Mwakyembe: Sikusinzia...

Mwakyembe: Sikusinzia...

"katika serikali na mashirika yetu ya UMA kwa muda mrefu Kama mwakyembe"
Sangara unaweza tuambia huo mda mrefu aliofanya kazi na hayo mashirika?
Na hii ndio tabia ya Tz kufanya kazi kwa mazoea nijuavyo yeye ni mara ya kwanza kuwa waziri kwenye hii wizara!
Au ulimaanisha matatizo kwenye mashirika na wizara zote za JK yanafanana?Such that ata solution zake zafanana?
 
Sangarara, na wewe unaongea (unaandika ?) tu kwa vile una hiyo fursa ya kuandika ama kuongea. Bila maneno meeengi nakuuliza kuwa: Unamfaham yule jamaa aliyekuwa akifanya experiment yake kwa kuwasha torch mchana kweupe? Je, aligunduwa nini? Je, alikuwa kichaa au? Ukiweza kujibu hayo masuali utamuunga mkono Dr Mwakyembe.

Acha upofu wa fikra wewe. Mtu yeyote ambaye analazimika kufanya ziara ama experiements kama unavyosema wewe ili kubaini matatizo yanayowakabili wananchi wake hafai kupewa nafasi yoyote ile ya kisiasa. na kwa msingi huu Mwakyembe anakalia hiyo ofisi kinyume na matarajio ya kisiasa.

Huyo mtu na experiment yake mimi siwafahamu, labda unipe taarifa zake zaidi, hivyo mpaka sasa mfano wake hauna uhusiano wowote ni utoto aliofanya mwakyembe.
 
Big up Sangarara, hawa watu hawana jipya ni usanii tupu. aende kariakoo jioni apande daladala za kimara au mbagala ili ajifunze vizuri
 
Kuna watu umu wanamind Mwakyembe no wonder ni wahanga wa hii pangua pangua ya JK.
 
unajua upinzani sio kupinga kila kutu ambacho chama tawala wanafanya, kwani pamoja na mabaya wayafanyanyo pia kuna mema wayafanyayo.Anachofanya Dr.Mwakyembe ni sawa kabisa kiutendaji kwani itamsaidi kwenye baadhi ya maamuzi yake ya kitendaji.
Wakuu lets be honest to ourselves kama mtu akifanya vizuri lets give him credit, na sio kupinga kila kitu kwasababu ya upinzani wa kivyama.
 
TRL walijua kuwa mkuu anasafiri?
Maana lazima wabehave na kurekebisha mambo kama wanajua the big boss yumo ndani ya mchuma.
Angekata ticket kwa kutumia jina la mtu mwingine, halafu akasema anaangalia tu treni then anazama mchumani bila maafisa kujua.
 
TRL walijua kuwa mkuu anasafiri?
Maana lazima wabehave na kurekebisha mambo kama wanajua the big boss yumo ndani ya mchuma.
Angekata ticket kwa kutumia jina la mtu mwingine, halafu akasema anaangalia tu treni then anazama mchumani bila maafisa kujua.
Ni kweli mkuu....tumeona unafiki wa watendaji wengi hasa pale maofisa wa juu wanapofanya ziara sehemu zao. Bora Mh mrema wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani aliwahi kufanya ziara ya kushtukiza kituo kikuu cha mabasi ya mikoani pale wananchi walipolalamika kuhusu nauli kupandishwa hasa kwenda mikoa ya kaskazini. Mh. Magufuli naye aliwahi kufanya pale kivukoni na matoteo tukayaona. Mh. Mwakyembe nae angefanya bila kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari nadhani matokeo ya utafiti wake yangekuwa bora sana kuliko aliyoyapata sasa
 
Acha upofu wa fikra wewe. Mtu yeyote ambaye analazimika kufanya ziara ama experiements kama unavyosema wewe ili kubaini matatizo yanayowakabili wananchi wake hafai kupewa nafasi yoyote ile ya kisiasa. na kwa msingi huu Mwakyembe anakalia hiyo ofisi kinyume na matarajio ya kisiasa.

Huyo mtu na experiment yake mimi siwafahamu, labda unipe taarifa zake zaidi, hivyo mpaka sasa mfano wake hauna uhusiano wowote ni utoto aliofanya mwakyembe.
Pamoja na upofu wangu wa fikra bado ninaamini kwa 100% kuwa Mh Dr Mwakyembe ana sababu ya msingi kufanya hivyo. Kuwa kiongozi katika serikali na mashirika mengi ya umma na kwa muda mrefu haitoshi kukupatia ufahamu wa kudumu wa matatizo ya kila sekta iliyopo nchini. Bado kuna nafasi ya kujifunza kwa vitendo. Usikae tu ofisini na kungoja kuletewa habari na wasaidizi wako. Wakati mwingine uende kwenye "site" ukajionee mwenyewe mambo ...

Matatizo ya wa-Tz wote karibu yanafanana, Kyera, Dodoma hadi Kigoma. Lakini bado kuna nafasi ya kujifunza, kuchunguza kwa vitendo na kutowa majibu stahiki.

Naomba umngoje kumlaumu pale atakapotoa majibu yasiyo na tija baada ya uchunguzi wake. Usilaumu hatua ya uchunguzi. Ungoje kulaumu matokeo ya hatua zisizofaa atakazochukua.

Nimezungumza kama kipofu tu, lakini nikifanya uchunguzi wa mambo hata mimi nitaweza kutowa majibu sahihi. Asante
 
Hapa ndipo nashindwa kuwaelewa watu. Hivi hata mtu akifanya jambo jema kwa kuwa itikadi yako ni tofauti na ya kwake linabadilika na kuwa baya???? Hapa Mwakyembe kakosea nini? Hivi yeye kufuatilia utendaji wa Shirika hili ambalo limekuwa kama ndoo mbovu ambayo kila jitihada za kujaza maji zimeshindikana kutokana na kuvuja nalo limekuwa kosa!!!!!!!!!! You are not serious. Kutokana na kupitia physically masuala yaliyo chini ya Wizara yake anajiweka katika nafasi nzuri ya kutoa maamuzi au ushauri sahihi tofauti na kukaa kwenye kiyoyozi na kungojea kila siku apokee taarifa za walio chini yake ambazo sometimes zinakuwa sugar quoted. Kwa kusafiri na wananchi ni sehemu mojawapo ya kupata mawazo raw from horses mouth. Maana mawazo aliyoyapata hayajachakachuliwa kwa maslahi ya yeyote maana ameyapata live kutoka kwa wadau wa usafiri huo. Hivyo nina hakika amejifunza jambo jipya.
Hongera bro. Mwakyembe keep it up lakini uyafanyie kazi na uyaweke bayana uliyoyaona na jinsi unavyokusudia kuyafanyia kazi.
 
Ina maana Dr. hakuwahi kupanada tren mpaka juzi ndio kapanda?
ili kufanya uchunguzi hatari tupu
 
Pamoja na upofu wangu wa fikra bado ninaamini kwa 100% kuwa Mh Dr Mwakyembe ana sababu ya msingi kufanya hivyo. Kuwa kiongozi katika serikali na mashirika mengi ya umma na kwa muda mrefu haitoshi kukupatia ufahamu wa kudumu wa matatizo ya kila sekta iliyopo nchini. Bado kuna nafasi ya kujifunza kwa vitendo. Usikae tu ofisini na kungoja kuletewa habari na wasaidizi wako. Wakati mwingine uende kwenye "site" ukajionee mwenyewe mambo ...

Matatizo ya wa-Tz wote karibu yanafanana, Kyera, Dodoma hadi Kigoma. Lakini bado kuna nafasi ya kujifunza, kuchunguza kwa vitendo na kutowa majibu stahiki.

Naomba umngoje kumlaumu pale atakapotoa majibu yasiyo na tija baada ya uchunguzi wake. Usilaumu hatua ya uchunguzi. Ungoje kulaumu matokeo ya hatua zisizofaa atakazochukua.

Nimezungumza kama kipofu tu, lakini nikifanya uchunguzi wa mambo hata mimi nitaweza kutowa majibu sahihi. Asante

Nakushukuru, nasubiri kuona matokeo. Ila kumbuka ninasukumwa na uzoefu wa vijisafari kama hivi kutokuwa na tija yoyote hasa katika kada ya viongozi wetu wa sasa, kuanzia kwa mheshimiwa Rais. Huyu amekuwa akizunguka wizara na idara nyingi za serikali matokeo yake amesababisha inefficience kubwa zaidi katika usimamizi wa serikali yetu.

Alikuwapo Lowasa, alifanya ziara nyingi na kutoa maelekezo na maamuzi ya papo kwa papo ambayo hatuoni mwangwi wake ukirindima mpaka sasa. Lowasa alikuwa akifuta leseni za mainginia kutokana na ujenzi mbovu wa maghorofa akiwa site, ujenzi wa maghorofa yenye viwangu vya chini ndio umeshamiri mara dufu sasa.

Huyu Mwakyembe huyu, majuzi kasema hajaenda Bandarini sababu bado anawapa muda wa kujipanga, how many times mr president went there? not less than three times since 2005, nini kimetokea? Nini Mwakyembe Jamani.

Both,Mwakyembe and CCM have to go kama kweli tunataka kuanza kuamini mategemeo ya ufanisi baada ya vijisafari vya namna hii kufanyika.

Nitasubiri Matokeo. Nashukuru.
 
Ina maana Dr. hakuwahi kupanada tren mpaka juzi ndio kapanda?
ili kufanya uchunguzi hatari tupu
Hata kama aliwahi kupanda mara 21 hapo kabla haimzuwii kupanda tena sasa hivi. Matatizo ya jana siyo ya leo. Hata kama matatizo ya jana na leo yakifanana, yatatofautiana unene. Mh Dr Mwakyembe anayo sababu ya msingi kupanda train ili kujifunza zaidi uhalisia wa matatizo ya usafiri huo.
 
hivi angeenda akapanda treni kimya kimya, akafanya utafiti wake huko njian kimya kimya..kisha akakaa chini kimya kimya na kuanza kuchambua hizo findings zake kisha kuandika report au hata kusema kile alichokiona na nini anatarajia kufanya kuboresha au kudumaza asingeweza kufika huko dodoma?!!
 
watakuwa wana matatizo ya akili kama hawatataka kusikia kuhusu reli, wenzetu nchi zilizoendelea wana matreni mengi ajabu na still maroli nayo yanaongezeka kila kukicha, kila kizazi kinapokuwa na huduma za usafiri zinatakiwa ziendelezwe zaidi, malori yataendelea kuitajika kwa ajili ya mizigo hata reli iweje.

wenye malori unadhan wanataka kusikia abt rail???thubutuuuuu
 
Nakushukuru, nasubiri kuona matokeo. Ila kumbuka ninasukumwa na uzoefu wa vijisafari kama hivi kutokuwa na tija yoyote hasa katika kada ya viongozi wetu wa sasa, kuanzia kwa mheshimiwa Rais. Huyu amekuwa akizunguka wizara na idara nyingi za serikali matokeo yake amesababisha inefficience kubwa zaidi katika usimamizi wa serikali yetu.

Alikuwapo Lowasa, alifanya ziara nyingi na kutoa maelekezo na maamuzi ya papo kwa papo ambayo hatuoni mwangwi wake ukirindima mpaka sasa. Lowasa alikuwa akifuta leseni za mainginia kutokana na ujenzi mbovu wa maghorofa akiwa site, ujenzi wa maghorofa yenye viwangu vya chini ndio umeshamiri mara dufu sasa.

Huyu Mwakyembe huyu, majuzi kasema hajaenda Bandarini sababu bado anawapa muda wa kujipanga, how many times mr president went there? not less than three times since 2005, nini kimetokea? Nini Mwakyembe Jamani.

Both,Mwakyembe and CCM have to go kama kweli tunataka kuanza kuamini mategemeo ya ufanisi baada ya vijisafari vya namna hii kufanyika.

Nitasubiri Matokeo. Nashukuru.
Nadhani umesahau kuwa tunazungumza juu ya kitendo cha Mh Dr Mwakyembe kupanda treni. Usichanganye na Mh Dr Kikwete (M/K CCM) na wala usichanganye na Mh EN Lowasa (Mb na W/Mkuu mstaafu). Pamoja na kwamba hawa wote wapo chama kimoja cha CCM lakini, wana tofauti katika hatua wanazochukuwa kutatua matatizo ya watu.

Kwa vile umekubali kusubiri matokeo, na mimi naunga mstari huo. Sasa tuko pamoja
 
[QUOTE

Maisha ya hao wananchi hao yanatofauti gani na yale ya wananchi wa Jimboni kwake Kyela? Majuzi alisema amepanda daladala kutoka mwenge kwenda tegeta na anadai kwamba tatizo pekee aliloliona na gharama kubwa ya nauli, matatizo ya wanaotumia usafiri wa daladala yanatofauti gani na wale wanaotumia treni?
Ni tatizo gani la usafiri wa treni mwakyembe amejifunza kupitia safari hiyo? alienda kuona kama kweli injini inazima zima? haya sasa siku hiyo haikuzima, kwa hiyo ametoka na picha gani hapo? kwamba habari za kuzima zima kwa injini za treni na hujuma za kishenzi zinazofanywa za kung'oa mataruma ya reli ni za uongo?

Give me a break.
[/QUOTE]

Nimefurahishwa sana na Hojaji zako..... Mimi nilikua nafikiria sana juu ya HOJA kwamba "ALIKWENDA KUFANYA UCHUNGUZI" Kweli naamini sasa kwamba Uongozi wetu ni wa kurithi na Wenye nacho tu ndio wanapata hata hizo nafasi za UWAZIRI ie Hussein Mwinyi, hajui reli ya kati wala Hood bus ikoje humo ndani. Sasa kumbe hata Mwakyembe hajui na wala hakuwahi kupanda Treni! Mwe!

Mimi nilidhani iwe kawaida kwa viongozi wetu kuwa watu wa kawaida hata kutumia usafiri wa kawaida ili kuwa aware NA SIO KWENDA KUWACHUNGUZA wananchi jinsi wanavyopata taabu. KIONGOZI MZURI HUJITOA KWA AJILI YA WALE ANAOWAONGOZA.:angry::angry::boxing:
 
Sasa natamani hata waziri wa afya naye alazwe Amana Hosp nayeye hasisinzie afanye uchunguzi.
 
Nahis tumelaaniwa hii nchi,mtu akifanya vibaya matusi akionesha nia na moyo wa kufanya kazi matusi tena,hata malaika aongoze taifa hili itakua bure kabisa.

Na kunatabia inakua sasa Tanzania ya kikundi cha watu fulani wa chama fulani wao nia yao ni kuona mambo yanaharibika na hayaendi vizuri ili wao wazidi kupata umaarufu wa kisiasa,huko ni kupoteza muda na haioneshi zamira safi kwa taifa hili,Hata kama mtu sio wa chama chako akifanya jambo jema aungwe mkono bila kujali itikadi yake.Kwani hakuna chama chochote Tanzania au duniani ambacho kikishika tu dola ndio itakua muarobaini wa matatizo yote ya nchi.
 
Nadhani umesahau kuwa tunazungumza juu ya kitendo cha Mh Dr Mwakyembe kupanda treni. Usichanganye na Mh Dr Kikwete (M/K CCM) na wala usichanganye na Mh EN Lowasa (Mb na W/Mkuu mstaafu). Pamoja na kwamba hawa wote wapo chama kimoja cha CCM lakini, wana tofauti katika hatua wanazochukuwa kutatua matatizo ya watu.

Kwa vile umekubali kusubiri matokeo, na mimi naunga mstari huo. Sasa tuko pamoja

Sawa, Naomba kuweka record sawa. Lowasa hakustaafu, aliachia nafasi ya uwaziri mkuu ili ainusuru serikali (na hii ni kwa mujibu wa maneno yake), mpaka sasa bado watanzania wanachunguza aliinusuru serikali namna gani? lakini kuhusu hasa kilichotokea kuna mambo mengi yanazungumzwa wengine wanasema alifukuzwa, wengine alishurutishwa na wengine alihujumiwa, cha msingi ni kwamba namna alivyooachia nafasi ile hakuwezwi kufananishwa na kustaafu hata mara moja.
 
Back
Top Bottom