Biblia imeandikwa kwa codes (mafumbo na mifano), huwezi kuelewa maudhui yake kama hutaweza gundua maan a halisi za mifano. biblia yenyewe inaweza kueleza maana ya kila fumbo lilipo ndani kosa huja pale tunapotumia uelewa wa mwanadamu kufafanua maneno ya Mungu. Yesu alikuja kwa mujibu wa maandiko lakini ajamu viongozi wakuu wadini walishindwa kumtambua na walipinga sana mafundisho yake na hata kumsulubisha. matendo 13:27.
Biblia imebeba ahadi ya Mungu (Agano) ambapo kwa kila mkristo anapaswa kulifahamu akishafahamu aamini the atende kwa kadiri ya Agano (mapenzi ya Mungu). Ni pale mtu anapoelewa Neno la Mungu ndipo anapoweza kuyafanya mapenzi yake na kupokea wokovu na uzima wa milele. mf, yesu alikuja kuhubiri juu ya ufalme wa mbinguni na ukisoma maandiko ameuzungumza mara nyingi kwa mifano na mafumbo swali la kujiuliza kama mkristo unaujua ufalme wa Mungu unafananaje. maandiko yanazungumza habari za mbinguni 1yoh 4:5