Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Siamini kuwa upo upande mwa Dr kuhusu ile ripoti.

Angemmaliza nani? Labda angeimaliza familia ya mkuu maana ndo inahusika.
Ajabu ya ripoti ile ni kuwa watu "safi" kabisa waliachia ngazi ili kuwalinda wahalifu bila hata kusutwa na dhamira zao kwa kitendo hiki kiovu kuliko maovu yaliyokuwa yametendeka.
 
Siamini kuwa upo upande mwa Dr kuhusu ile ripoti.

Angemmaliza nani? Labda angeimaliza familia ya mkuu maana ndo inahusika.


Ndilo lilikuwa kusudi lake kuacha kusema yote...na hili lilikuwa kosa la pili.......
 
kwa nini hii thread imeunganishwa??? ingeacha peke yake
 
Ajabu ya ripoti ile ni kuwa watu "safi" kabisa waliachia ngazi ili kuwalinda wahalifu bila hata kusutwa na dhamira zao kwa kitendo hiki kiovu kuliko maovu yaliyokuwa yametendeka.

Duh Mshikaji, jamaa mligombea "kitu" nini? maana! dah.

Kukujibu ile ilikua CALCULATED move ya 2015 ili tusivunje MKATABA WETU na mkuu.
 
Ole wao wafanyao hayo maana halitabakia jiwe juu ya jiwe. Mungu wetu ataweka kila kitu peupe ndio waanze kutumikia adhabu.
 
Ole wao wafanyao hayo maana halitabakia jiwe juu ya jiwe. Mungu wetu ataweka kila kitu peupe ndio waanze kutumikia adhabu.

dada jane,

Taarifa zilizopo ni kwamba mhudumu wa ofisi ya Dr Mwakyembe pale Wizara ya Ujenzi alifariki ghafla, ni baada ya taarifa kuanza kuzagaa kwamba Dr kalishwa sumu.

Ni wazi Mungu ameanza kuwaumbua!!!
 
Duh Mshikaji, jamaa mligombea "kitu" nini? maana! dah.

Kukujibu ile ilikua CALCULATED move ya 2015 ili tusivunje MKATABA WETU na mkuu.
Sasa imekuwa MISCALCULATION. Inapoteza maisha ya watu. Hofu imetanda kila mahala. Viongozi wetu kukaa wakanywa chai pamoja wakazungumzia mustakbali wa NCHI haiwezekani tena. "Natural death" sasa hivi haipo tena. Kila kuugua, kufa kwa KIONGOZI yeyote kuna mkono wa mtu sasa.
Kwa nini tusiwaweke kando hawa waliofikishana hapa ili TAIFA bila wao lisonge mbele?
 
Inasikitisha sana kwa hali ya Mwakyembe ilivyo sasa. Ila nachoomba aseme ukweli ili tujua nini kimemsibu na nini tukifanye. kwani ulishatoa waraka ambao ulielezea jinsi hali yako ya usalama ilivyotete na sasa haya tena yanatokea. Hivyo kunauhusiano wa moja kwa moja kati ya haya.
 
Mungu Muweza wa yote Atatenda Miujiza ya Kumponya Mwakyembe. Amina.
 
Sijui kwanini roho yangu inanisuta kumhurumia Mwakyembe ikiwa yeye hakuwahurumia watanzania mil.45.
 
dada jane,

Taarifa zilizopo ni kwamba mhudumu wa ofisi ya Dr Mwakyembe pale Wizara ya Ujenzi alifariki ghafla, ni baada ya taarifa kuanza kuzagaa kwamba Dr kalishwa sumu.

Ni wazi Mungu ameanza kuwaumbua!!!

Hiyo ni kweli kabisa na hawa jamaa washenzi kweli wamemuua huyo jamaa ili kusiwepo na ushahidi, mwakyembe mwenyewe anasema ilikuwa ijumaa aliponawa ofisini kwake na ndipo baadae kama baada ya masaa kadhaa mikono ikaanza kupauka, akapaka mafuta haikusaidia tatizo alidharau alifikiri ni kitu kidogo kumbe ndio ilikuwa inasambaa kadri siku zilivyokuwa zinakwenda.

kuna jamaa hapo juu anasema hii nchi tunakwenda wapi kiasi kwamba watu hawaaminiani hata kupeana mikono maofisini, hawanyi hata maji, emagine kwenye cabinet meeting ya jk kuna watu wanajulikana kabisa kama akina mwandosya hawagusi kitu wala kula na kumywa chochote mle ndani sasa maisha gani hayo watajengaje nchi hivyo?

wahudumu wenyewe wanajua flani halagi hivyo hawamwekei, eh EL Kiboko!
 
...
kuna jamaa hapo juu anasema hii nchi tunakwenda wapi kiasi kwamba watu hawaaminiani hata kupeana mikono maofisini, hawanyi hata maji, emagine kwenye cabinet meeting ya jk kuna watu wanajulikana kabisa kama akina mwandosya hawagusi kitu wala kula na kumywa chochote mle ndani sasa maisha gani hayo watajengaje nchi hivyo?

wahudumu wenyewe wanajua flani halagi hivyo hawamwekei, eh EL Kiboko!

Na sio kwenye cabinet tu, popote pale ambapo makundi husika huwa yanakutana, watu wanakuwa waoga hata kusalimiana, hkwa hofu ya kupakazwa sumu. Ni suala ambalo lipo siku nyingi sana kwamba wajumbe wa kamati kuu na cabinet huwa wanaingia na maji 'YAO' mkononi toka nje ya jengo, kwa hofu ya kukumbwa na yaliyomkuta mbunge wa Kyela.
Mungu amsaidie apone
 
Siamini kuwa upo upande mwa Dr kuhusu ile ripoti.

Angemmaliza nani? Labda angeimaliza familia ya mkuu maana ndo inahusika.

Hapa ndipo kizunguzungu inaingia. Mwakyembe aliwasilisha ripoti ya Richmond bungeni kwa mbwembwe akiweka msisitizo jinsi EL alivyohusika katika kuvuruga taratibu ili Richmond ipate tenda. Hata baadaye, nje ya bunge, amekuwa akiwashangaa watu wanaojaribu kumsafisha EL na sakata hilo. Sasa kama kweli mhusika ni mkulu mwenyewe (na Mwakyembe anajua) na ndio maana ripoti iliminywa ili kumnusuru, basi ndugu yetu atakuwa anabeba mzigo mzito sana wa dhamiri isiyo safi. Hapo atahitaji maombi ya nguvu si kumponyesha mwili tu bali hasa kumnusuru kiroho.
 
Kwa watu mashuhuri au maarufu hakuna siri kwa mambo yao!
 
Yeye mwenyewe pia hakufanya FAIR PLAY kwenye ripoti yake. Inawezekana ni maradhi tu lakini wabongo hatuchoki kutafuta sababu.

fair player ipi uliyoitaka? mbona mnarudia mle mle jamani? au ndio lowasa kawatuma!
 
Duh!!!siku ya kufa kwangu,kama Mungu ndo mwenye mamlaka na kama kwa nguvu zake uovu hautashinda basi wauaji wa Mwakyembe na wapatilizwe na hasira yake Mwenyezi

Nani kakuambia Mwakyembe anakufa? Wewe Mungu?
 
Endapo siri aliyo nayo ni pamoja na kile ambacho hakukisema ili kuinusuru Serikali nzima ya CCM (au mkulu mwenyewe kama wengine wanavyodai) basi sidhani kama mwenye sababu (motive) kubwa ya kutaka kumpotezea atakuwa EL - labda kwa kisirani tu; lakini wale ambao hawajatajwa ambao kawabakiza ndani ya mtima ndo wanaweza kuwa wanahanja kuhakikisha hiyo "siri" haitoki.
 
Back
Top Bottom