Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniphace Mwabukusi, amevitaka vyombo vya dola kuhakikisha kuwa mwanaharakati Mdude Nyagali anapatikana akiwa hai, huku akilaani vikali kauli ya kutolewa zawadi ya Shilingi milioni tano kwa atakayesaidia kupatikana kwake akiwa hai au mfu.
“Tumesikia na kuona maafisa wa polisi kutoka Makao Makuu wakishughulikia suala la Mdude, lakini pia tumeshuhudia tangazo lililosambazwa mitandaoni kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akiahidi zawadi ya Shilingi Milioni Tano kwa atakayefanikisha kupatikana kwa Mdude – eti akiwa hai au amekufa. Hili haliingii akilini,” amesema Mwabukusi kupitia chapisho lake katika mtandao wa X siku ya Jumanne.
Amesisitiza kuwa Mdude siyo jambazi, mwizi wala mhalifu wa kawaida, bali ni mwanaharakati ambaye adui zake wakuu ni wale wasio na uvumilivu wa kukosolewa.
“Msimamo wetu kama Rafiki za Mdude ni mmoja: Tunamtaka Mdude akiwa hai. Kama kuna kosa lolote, ashitakiwe kwa mujibu wa sheria. Hatuwezi kuvumilia taifa linalogeuka kuwa la mateso na vitisho kwa wanaoikosoa serikali,” ameongeza.
Aidha Mwabukusi ametahadharisha kuwa uvumilivu wa wananchi unafikia ukingoni, na kama ukweli kuhusu kupotea kwa Mdude hautatolewa haraka, hatua kali zaidi zitachukuliwa.
“Tunaendelea kujitahidi kuwa na hekima kabla ya kufikia ukomo wake. Bila Mdude na majibu yanayoeleweka kuhusu nani anawateka Watanganyika, punde tutafikia mahali pa kuchora mstari na kutafuta suluhisho mikononi mwetu. Mungu atakuwa upande wetu, Katiba itakuwa upande wetu, sheria itakuwa upande wetu, na jumuiya za kimataifa zitakuwa upande wetu”, ameeleza huku akimalizia kwa maneno yenye hamasa kubwa: “Sisi siyo njiwa tunduni, sisi ni tai kichaa.”
Siku ya Jumatatu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dkt. Juma Homera alisema kuwa tayari amelielekeza Jeshi la Polisi kuongeza jitihada za kuwatafuta wahusika waliomshambulia kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mdude Nyagali, huku akiahidi Tsh Milioni 5 kwa atakayesaidia kumpata kada huyo alipo akiwa hai au amekufa.
Akizungumza baada ya viongozi wa CHADEMA mkoani humo na Kanda ya Nyasa kufika ofisini kwake kujua hatua zilizochukuliwa, Dkt. Homera alisema yupo pamoja na chama hicho kuhakikisha
Source: Jambo TV
Soma pia Pre GE2025 - RC Mbeya atoa TSh 5 Milioni kwa atakayetoa taarifa za Mdude, aagiza Polisi kuwasaka waliomteka
“Tumesikia na kuona maafisa wa polisi kutoka Makao Makuu wakishughulikia suala la Mdude, lakini pia tumeshuhudia tangazo lililosambazwa mitandaoni kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akiahidi zawadi ya Shilingi Milioni Tano kwa atakayefanikisha kupatikana kwa Mdude – eti akiwa hai au amekufa. Hili haliingii akilini,” amesema Mwabukusi kupitia chapisho lake katika mtandao wa X siku ya Jumanne.
Amesisitiza kuwa Mdude siyo jambazi, mwizi wala mhalifu wa kawaida, bali ni mwanaharakati ambaye adui zake wakuu ni wale wasio na uvumilivu wa kukosolewa.
“Msimamo wetu kama Rafiki za Mdude ni mmoja: Tunamtaka Mdude akiwa hai. Kama kuna kosa lolote, ashitakiwe kwa mujibu wa sheria. Hatuwezi kuvumilia taifa linalogeuka kuwa la mateso na vitisho kwa wanaoikosoa serikali,” ameongeza.
Aidha Mwabukusi ametahadharisha kuwa uvumilivu wa wananchi unafikia ukingoni, na kama ukweli kuhusu kupotea kwa Mdude hautatolewa haraka, hatua kali zaidi zitachukuliwa.
“Tunaendelea kujitahidi kuwa na hekima kabla ya kufikia ukomo wake. Bila Mdude na majibu yanayoeleweka kuhusu nani anawateka Watanganyika, punde tutafikia mahali pa kuchora mstari na kutafuta suluhisho mikononi mwetu. Mungu atakuwa upande wetu, Katiba itakuwa upande wetu, sheria itakuwa upande wetu, na jumuiya za kimataifa zitakuwa upande wetu”, ameeleza huku akimalizia kwa maneno yenye hamasa kubwa: “Sisi siyo njiwa tunduni, sisi ni tai kichaa.”
Siku ya Jumatatu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dkt. Juma Homera alisema kuwa tayari amelielekeza Jeshi la Polisi kuongeza jitihada za kuwatafuta wahusika waliomshambulia kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mdude Nyagali, huku akiahidi Tsh Milioni 5 kwa atakayesaidia kumpata kada huyo alipo akiwa hai au amekufa.
Akizungumza baada ya viongozi wa CHADEMA mkoani humo na Kanda ya Nyasa kufika ofisini kwake kujua hatua zilizochukuliwa, Dkt. Homera alisema yupo pamoja na chama hicho kuhakikisha
Source: Jambo TV
Soma pia Pre GE2025 - RC Mbeya atoa TSh 5 Milioni kwa atakayetoa taarifa za Mdude, aagiza Polisi kuwasaka waliomteka
Inasikitisha sana tena sana. Yaani uende kwa wahusika utoe taarifa ya kuona maiti ya mtu ili upewe shilingi milioni tano!!!!. Kwanza itakupasa uwasaidie hao wahusika ni vipi umeiona hiyo maiti na kuitambua kwani tayari itakuwa imekwishaharibika vibaya. Tusilete mizaha katika mambo ambayo yanagusa uhai wa Binadamu wenzetu.
Aliyewahi kuwa Rais wa Utawala wa Makaburu kule nchini Afrika Kusini Bw. Pieter W. Botha pia alikuwa anamiliki Magenge ya Wahalifu wanaoteka Watu na kuua kwenye nchi hiyo. Lakini Wapiganaji wa Chama Cha ANC napo walipoanza mashambulizi ya kulipiza Visasi dhidi ya Watekaji hao na kuwaua, Watekaji wenyewe walikuwa wanaogopa kwenda kuwashambulia Watu mitaani. Hata Rais Botha mwenyewe aliingiwa na hofu baada ya kuona kwamba Watu Wake walikuwa wanauawa kwa wingi Sana.
Rais huyo aliogopa kwenda kufanyia kazi zake katika Ikulu yake iliyopo Mjini Pretoria, badala yake aliitelekeza Ikulu hiyo na kwenda kufanyia kazi zake katika Ikulu za Mafichoni zilizokuwepo Jijini Johannesburg ili kuwakwepa Wapiganaji wa ANC wasiweze kumfuatilia, kumfikia na kumshambulia yeye. Kamwe, alikuwa hafanyi kabisa Mikutano ya hadhara, muda mwingi sana wa Utawala wake alikuwa yupo mafichoni. Hata misafara yake ilikuwa haina Ving'ora, siku zote kabisa katika Utawala wake alikuwa anasafiri na misafara ya kimya kimya bila Wananchi kujua kwamba Rais wa nchi hiyo anapita.
Zaidi Sana alikuwa anapendelea zaidi kufanya mikutano ya ndani na Wazungu wenzake, Umma ulikuwa unajulishwa kupitia kwenye Matangazo ya kwenye Television.