kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,319
- 12,622
Nikiwa barabarani naendesha gari, Siti yangu ya mbele alikaa mjukuu wangu wa miaka 11. Mbele yetu kulikuwa na gari Ina namba za Zanzibar kwenye number plate yenye bendera ya Zanzibar. Mjukuu akaniuliza Ile gari mbona Ina namba za tofauti na hizi zetu, ni gari kutoka nchi gani?.
Nikamwambia ni gari kutoka Zanzibar. Akauliza kwani Zanzibar sio Tanzania? Nikamwambia Zanzibar ni Tanzania. Akaendelea kusema kwani T kwenye namba za magari inamaanisha Tanzania au Tanganyika? Nikamjibu inamaanisha Tanzania. Hakuuliza tena, bali nikamuona kama vile hakuridhika na majibu yangu anaona ninamchanganya TU.
Kuna watu ndani ya muungano waliondoa super league ikaonekana ni sawa, Kuna watu walitaka bendara Yao na wimbo wao wa taifa wakaonekana wako sawa TU, Kuna watu wakataka zibaki serikali mbili ya tanzania na ya Zanzibar ikaonekana ni sawa TU. Kuna watu wanafaidi sana ndani ya muungano lakini hawataki kuweka mambo yanavyotakiwa yawe kwa sababu zao TU.
Nikamwambia ni gari kutoka Zanzibar. Akauliza kwani Zanzibar sio Tanzania? Nikamwambia Zanzibar ni Tanzania. Akaendelea kusema kwani T kwenye namba za magari inamaanisha Tanzania au Tanganyika? Nikamjibu inamaanisha Tanzania. Hakuuliza tena, bali nikamuona kama vile hakuridhika na majibu yangu anaona ninamchanganya TU.
Kuna watu ndani ya muungano waliondoa super league ikaonekana ni sawa, Kuna watu walitaka bendara Yao na wimbo wao wa taifa wakaonekana wako sawa TU, Kuna watu wakataka zibaki serikali mbili ya tanzania na ya Zanzibar ikaonekana ni sawa TU. Kuna watu wanafaidi sana ndani ya muungano lakini hawataki kuweka mambo yanavyotakiwa yawe kwa sababu zao TU.