Kwani wiki nne hazijaisha? Siku za kukaa kazini ngapi ktk wiki? Mtu kaamua tu kuleta thread isiyo na tija!
wiki nne zimekwisha tarehe 04. Huyu na wana ccm wenzake waliokuwa wanajisifia hapa kuwa wamekuja kukomesha upinzani alidhani amepata kitu cha kuhamisha nguvu za mjadala wa watu hapa na kumbe akajikuta anapata aibu ya mwaka.
Naona watu wa spin mnataka kulazimisha kuwa mwezi ni wiki nne, haya twende kwenye hesabu labda ndio mtaelewa manpokosea.
kama mwezi ni wiki nne mwaka una siku ngapi?
Miezi 12 kila mwezi una wiki 4 Na kila wiki ina siku saba 7: 12 * 4*7 = 336
Kwa hiyo wenzetu nyinyi mwaka wenu una siku 336!
Halafu wakati mwingine mnapojibu swali lisomeni vizuri kwanza kabla ya kukurupuka, swali ni kwani mwezi una SIKU ngapi, swali halikuwa mwezi una WIKI ngapi.
Spin zimetawala mwenendo wako MGAYA unapaswa kujirekebisha, unaweza kuonyesha post yoyote niliyosema mimi ni mwana CCM au niliyojisifia kuwa nimekuja kukomesha upinzani?
Sina matatizo na kubadilisha maamuzi. Siku yoyote mtu yeyote akigundua amefanya maamuzi yasiyo sahihi vi vyema kubadilisha ili aanze kufanya yale yaliyo sahihi. Tatizo langu ni pale maamuzi hayo yanapokuwa ni ya kuwapa mawazo watu wengine au ni kwa manufaa ya umma kama ilivyo hapa JF. Mtu anapofanya maamuzi na akaueleza umma maamuzi yake na pengine kuwashawishi baadhi ya watu wamuunge mkono kwa uamuzi wao huo basi ni JUKUMU la mtu huyo kuwaarifu umma kuwa AMEBADILI uamuzi. MWK amekuja na thread ya kumuomba Rais ajiuzuru na amelikwepa jukumu lake la kuwakumbusha wasomi wa thread hiyo kuwa hapo awali aliandika maelezo tofauti juu ya swala hilohilo.
Lengo la thread hii ni kukumbushana MAJUKUMU tuliyo nayo katika kuelemisha jamii.Tukiacha mapengo kama haya tunakuwa sio waelimishaji bali ni wana propaganda - spin masters!
Tujiweke katika nafisa ya wale walioamua kuungana na MWK kumpa Rais mwezi mmoja kama alivyoandika halafu kabla mwezi haujaisha tunaona haya aliyoandika tena, bila kugusia kile alichoandika awali - je tungemfikiriaje MWK?
Ze Marcopolo, ingawa siko kumtetea Mwafrika wa Kike, naamini kuwa pale 08 May 2008 alipotoa duku duku lake alikuwa na hiyo dhamira ya kumpa muungwana hiyo moratorium ya mashambulizi kwa mwezi mmoja. Hata hivyo, kwa kuwa dada Mwafrika wa Kike akagundua, ebo mbona huyu ninayempa pumzi ajirekebishe mbona hajaafanya chochote cha maana, ilipofika 05 Juni 2008 akaamua kumfungia kazi. Kumbuka, Mwafrika wa Kikenaye ni binadamu ana uhuru wa kubadilisha mtazamo pale anapojisikia, kama mwanasiasa mahiri Harold Wilson anavyotukumbusha hapa chini:
"He who rejects change is the architect of decay. The only human institution which rejects progress is the cemetery" - Harold Wilson
Ni wapi MWK aliposema kuwa anaongelea mwezi wa siku na sio mwezi wa wiki? wewe umeuliza swali lakini baadaye kwenye post yako nyingine ukasema kuwa MWK hakusubiri mwezi upite ndiyo amkosoe Kikwete.
Wewe ndiyo ulitakiwa kusoma alichoandika MWK kabla ya kuanzisha thread ambayo imekuumbua na kukuaibisha hapa.
hata hivyo hapajaharibika neno.Mwafika kaona hapana jamaa anazidi ku bore akaamua kuingia nuke sasa kuna ubaya hata kama siku zilibakia chache ili mwezi ufike ?
Hivi kumbe kuna mwezi wa wiki na mwezi wa siku!
Kujadiliana na wewe Mgaya ni kupoteza muda, upeo wako ni mdogo. Nasikitika kukwambia hivyo.
"We make decesions from facts; when facts change, we change decesions"
Asha