Mwakyembe: ATCL Kununua Ndege Mbili Mpya!

Mwakyembe: ATCL Kununua Ndege Mbili Mpya!

Hivi katika bajeti ya Wizara yake, kweli wametenga pesa ya kutoshaya kununua hizo ndege 2 na meli? Tatizo wabunge wengi wa CCM ni VILAZA hata kufuatilia jambo dogo kama hilo wao ni shida. Kama hakuna pesa ya kutosha iliyotengwa kununua hizo ndege na meli. Je huyo Mwakembye atanunua hizo meli na ndege kwa ma........nde yake?!
 
Dk. Harrison Mwakyembe ameliambia Bunge punde tu kuwa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) litanunua ndege mbili mpya katika mwaka ujao wa fedha.

Katika maelezo yake hajaweka wazi hadi sasa ATCL ina ndege ngapi zinazomilikiwa kwa asilimia 100 na shirika hilo mbali na kuzungumzia ndege kadhaa za kukodi.

Najua JF ina wajuvi wengi, mwenye taarifa hizi atiririke hapa tujue!
Isijekuwa ndege za kichina, maana inasemekana ni rahisi kwa bei!
 
Sijui hizi ahadi mwisho wake ni lini
Ukitafakari Hii nchi na viongozi wake,inatia hasira
 
Halafu wizara yake itaishia kupewa 25% ya budgeted amount for 2014/2015 fiscal year ataishia kuuchuna kimyaaa, akiulizwa mwakani ndege mbili ulizoahidi ziko wapi? Ndio ataanza blah blah zao ooh!!! Wizara ilipewa 25% ya pesa ilizoomba hivyo tukashindwa kununua ndege kama tulivyoahidi kwenye kikao cha bajeti kilichopita.

Hivi kabla ya mwaka kwisha huwezi kuibana wizara ya fedha kama kasma yako haijafika na mwaka unaisha?
 
Ahadi kama vikao vya harusi, si angesubiri anunue kwanza ndo aje kubwabwaja mbele ya wasanii wenzake?
 
Hili nchi sisi ni wapumbavu! Kila mmoja anaahidi tu, muda wenyewe umebaki mfupi badala ya kushughulika na ahadi za Vasco da Gama bado wanaongeza ahadi zingine tu, she.nzy kabisa! Hebu watuache tupumue aiseee, hapa tunajipanga kusubiri utawala Mmasai wa Kimeru au kutoka UKAWA, period!!!
 
Labda kama ni ndege za miti. Huyu si ndo alikikana kitabu chake mwenyewe
 
Mwakyembe namuheshimu sana..kuna baadhi ya mambo anajitofautisha na mawaziri wengine wa CCM,ila ktk hili huyu Mnyakyusa anapiga tu siasa hakuna uhalisia.
Mwaka jana walikuja na porojo hizo hizo,lkn mwaka umeisha bila kuwa na matokeo chanya,ATCL inamiliki ndege moja tu aina ya Bombadier DH8(?)5H-MWF,Baada ya ile moja kupata Snug kule Kigoma na wajanja wakala malipo ya bima na hawajanunua nyingine.
Baada ya kuona Bunge la Bajeti linakaribia Wizara na ATCL wakaamua kwenda kukodi(lease)ndege nchini Kenya,aina ya CRJ-200 kwa ghalama kubwa,na waliokodisha wakakataa ndege yao usiwekwe twiga wetu wala Registration ya Kibongo(Tz),walichoruhusu ni kuandikwa kwa Jina la "Air Tanzania-The Wings of Kilimanjaro",ndege imebaki na Reg ya Kenya ya 5Y-WWA,marubani wao,Air hostess wao na hata Engineer ni wao.
Juma lililopita Serikali ilipoona inakaribia kusoma bajeti ya Wizara ikaanzisha Route ya Dar-K'njaro-Znz,hii ni kuhadaa tu watu kuwa shirika lao pendwa ATCL lipo "hai";na kiukweli shirika hili linapendwa sana na Watz,hata liwe na kandege kamoja ka magumashi bado watu watakata tiketi na kupanda,kwa ndege hizo mbili moja ya kukodi na moja wanaomiliki ATCL inafanya safari za Dar to Mwanza,Dar to K'njaro,Dar to Hahaya,Dar-Kigoma-Bujumbura.
Waliingia mkataba na mwarabu wa Oman,lkn Omana akataka jengo la ATCL kwa miaka 90,wakaenda kwa Mchina napo wakashindwana,hizo tetesi za kuleta ndege mbili hazijaanza leo,toka mwaka wa jana wa pesa...waalisema wataleta Bombadier CRJ-900,lkn kimya na wamekuja na story nyingine...Usaniii mtupu.
ATCL ilikufa kifo cha membe pale "wahuni"wachache walipoihujumu,KLM ilitaka kuingia ubia na ATCL lkn wahuni wachache wapenda 10% wakapotezea dili...KLM akaamua kuingia kufanya kazi na Kenya Airways(KQ),leo hii Wakenya wapo juu sana,wanamiliki ndege aina ya E190 za kutoka Brazil za kutosha,wana B767.,B737,B738 na mpaka sasa wamevuta B777-200(?).....Pale waziri mwenye dhamana ya shirika wakati huo alipoamua kujiingiza ktk biashara ya usafiri wa anga ndipo shirika letu lilipokufa rasmi,hakuwa tayari kuona National Carrier inakua zaidi ya shirika lake na la wabia wenzake.
Leo wanataka kulifanya shirika lao binafsi kama ndio National Carrier....jawabu la kurudisha ATCL ktk hadhi yake,ni kama sbb zile zile za kuirudisha Tz ktk ramani yake.....KUIONDOA CCM NA VIBARAKA WAKE MADARAKANI
 
Mwakyembe namuheshimu sana..kuna baadhi ya mambo anajitofautisha na mawaziri wengine wa CCM,ila ktk hili huyu Mnyakyusa anapiga tu siasa hakuna uhalisia.
Mwaka jana walikuja na porojo hizo hizo,lkn mwaka umeisha bila kuwa na matokeo chanya,ATCL inamiliki ndege moja tu aina ya Bombadier DH8(?)5H-MWF,Baada ya ile moja kupata Snug kule Kigoma na wajanja wakala malipo ya bima na hawajanunua nyingine.
Baada ya kuona Bunge la Bajeti linakaribia Wizara na ATCL wakaamua kwenda kukodi(lease)ndege nchini Kenya,aina ya CRJ-200 kwa ghalama kubwa,na waliokodisha wakakataa ndege yao usiwekwe twiga wetu wala Registration ya Kibongo(Tz),walichoruhusu ni kuandikwa kwa Jina la "Air Tanzania-The Wings of Kilimanjaro",ndege imebaki na Reg ya Kenya ya 5Y-WWA,marubani wao,Air hostess wao na hata Engineer ni wao.
Juma lililopita Serikali ilipoona inakaribia kusoma bajeti ya Wizara ikaanzisha Route ya Dar-K'njaro-Znz,hii ni kuhadaa tu watu kuwa shirika lao pendwa ATCL lipo "hai";na kiukweli shirika hili linapendwa sana na Watz,hata liwe na kandege kamoja ka magumashi bado watu watakata tiketi na kupanda,kwa ndege hizo mbili moja ya kukodi na moja wanaomiliki ATCL inafanya safari za Dar to Mwanza,Dar to K'njaro,Dar to Hahaya,Dar-Kigoma-Bujumbura.
Waliingia mkataba na mwarabu wa Oman,lkn Omana akataka jengo la ATCL kwa miaka 90,wakaenda kwa Mchina napo wakashindwana,hizo tetesi za kuleta ndege mbili hazijaanza leo,toka mwaka wa jana wa pesa...waalisema wataleta Bombadier CRJ-900,lkn kimya na wamekuja na story nyingine...Usaniii mtupu.
ATCL ilikufa kifo cha membe pale "wahuni"wachache walipoihujumu,KLM ilitaka kuingia ubia na ATCL lkn wahuni wachache wapenda 10% wakapotezea dili...KLM akaamua kuingia kufanya kazi na Kenya Airways(KQ),leo hii Wakenya wapo juu sana,wanamiliki ndege aina ya E190 za kutoka Brazil za kutosha,wana B767.,B737,B738 na mpaka sasa wamevuta B777-200(?).....Pale waziri mwenye dhamana ya shirika wakati huo alipoamua kujiingiza ktk biashara ya usafiri wa anga ndipo shirika letu lilipokufa rasmi,hakuwa tayari kuona National Carrier inakua zaidi ya shirika lake na la wabia wenzake.
Leo wanataka kulifanya shirika lao binafsi kama ndio National Carrier....jawabu la kurudisha ATCL ktk hadhi yake,ni kama sbb zile zile za kuirudisha Tz ktk ramani yake.....KUIONDOA CCM NA VIBARAKA WAKE MADARAKANI
Mkuu nasikia Lusajo ni mjomba wake kabisa na anavurunda sana ila ndo kamkabidhi shirika


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
safi mwakyembe keep going

Huyu nae mwacheni aote mbona ameshindwa kununua meli ya kuwahudumia watu wa kwao kyela? Atcl ina madeni lukuki na serikali ya magamba imefilisika hizo hela za kununulia ndege mpya zitatoka wapi; pengine hao waarabu wa Oman wanaotaka kuinunua ATCL!!!! Hawa magamba wote ni wasanii kwani hata bosi wao aliahidi kununua meli kule lake victoria kureplace MV Bukoba lakini mpaka sasa ni hekaya za Abunuwasi!
 
..waziri mnaa tu huyu...nchi hii kama watawala wangetaka tungeweza kuwa na ndege hata za dreamliner(from Boeng)hata sawa na Kenya.....nasema kama watawala wangetaka hili lingewezekana....kwa kuangalia wizi unaotokea huko kwenye madini yetu na malia asili na mapesa yanayoibwa kule BOT.....tungeweza kabisa kuwa na ndege mpya kabisa za maana...tena kwa viwanja hivi hivi vya ndege tulivyonavyo...maana kwenye viwanja tulivyonavyo zinatua ndege zote kubwa toka kwa wenzetu(KQ,ethiopian, KLM, british airways, swissair etc etc).....Kwa hiyo sisi kutokuwa na ndege za maana wala si viwanja....bali kukosa utashi kwa watawala wetu na pia kuibiana wenyewe kwa wenyewe.....Najiuliza sana mbona watawala wanaweza kununua magari ya kifahari kila wizara ..tena brand new.....Inakuwaje wanaridhika taifa hili kukosa ndege za maana??.....


..HIvi kweli pamoja na watawala kusafiri huko nje kwa kupanda ndege za wenzetu ..haiwaumi wao kutokua na ndege za taifa lao??...Kwanini wanashindwa kununua ndege mpya kubwa kwenye nchi hii yenye utajiri wa mali asili na utalii????..kuibiana ndio shida ya taifa hili...tungeweza kuwa na kila kitu cha maana...kama tungeacha kuibiana...
 
halafu wizara yake itaishia kupewa 25% ya budgeted amount for 2014/2015 fiscal year ataishia kuuchuna kimyaaa, akiulizwa mwakani ndege mbili ulizoahidi ziko wapi? Ndio ataanza blah blah zao ooh!!! Wizara ilipewa 25% ya pesa ilizoomba hivyo tukashindwa kununua ndege kama tulivyoahidi kwenye kikao cha bajeti kilichopita.

nilikuwa nakusubiri kama umeona upuuzi wao wa kila siku as long umemaliza

sina comment mkuu
 
Vipi hajazungumzia wizi unaoendelea bandarini?

Alitudanganya kuwa amekomesha wizi wa mizigo,na kukwapua vitu kwenye magari ya wateja.

Lakini hivi karibuni jamaa zangu watatu wote waliopitisha magari yao bandari ya Dar es Salaam ,wamekuta sreen imenyofolewa,mmoja wamekomba jeki,mwingine wameina spare tyre na kumuwekea ambayo imesha kwisha.

Tanzania tumeoza kila kona,acha kagame atudharau.

Aliyekuambia Rwanda hakuna ufisadi nani?

Rwanda corruption tenders
 
Back
Top Bottom