BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari ya uwapo wa mvua kubwa inayotarajiwa kunyesha katika mikoa 15 inayoweza kuleta athari ya mafuriko.
Mikoa iliyotajwa ni Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Tabora, Kigoma, Katavi, Dodoma, Singida, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa na Kusini mwa Mkoa wa Morogoro.
Taarifa iliyotolewa na TMA, ilisema mvua hiyo inaweza kuleta kiwango cha wastani cha athari ikiwamo mafuriko, baadhi ya maeneo kuzungukwa na maji na kuharibu shughuli za kiuchumi.
Aidha, taarifa ilisema mvua ilitarajiwa kunyesha kwa siku tatu kuanzia jana hadi kesho katika mikoa hiyo na kuwambukusha wananchi kuchukua tahadhari na kujiandaa kwa kununua mahitaji ya muhimu na kuweka ndani.
Julai 29, mwaka huu, TMA ilitangaza ujio wa El-Nino katika kipindi cha msimu wa vuli iliyotatarajiwa kunyesha kuanza Oktoba hadi Desemba, mwaka huu na kutoa angalizo kuwa, inaweza kusababisha athari katika maeneo mbalimbali.
Mikoa iliyotajwa ni Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Tabora, Kigoma, Katavi, Dodoma, Singida, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa na Kusini mwa Mkoa wa Morogoro.
Taarifa iliyotolewa na TMA, ilisema mvua hiyo inaweza kuleta kiwango cha wastani cha athari ikiwamo mafuriko, baadhi ya maeneo kuzungukwa na maji na kuharibu shughuli za kiuchumi.
Aidha, taarifa ilisema mvua ilitarajiwa kunyesha kwa siku tatu kuanzia jana hadi kesho katika mikoa hiyo na kuwambukusha wananchi kuchukua tahadhari na kujiandaa kwa kununua mahitaji ya muhimu na kuweka ndani.
Julai 29, mwaka huu, TMA ilitangaza ujio wa El-Nino katika kipindi cha msimu wa vuli iliyotatarajiwa kunyesha kuanza Oktoba hadi Desemba, mwaka huu na kutoa angalizo kuwa, inaweza kusababisha athari katika maeneo mbalimbali.