwa kuwa itikadi yako ni tofauti na ya kwake linabadilika na kuwa baya???? Hapa Mwakyembe kakosea nini? Hivi yeye kufuatilia utendaji wa Shirika hili ambalo limekuwa kama ndoo mbovu ambayo kila jitihada za kujaza maji zimeshindikana kutokana na kuvuja nalo limekuwa kosa!!!!!!!!!! You are not serious. Kutokana na kupitia physically masuala yaliyo chini ya Wizara yake anajiweka katika nafasi nzuri ya kutoa maamuzi au ushauri sahihi tofauti na kukaa kwenye kiyoyozi na kungojea kila siku apokee taarifa za walio chini yake ambazo sometimes zinakuwa sugar quoted. Kwa kusafiri na wananchi ni sehemu mojawapo ya kupata mawazo raw from horses mouth. Maana mawazo aliyoyapata hayajachakachuliwa kwa maslahi ya yeyote maana ameyapata live kutoka kwa wadau wa usafiri huo. Hivyo nina hakika amejifunza jambo jipya.
Hongera bro. Mwakyembe keep it up lakini uyafanyie kazi na uyaweke bayana uliyoyaona na jinsi unavyokusudia kuyafanyia kazi.
Hii ndiyo bongo bwana; ukifanya ubaya unalaumiwa na ukifanya wema unalaumiwa pia tena kwa maneno ya kebehi.
 
Next time wabunge na mawaziri wote watumie train kwenda Dodoma kwenye vikao vya bunge. Hii inapunguza gharama za mafuta ya gari na kupunguza utorokaji wa wabunge katika bunge. Hongera sana Mwakyembe.
 
nina mashaka na wanaopinga utendaji kazi mzuri wa mwakyembe, mi binafsi nahsi wanaopinga sio wapinzani bali ni watendaji wabovu wa TRL. Mambo wanayoyafanya yanawasuta. Kaza buti Mwakyembe wananchi wa mikoa ya Tabora, Kigoma na Mwanza wanateseka mno.
 
Waziri wa Uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe amesema kuwa hakupata kusinzia njia nzima, wakati akisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa treni, kwakuwa anafanya utafiti wake.

Waziri Mwakyembe amesema kuwa hakuweza kusinzia kwakuwa alihitaji kujiridhisha na hali ya usafiri wa treni na pia kujionea hali halisi ya wananchi wa Tanzania sehemu ambapo treni linapita.

'Nimejifunza mengi sana;ya Wizara yangu na Wizara nyinginezo' alisema Dr.Mwakyembe. 'Nitatumia niliyoyaona kwa maslahi ya Taifa' aliongeza.

Chanzo: Mimi mwenyewe niliyeambatana naye kwenda Dodoma kwa treni...

Kimtazamo naona Mwakyembe kafanya jambo sahihi ila tunacho subiri ni ripoti ya utafiti wake na jinsi atakavyo itumia kutatua matatizo ya usafiri hapa nchini.
 
Mbona anafanya kazi kwa kutaka coverage kubwa sana ya media? anamaanisha nini

Haya pia tuliyaona kwa Ezekia Mainge alipokuwa anakimbizana na wachoma mkaa ktk hifadhi za Taifa, kumbe ilikuwa ni changa la macho. Alijitahidi sana kuficha appetite yake ya mafaranga kupitia media lkn hamu ya kula ikamuumbua.

Kwanza waziri mzima kukimbizana maporini manake nn! utawakimbiza wangapi?

Mwakyembe apande na mabasi ya mikoani aone hizo speed kama haamini. Bado meli/ boti. Bado Toyo (boda boda)
kaaazi kweli kweli!!
 
Back
Top Bottom