Mungu yuko wapi?

Kwani ni nini maana ya Hammaz?

Unajua kupinga/kubisha ni rahisi sana! Na ndiyo kazi ambayo inahitaji zero qualifications, ni kwa sababu kila mtu anaiweza.

"Majina lukuki na rejea za uongo za wanawazuoni." Hapa hujajibu, bali umetuhumu na ukifanya hivi hujengi bali unabomoa zaidi na kwa watu wanaohitaji manufaa kwenye mjadala wataona unafanya malumbano yasiyo na msingi. Maadamu umetuhumu sipo sawa ni jukumu lako kuleta kilicho sahihi.

Bw. Mkubwa uliyemkoti na kuzingumzia mimi amesema Mungu yupo juu ya Arsh, akaleta na uthibitisho wa aya kuwa baada ya uumbaji wa mbingu na ardhi kisha Mungu aka stawaa alal arshi. Aya ipo wazi kabisa na imeelezea kwa uwazi kabisa. Kwa namna hii Hammaz akaja na hadithi za wazi na niliziandika kwa haraka nyengine hazijakaa sawa kiuandishi lakini maudhui yake yapo wazi.

Mtume amesema mmoja wenu akiswali, asiteme mate mbele kwani Allah yupo mbele yake. Mwisho wa kunukuu.

Hadithi ambayo Allah akimuuliza mja wake kwa nini hakuenda kumzuru kipindi alipokuwa mgonjwa. Mja akauliza Allah nawe huumwa? Mungu akajibu fulani aliumwa, laiti ungelimzuru ungenipata kwake. Mwisho wa kunukuu.

Mtume anasema unaposujudu unakua karibu na Mungu. Mwisho wa kunukuu.

Hadithi hizo chache zipo wazi kabisa mithili ya aya aliyoitoa Bwana Mkubwa. Swali ni hili!

-Mungu ametajwa yupo juu ya Arshi
-Mungu yupo kwa wagonjwa
-Mungu yupo mbele unaposwali.
-Mungu huyu huyu ambaye ametajwa sehemu hizo zote nilizonukuu ukisujudu upo nae karibu.

Sasa Mungu yupo wapi?
 
Hiyo mbingu ya saba ipo wapi?

Kabala A'rsh haijaumbwa Allah alikuwa wapi?

Hizi Mbingu saba zipo wapi?
Haya maswali ni yana mantiki kubwa sana.

Ukitafakari mbingu zimeumbwa lakini zimeumbiwa kwenye nini? Hapa hauna jawabu!

Hivyo palipoumbiwa mbingu huwezi sema ni juu ama chini au kulia ama kushoto na si mbele wala nyuma. Pengine panaweza kusemwa pako juu kwa sababu dunia ipo chini.

Lakini hivi vyote dunia na mbingu na vilivyomo ndani yake vipo wapi? Itasemwa kwenye space. Space itasemwa lakini utakosa jawabu! Hivi vyote vimeumbwa pasipo na mahali yaani ombwe! Yaani hakuna kitu. Na kabla ya chochote Mungu alikuwepo yaani hakuna mbele, nyuma, juu, chini, kulia wala kushoto. Kwa tafsiri nyengine hakuna kilichomfunga wala kilichomkusanya (ametapakaa pasipo na kitu wala pasipo na mipaka).

Ikiwa mbingu na ardhi zimeumbwa pasipo na kitu na kuletwa kwenye hali ya ukitu, aliyekuwepo pasipo na chochote kuwepo ambaye hakukuwa na mipaka wala kilichomkusanya na akaileta hiyo mbingu na ardhi kwenye uwepo pa ambapo hakuna kitu yaani ime hang wapi, huwezi kusema yupo juu! Kwa sababu alikuwepo pasipo na chochote hata hiyo mipaka haikuwepo! Hivyo Mungu hahimiliwi na mipaka! Hayupo juu wala chini, wala kulia wala kushoto, wala mbele wala nyuma.

Hivyo nikiulizwa Mungu yuko wapi sitokuwa na jibu kwa sababu hakukuwa na mipaka iliyomfunga alikuwa ametapakaa. Yaani mahali popote tulipo Bwana Mkubwa yupo! Hata huko pasipo na mipaka ambapo alikuwepo kabla ya kuumba chochote alikuwa ametapakaa kwa kuwa hakuna mipaka hakuna kilichomfunga.

Hivyo nikiulizwa Mungu yupo wapi nitajibu; alikuwepo Mungu kabla ya sehemu au mahali, na alipokuwepo huko huko kabla ya sehemu ndipo alipoku huko huko!
 
Hayo majibu yako yanawezekana kama tu unaongelea Mungu kama alivyoelezwa na Biblia. Check majibu yangu mwanzoni mwa mada yatakuongezea kitu
 
Kitu kisichokuwa na mwanzo wala mwisho ni utata. Hapo utaelewaje? Wewe jua tu una mwanzo na mwisho, na kama kuna maisha baada ya kufa ni wakati wa kupata jibu kuhusu Mungu. Chapa kazi kwa kuzingatia "maisha ni mchezo".
 
The universe is the spirit of God. The spirit is everywhere but God he not in everywhere but sees all. Top dimension the deepest one as the souce of all things. But is not the place that some one can go as tour only your awereness can sense the source. What makes you breath in the spirit of God but not God. There is many many Gods but YHAWEH IS MOST HIGH GOD BECAUSE HES THE PART OF TRINITY.Spirit, fther and Son. Yan 963
 
Si binadamu pekee ndo walioumbwa na Mungu zipo sayari zingine pia zipo na watu na viumbe vingine. Mfano UFO ni viumbe halisi na Wana akili zaidi kuliko binadamu. Yote mapya Yaliyomo kwenye ulimwengu huu yamekuwepo kwenye sayari zingine miaka 3000 kabla. Sayari zingine wao wapo mbele yetu kitechnolojia miaka 3000 mbele
 
UFO sio viumbe mkuu bali ni kama ndege za aliens.kwenye summarian tablet ushahidisha kwamba alieans ndo walimuumba binadam na step zote na erros zilizo tokea zimerekodiw
 
 
PERFECT
,
 
hiyo arshi Ni lugha gani..?...tafsiri ya Hilo neno kwa kiswaili Ni ipi..?

Mkuu umesema apa kwamba chini ya arshi Kuna maji.
je..? Wakati maji yanabeba hiyo arshi yalikua juu yakitu gani..?
 
Sayari ya dunia pamoja na na galaxy yetu yenye sayari 9 (solar system) ni changa sana kiumri ukilinganisha na galaxy zingine. Kwenye uumbaji basi solar system ni ya Karibuni.
Hauna kashata hapo mkuu uniongeze!!?
 
Swali ni yupo wapi????
 
Kustawi??? Ukiwa na maana gani?? Hicho kiti cha enzi kina kazi gani??
 
Nikichoka na mihangaiko na pilikapilika za kazi basi huwa napenda ku peruse jf, kwani Jf ni burudani tosha ya mtu kujiliwaza.

🤣🤣🤣.

Mungu yupo wapi??--- hili ni swali la tatu kabla ya maswali--- Mungu ni nani/ni nini na Mungu katokea wapi??! , na maswali haya yamekujuja kwasababu tu kwamba imethibitika pasi shaka kwamba Mungu yupo na hii ni hatua ya msingi sana katika maendeleo ya kiroho na kimwili kwa mwanadamu.
 
^When men choose not to believe in God, they do not thereafter believe in nothing, they then become capable of believing in anything.^
--Gilbert Chesterton
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…