Ni kweli mkuu!
Pia siamini kuwa Mwafrika ana akili ndogo.
Kuna member mmoja kaandika hapa kuwa nchi nyingi za Asia ktk miaka ya 1960, zilikuwa ktk viwango vya uchumi sawa na baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Tanzania. Najiuliza, hivi akili za Waafrika zilianza kupungua kuanzia 60's kwenda mbele?
Tatizo letu kubwa ni: UZEMBE, KUTOWAJIBIKA, UVIVU, ELIMU DUNI & UBINAFSI.
Siamini sana kama Mungu aliwapa akili ndogo Waafrika!
Huu UZEMBE, KUTOWAJIBIKA, UVIVU, ELIMU DUNI & UBINAFSI ni matokeo ya kuwaruhusu watu wasio na upeo wa kufikiri kutuamulia mambo ya msingi.
Baadhi ya viongozi wetu ni wanyonyaji wapumbavu tu wanofikiri kuwa wamechukua nafasi ya wakoloni dhidi ya waafrika wenzao na kwa bahati mbaya walipata na wanaendelea kupata nafasi zao kwa sababu za kihistoria (kurithi), kupindua na taratibu nyingine za hovyo za kuchaguana na kuteuana!