Mungu na tma hawana ushirika

Alwaz

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,122
10,829
Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania imezoea kuwazingua watanzania kwa utabiri wao wa hali ya hewa wenye maneno ya jumla jumla kama vile ukanda wote .......,manyunyu n.k.Mwaka jana walitabiri Elnino wanacnhi wakahama mabondeni matokeo yake ikawa ukame mkali uliokausha hata mabwawa ya kuzalidsha umeme.
Mwezi Disemba mwaka jana 2011 yalikuja mafuriko ambayo hayajapata kutokea tangu kabla ya ukoloni na watu zaidi ya 40 waliokuwa mabondeni Dar wakafa.Ukweli ni kuwa TMA hawakuwa na taarifa nayo.
Baada ya mafuriko hayo TMA walijitoa kimasomaso na kutabiri mafuriko zaidi na balaa mwishoni mwa mwaka.Mpaka leo iko kimya.Hali hii inathibitisha kwamba Mungu(Allah s.w.) hana ushirika wala biashara yoyote na TMA.
 
Back
Top Bottom