Mwakyembe kusema kwamba Mhe.Nassari aliingia na chupa ya konyagi bungeni akazuiwa mlangoni sidhani

PRODA LTD

JF-Expert Member
Oct 20, 2016
1,005
1,333
Habari inayodaiwa kutolewa na Mwakyembe kwamba Mhe.Nassari aliingia na chupa ya konyagi bungeni akazuiwa mlangoni (lango kuu la bunge) sidhani kama imetoka kinywani kwa Mwakyembe. Kwa sababu siamini mtu mzima tena mwenye PhD kama anaweza kusema uongo wa hovyo kiasi hicho.

Habari hiyo ni ya uongo kwa sababu mbili kubwa:

[HASHTAG]#Mosi[/HASHTAG]; Kabla ya kufika lango kuu la bunge (main entrance) kuna geti. Na pale getini kuna scanner, ambapo mtu yeyote anayepita pale (wakiwemo wabunge) hukaguliwa na kuna vitu hawaruhusiwi kupita navyo. Vinabaki pale getini watavichukua wakati wa kutoka. Mojawapo ni kileo cha aina yoyote pamoja na silaha yoyote. Sasa Nassari alipitaje na chupa ya Konyagi hadi lango kuu la bunge kama inavyoelezwa? Ina maana hakukaguliwa getini? Scanner ilikua imekufa? Askari hawakuwepo? Uongo mtupu.!

Halafu Mwakyembe anataka kutuaminisha kwamba Joshua alidhamiria kuingia na Konyagi hiyo ndani ya ukumbi wa bunge? This cant be serious. Ukumbi wa bunge wenye CCTV camera kila kona na camera za waandishi wa habari aingie na Konyagi? Ili iweje? Ainywe mbele ya CCTV camera, waandishi, spika, mawaziri na wabunge wenzie? Uongo mtupu. Huu uongo wanaweza kuamini watu waliopata division zero tu kama Bashite na si vinginevyo.

[HASHTAG]#Pili[/HASHTAG]: Joshua Nassari ni Mkristo aliyeokoka (A saved christian). Sio tu kwamba hanywi pombe, bali hata kubeba pombe habebi, sembuse kwenda nayo bungeni??

Mwakyembe aache kushuhudia wenzie uongo akiwa kama Mkristo. Hiyo ni dhambi na anatakiwa atubu. Ni aibu PhD holder anashindwa kwa hoja na kijana mdogo anaamua kudamage reputation yake kwa kumpakazia mambo ya hovyo. Nassari hanywi pombe kabisa. Sasa aliibeba ya nini? Ukiwa muongo unatakiwa kuwa smart.

Mwakyembe alitakiwa kuchunguza kwanza kama Nassari anakunywa pombe au lah kabla hajamakazia. Unampakazia mtu kubeba konyagi wakati hanywi pombe kabisa.!! Maajabu. Ni sawa na kutaka kumchafua padri kwa kutangaza umemkuta mke wake guest house na mwanaume mwingine, wakati mapadri hawaoi. Mwishoni unaumbuka wewe. Shame.!!
 
Kwenye mfano wa Padri, umechemka. Kuna nchi baadhi ya mapadri wameruhusiwa kuoa na kanisa Katoliki limeridhia.
 
Kuna tetesi tetesi kuhusu ukimya wa nassari,haonekani kwenye masuala ya lema wala ya chadema,nadhani amekaribia kupata anguko kubwa muda si mrefu
 
Mwakyembe aache kushuhudia wenzie uongo akiwa kama Mkristo. Hiyo ni dhambi na anatakiwa atubu. Ni aibu PhD holder anashindwa kwa hoja na kijana mdogo anaamua kudamage reputation yake kwa kumpakazia mambo ya hovyo. Nassari hanywi pombe kabisa. Sasa aliibeba ya nini? Ukiwa muongo unatakiwa kuwa smart.
 
Kwenye mfano wa Padri, umechemka. Kuna nchi baadhi ya mapadri wameruhusiwa kuoa na kanisa Katoliki limeridhia.

Chief usipoteshe sio kanisa katoliki ninalolijua mimi. Kanisa halina double standard. Litakua kanisa lako na watu wako
 
Kwenye mfano wa Padri, umechemka. Kuna nchi baadhi ya mapadri wameruhusiwa kuoa na kanisa Katoliki limeridhia.
Mapadri wanaowa lakini si wa kanisa katoliki bali ni wa kanisa la Anglicana.

Hata aliyekuwa Jaji mkuu wa Tanzania Augustino Ramadhani kwa sasa pia ni padre wa kanisa la Anglicana Dayosisi ya Zanzibar.
 
Back
Top Bottom