bless on
JF-Expert Member
- May 22, 2026
- 750
- 1,745
Kosa kubwa ambalo hawa Wazungu na Waarabu walilifanya wakati wanatunga hizi stori zao ni kumpaka rangi MUNGU aonekane ni mkatili. Fungua vitabu vyao uone
Kwenye hivyo vitabu vyao, Mungu anaangamiza mauaji ya halaiki na huyo huyo anabariki.
Kwenye hivyo vitabu, Mungu anasema yeye ndiye anayeleta maafa na uovu (Isaya 45:7).
Kwenye hivyo vitabu, Mungu anamtuma pepo mchafu kutesa watu.
Walichokosea ni kumfanya Mungu aonekane mkatili na muangamizaji, wakimpa sifa ambazo ninyi mnasema ni za Shetani, kumbe ni wao ndio wamechanganya madesa.
Badala ya kumfanya MUNGU kuwa MWEMA kwa asilimia mia moja Mungu wa nuru, amani, na upendo usio na masharti wakachanganya roho ya kikatili ndani yake ili watutawale.
Wazungu na Waarabu walitengeneza movie ya kutisha. Wamemweka Mungu upande mmoja na kumpa kazi ya kutesa na kuangamiza watu, halafu wakamweka Shetani upande mwingine kama kisingizio.
Mungu aliyeandikwa kwenye Biblia yenu na Kurani yenu, ambaye mnamtetea ni mhusika aliyetungwa na wageni akiwa na sifa za kikatili.
Walipaswa kumuacha Mungu awe MWEMA pekee, lakini kwa sababu walikuwa na ajenda za kututawala, wakamtengeneza Mungu anayefanana na ukatili wao wa kikoloni na kibeberu.
Mungu yupo na ni mwema 100% Lakini sio huyo wa kwenyekaratasi zilizotungwa na wageni kuja kutuvuruga akili zetu!..
Hebu someni hivi vifungu vyenu muone jinsi walivyomdhalilisha Mungu na kumfanya kuwa muangamizaji.
Kutoka 32:27 Mungu anawaambia watu wauane, kaka amuue ndugu yake!
1 Samweli 15:3 Mungu anaamuru mpaka watoto wachanga na wanyama wauawe!
Kurani Inasema Nitatia hofu katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo, na wapigeni katika kila ncha ya vidole."
Hivi kweli? Huyu ndiye Mungu mnayemsujudia? Huyu ni Mungu au ni jenerali wa vita wa Kiarabu au Kizungu? Hapa ndipo walipochemsha! Wangemfanya MUNGU kuwa MWEMA pekee, Mungu ambaye ni nuru tupu, asiye na chembe ya ukatili, tusingekuwa hapa tunabishana leo.
Hivi vitabu vililetwa kututawala na kutuliza amani duniani kwa kutumia hofu. Wazungu na Waarabu walijua fika kuwa ili kumfanya binadamu awe mtumwa mnyenyekevu, ni lazima umtengenezee hofu ya kitu asichokiona.
Kwenye hivyo vitabu vyao, Mungu anaangamiza mauaji ya halaiki na huyo huyo anabariki.
Kwenye hivyo vitabu, Mungu anasema yeye ndiye anayeleta maafa na uovu (Isaya 45:7).
Kwenye hivyo vitabu, Mungu anamtuma pepo mchafu kutesa watu.
Walichokosea ni kumfanya Mungu aonekane mkatili na muangamizaji, wakimpa sifa ambazo ninyi mnasema ni za Shetani, kumbe ni wao ndio wamechanganya madesa.
Badala ya kumfanya MUNGU kuwa MWEMA kwa asilimia mia moja Mungu wa nuru, amani, na upendo usio na masharti wakachanganya roho ya kikatili ndani yake ili watutawale.
Wazungu na Waarabu walitengeneza movie ya kutisha. Wamemweka Mungu upande mmoja na kumpa kazi ya kutesa na kuangamiza watu, halafu wakamweka Shetani upande mwingine kama kisingizio.
Mungu aliyeandikwa kwenye Biblia yenu na Kurani yenu, ambaye mnamtetea ni mhusika aliyetungwa na wageni akiwa na sifa za kikatili.
Walipaswa kumuacha Mungu awe MWEMA pekee, lakini kwa sababu walikuwa na ajenda za kututawala, wakamtengeneza Mungu anayefanana na ukatili wao wa kikoloni na kibeberu.
Mungu yupo na ni mwema 100% Lakini sio huyo wa kwenyekaratasi zilizotungwa na wageni kuja kutuvuruga akili zetu!..
Hebu someni hivi vifungu vyenu muone jinsi walivyomdhalilisha Mungu na kumfanya kuwa muangamizaji.
Kutoka 32:27 Mungu anawaambia watu wauane, kaka amuue ndugu yake!
1 Samweli 15:3 Mungu anaamuru mpaka watoto wachanga na wanyama wauawe!
Kurani Inasema Nitatia hofu katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo, na wapigeni katika kila ncha ya vidole."
Hivi kweli? Huyu ndiye Mungu mnayemsujudia? Huyu ni Mungu au ni jenerali wa vita wa Kiarabu au Kizungu? Hapa ndipo walipochemsha! Wangemfanya MUNGU kuwa MWEMA pekee, Mungu ambaye ni nuru tupu, asiye na chembe ya ukatili, tusingekuwa hapa tunabishana leo.
Hivi vitabu vililetwa kututawala na kutuliza amani duniani kwa kutumia hofu. Wazungu na Waarabu walijua fika kuwa ili kumfanya binadamu awe mtumwa mnyenyekevu, ni lazima umtengenezee hofu ya kitu asichokiona.
