Mungu Mlinde Dr. Slaa Aiokoe Tanzania

Mungu Mlinde Dr. Slaa Aiokoe Tanzania

udini upo, unaendelea, na wadini kama hawa wataendelea kuwepo!.

Mwanafunzi wa Ilunga naona umerudi jukwaani kushabikia udini; hivi huyu slaa kwenye bible ametajwa kwenye kitabu gani mpaka kila jina lake linapotajwa ukimbilie kwenye udini? Matendo yake ndiyo yanayomsuta kwa dini slaa haijui na kumhusisha udini kuwatusi waumini waadilifu.

Chama
Gongo la mboto DSM
CC Ritz
 
Last edited by a moderator:
DR Wilbroad Peter Slaa(Padri Mstaafu) Phd holder in Theology! Kimsingi yeye kasomea mambo ya kanisani kama kuongoza misa,kushika rosali,kuongoza sala ya watu kutubu,kuimba nyimbo za salamu maria,kuendesha mikutano kwenye vigango na parokia,kufungisha ndoa za mitaguso,kuombea ekaristi takatifu,kuongoza ibada ya majivu na mitende,kuongoza ibada za kipaimara.....Hivi Tanzania tunachagua Padri kwa Kazi ya Kuongoza Taifa kwa Ibada? Nchi yenye watu wa dini mbalimbali!
 
he is already blessed....aya mashetan ccm wangesha mmaliza sema ni mko wa Mungu tu...viva chadema glory Slaa
 
anayechagua wazinifu amelaaniwa milele, anayeunga mkono wanaolisha watu sumu ni laana kwake na kwa mungu

Hivi riz 1 na miraji ni watoto wa mama salma?
hakika nawe u ktk laamana maana ulimchagua mzinifu mng'oa kucha kwa mlaizi.
 
hivi huyu slaa kwenye bible ametajwa kwenye kitabu gani mpaka kila jina lake linapotajwa ukimbilie kwenye udini? Matendo yake ndiyo yanayomsuta kwa dini slaa haijui na kumhusisha udini kuwatusi waumini waadilifu.

Chama
Gongo la mboto DSM
CC Ritz

Hee!.. Viongozi wa siasa wanatajwa kwenye bible? Kwenye Koran je?
 
DR Wilbroad Peter Slaa(Padri Mstaafu) Phd holder in Theology! Kimsingi yeye kasomea mambo ya kanisani kama kuongoza misa,kushika rosali,kuongoza sala ya watu kutubu,kuimba nyimbo za salamu maria,kuendesha mikutano kwenye vigango na parokia,kufungisha ndoa za mitaguso,kuombea ekaristi takatifu,kuongoza ibada ya majivu na mitende,kuongoza ibada za kipaimara.....Hivi Tanzania tunachagua Padri kwa Kazi ya Kuongoza Taifa kwa Ibada? Nchi yenye watu wa dini mbalimbali!

Weweee!... Hivi anayeongoza sasa si kiongozi wa dini? ..hakuna mtu asiye na mafunzo ya dini yake?
Hata JK kaificha title ya Alhaj na tena taaluma za kuongoza dini si lazima mtu akeshe mahali.. Ujuzi alionao JK katika dini ni mkubwa kuliko baadhi ya masheikh!
Tumeongozwa na mashehe wengi tu.. Sheikh Abeid Amani Karume na Sheikh Ali Hassan Mwinyi.
Acha kuligawa taifa.
 
Watoto wa ilunga wanajenga misikiti Oman wakimaliza muda wao wanenda kupumzika.
 
Hee!.. Viongozi wa siasa wanatajwa kwenye bible? Kwenye Koran
je?

Alaa kumbe!!! slaa ni kiongozi wa siasa sasa inakuwaje tunapomjadili kiongozi wa siasa ukimbilie kusema ni udini? Mimi nilidhani slaa ni nabii ametajwa kwenye Biblia takatifu na ndio sababu nilikuuliza huyu nabii mpya kaandikwa kwenye kitabu kipi?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Alaa kumbe!!! slaa ni kiongozi wa siasa sasa inakuwaje tunapomjadili kiongozi wa siasa ukimbilie kusema ni udini? Mimi nilidhani slaa ni nabii ametajwa kwenye Biblia takatifu na ndio sababu nilikuuliza huyu nabii mpya kaandikwa kwenye kitabu kipi?

Chama
Gongo la mboto DSM

Hujishitukii.. Tangu mwonzo nime-quote vielelezo vya dhahiri ambavyo wewe na wenzako mmeacha njia na kushadadia udini.
 
Hujishitukii.. Tangu mwonzo nime-quote vielelezo vya dhahiri ambavyo wewe na wenzako mmeacha njia na kushadadia udini.
Wewe mwanafunzi wa Ilunga ndio umeshadadia udini; mimi nmjadili mwanasiasa laghai slaa; sasa wewe kama una hisia zako za kidini huo mpango wako hapa mimi siasa tupu udini hauna nafasi katikaa ubongo wangu.
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Mleta mada kama humjui vizuri huyu babu unae muombea alindwe, hemu soma hapa ili wewe mwenyewe uiondoe thread yako;

i) Huyu babu ni muasi wa upadre.

ii) Mwizi wa wake za watu.

iii)Mbadhilifu na fisadi wa mali za chama.

iv) Mpenda machafuko na vurugu.

Na mengine mengi...

Niwe mkweli tu, sijaona zuri la huyu babu.

Mwanaume aliyeibiwa mke yupo hai? Sasa ametafuta mke mwingine? Alienda mahakamani?
 
Nimekuwa mwana CCM maisha yangu yote. Nakiri kwamba chama changu kimeleta umasikini na matatizo ya kutisha kwa Watanzania. CCM imekuwa ni hatari kuliko hata Ukimwi, kwani inawaua na kuwatesa raia wake bila huruma. CCM na serikali yake inatumia Polisi kungoa watu kucha bila ganzi. Wokovu tulionao leo, ni Dr Slaa au Mwakyembe. Katika dhoruba tuliyonayo ndani ya CCM, Dr. Mwakyembe hana ujanja kuweza kuliongoza nchi. Nyangumi ndani ya CCM watammeza. Tafadhalini watanzania wapenda amani. Tushirikiane, kuakikisha Dr. Slaa tunamlinda asidhuriwe na CCM.
Umesema vyema: ila endelea kusoma madongo ya majambazi na majangili na vibaraka wao waliobakia huko watakavyokukashifu!
 
DR Wilbroad Peter Slaa(Padri Mstaafu) Phd holder in Theology! Kimsingi yeye kasomea mambo ya kanisani kama kuongoza misa,kushika rosali,kuongoza sala ya watu kutubu,kuimba nyimbo za salamu maria,kuendesha mikutano kwenye vigango na parokia,kufungisha ndoa za mitaguso,kuombea ekaristi takatifu,kuongoza ibada ya majivu na mitende,kuongoza ibada za kipaimara.....Hivi Tanzania tunachagua Padri kwa Kazi ya Kuongoza Taifa kwa Ibada? Nchi yenye watu wa dini mbalimbali!
Nape amerudi na mafungu kibao! mtalipwa hadi 2015? hongereni!!! vilaza!!!!!!
 
Wewe mwanafunzi wa Ilunga ndio umeshadadia udini; mimi nmjadili mwanasiasa laghai slaa; sasa wewe kama una hisia zako za kidini huo mpango wako hapa mimi siasa tupu udini hauna nafasi katikaa ubongo wangu.
Chama
Gongo la mboto DSM
CHAMA ndiyo senior fellow wa NAPE ndiye mlipaji wa walinzi wa majangili na majambazi wa CCM
 
Not to be a Red comrade or anything.

Mentality nzima ya "Mungu Mlinde Dr. Slaa Aiokoe Tanzania" ina matatizo lukuki, neno kwa neno.

Ukianza kwa mungu tu una deal na a hoax. Mungu hayupo. Kwa hiyo habari nzima ya mungu kutoa ulinzi ni ushairi shayiri tu.

Tanzania ina umaskini mkubwa kwa sababu ya kukataa uchunguzi na kwenda na imani imani tu, mojawapo ya msingi kabisa inayotufanya tuwe masikini ni hii ya mungu.

Watu wanaoamini kuwapo kwa mungu ni rahisi zaidi kukubali kuwa katika utawala dhalili usioheshimu haki za msingi za binadamu, kuliko wale ambao hawaamini kuwapo kwa mungu. Mungu analeta excuses kibao za kukubali udhalili. Kuanzia "utapewa malipo peponi" mpaka "watiini watawala maana wamewekwa na mungu".

Kwa hiyo kama unataka Tanzania iendelee ondoa habari za mungu katika mawazo kwanza. Mungu ni tatizo Tanzania, si suluhisho.

Mlinde? Of course kama mungu hayupo hawezi kumlinda, lakini hata kama angekuwapo. Asipomlinda - short of against death- na kumpa majaribu zaidi ndo tutamjua kama ni kiongozi bora au anaelea kwa sababu ya hali nzuri tu. Ayubu hakuthibitisha imani yake na uthabiti kwa kulindwa na mungu, alithibitisha hayo kwa kutolindwa na mungu.

Aiokoe? Kwa nini Tanzania itake mtu wa kuiokoa? Huyu Dr. Slaa ni nani mpaka aiokoe Tanzania? Yeye ni Masiha au Mahdi gani huyu?

Uongozi wetu hauhitaji charismatic figures wa kutuokoa, hatuhitaji top down leadership. Hii ina introduce a single point of failure. We have been there, done that, bought the T-Shirt to show. It is written "Nyerere, baba wa Taifa" aka Mchonga aka Haambiliki.

Kwa nini tutake strongman mwingine badala ya kutaka a grassroots empowerment? Kwa nini tusitake ushirikishwaji wa umma zaidi? Kwa nini tusitake wabunge machachari zaidi wanaohuishwa na jumuiya thabiti zenye uelewa wa mamabo zaidi?



Ndugu yangu argument zako nazo zimekaa kishabiki zaidi kuliko dhana nzima unayoipinga na kutaka kutuaminisha. Unaposema mungu hayupo unakosea kwa sababu kuna mungu wengi sana ambao kwa wingi wanaitwa miungu! Chochote kile mtu anachoamini, iwe ni jiwe, mti, mlima na sanamu kadha wa kadha kwake mtu huyo ni mungu. Kwa hiyo unaposema mungu hayupo (existence)sikuelewi japo najua miungu hiyo inaweza kuwa haisaidii chochote!!!

Lakini dhana ya mleta uzi ni kuhusu Mungu wa mbinguni ambaye pia huwezi kutushawishi tuamini hayupo bila kutupa ushahidi kitu ambacho vilevile ni subjective. Mwishowe tutaishia kukutaka ututhibitishie kama kweli hayupo na hapo tutatumia muda mwingi kubishania facts ambazo sio lengo la uzi huu.

Mapungufu mengine katika hoja zako ni kuwa watu wenye kuamini uwepo wa Mungu huishia kukubali tawala dhalimu na zisizo za kidemokrasia lakini unasahau kuwa hakuna utawala wowote wa Mungu unaopaswa au kuruhusiwa kuendekeza wizi, rushwa, dhulma uvivu na kadhalika kwa kuwa vitu hivyo ni dhambi. Na kuhusu demokrasia, sijui kwa nini unashindwa kusoma historia ukagundua kuwa nchi nyingi zilizokana/zinazokana uwepo wa Mungu huishia kuongozwa na udikteta mfano nchi nyingi za ukomunisti!

Mwisho niseme tu kama lengo lako ilikuwa ni kutaka Watanzania tusiwe na utegemezi katika viongozi kutuletea maendeleo na badala yake tuyatafute sote kwa pamoja kwa kukuza taasisi za kijamii, hilo naungana na wewe lakini usihusishe na imani ya watu kwa Mungu.

Kwa hiyo si kweli kwamba Mungu ni tatizo, tatizo ni kutokuwepo kwa imani thabiti juu ya Mungu ambayo ingetuondolea uvivu, wizi wa mali za umma, ubinafsi, rushwa, dhulma, na madudu yote ambayo katika vitabu vya dini vimetajwa kama dhambi.
 
Ndugu yangu argument zako nazo zimekaa kishabiki zaidi kuliko dhana nzima unayoipinga na kutaka kutuaminisha. Unaposema mungu hayupo unakosea kwa sababu kuna mungu wengi sana ambao kwa wingi wanaitwa miungu! Chochote kile mtu anachoamini, iwe ni jiwe, mti, mlima na sanamu kadha wa kadha kwake mtu huyo ni mungu. Kwa hiyo unaposema mungu hayupo (existence)sikuelewi japo najua miungu hiyo inaweza kuwa haisaidii chochote!!!

Unaanza kwa risala ndefu sana wakati unajua kabisa haihusiki, inaonekana kuchonga ni aina ya burudani kwako.

Kwanza kabisa naomba unielezee undugu wetu ukoje. I am not one for undugu wa lip service katika nchi ambayo undugu unatoweka faster than the speed of light, defying the known natural speed limit. Kwa hiyo kabla ya kuni patronize na undugu, naomba unieleze undugu wetu ukoje, maana huwezi hata kusema ni ndugu katika imani ya Yesu/ mungu, kwani sina imani hiyo.

I extract exactitude. Fellow JF member? yes. Ndugu? I don't know about that. Waswahili walisema "Mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba".

Undugu mwingi hufuga umasikini, kwani "Mtegemea cha ndugu, hufa masikini". So let's be very clear on that, sio kila mtu anapenda undugu ndugu wa jumlajumla.

Lakini dhana ya mleta uzi ni kuhusu Mungu wa mbinguni ambaye pia huwezi kutushawishi tuamini hayupo bila kutupa ushahidi kitu ambacho vilevile ni subjective. Mwishowe tutaishia kukutaka ututhibitishie kama kweli hayupo na hapo tutatumia muda mwingi kubishania facts ambazo sio lengo la uzi huu.

Mwenye kuthibitisha siku zote ni yule anayesema kitu kipo, si yule anayesema kitu hakipo.

Mapungufu mengine katika hoja zako ni kuwa watu wenye kuamini uwepo wa Mungu huishia kukubali tawala dhalimu na zisizo za kidemokrasia

Naam, na nimekupa vifungu hapo juu, na vingine zaidi vipo kama unataka. The very godhead idea in it's Abrahamic manifestation is that of a repressive regime, so if one accepts that jurisprudence, why not accept of one bestowed on a demigod on earth "by the mandate of heaven". There is a reason all the oppresive Paharaohs and Chinese dynasties used this stamp to get mass approval. Read history.

lakini unasahau kuwa hakuna utawala wowote wa Mungu unaopaswa au kuruhusiwa kuendekeza wizi, rushwa, dhulma uvivu na kadhalika kwa kuwa vitu hivyo ni dhambi.

Nikisema siamini kwamba mungu yupo, siwezi kusahau kuwa hakuna utawala wowote wa mungu unaopaswa kuruhusiwa kuendeleza wizi etc.

Ntasahau vipi kitu kisichokuwapo? Utawala wa mungu ndo upi huo? Mungu ni nani? Kama mungu hayupo kutakuwaje na utawala wa mungu? Idea nzima ya "utawala wa mungu" ni ulaghai wa kuwachota binadamu akili.

Na kuhusu demokrasia, sijui kwa nini unashindwa kusoma historia ukagundua kuwa nchi nyingi zilizokana/zinazokana uwepo wa Mungu huishia kuongozwa na udikteta mfano nchi nyingi za ukomunisti!

Ukomunisti umekufa kifo cha asili, kati yangu na wewe unayeongelea Ukomunisti nani hasomi historia sasa?

Do not pigeonhole atheism into the constrains of Communism. I can be a Secular Humanist atheist who deplore Communism as much as I do deplore the intrinsic sheepishm in the autocratic "democracies" flagging god and country.

From the outset I disassociated myself with communist by saying "Not to be a Red Communist or anything". Do you know what that means? I am too much of a freedom lover to embrace communism.

Halafu suala likiwa kwamba wanaoamini mungu ni rahisi kuwa cajoled na tawala dhalimu, jibu liwe wanaoamini mungu na kukosa kuwa cajoled hivyo. Ukianza kuingiza Ukomunisti uliokufa utachekesha maana huna hata numbers za kufanya a reciprocal comparison. Ukomunisti umebaki wapi sasa? Korea ya Kaskazini na Cuba (Cuba nako uko kitandani kama baba yake Castro). How could you even draw a comparison?

Halafu usitake kuleta a shallow understanding of communism through the lens of hijacked communism. Ukienda kwenye Marxism-Leninism principles utaona jinsi watu wanavyokuwa empowered kufikiri critically na sio kufuata mkumbo tu.

Mwisho niseme tu kama lengo lako ilikuwa ni kutaka Watanzania tusiwe na utegemezi katika viongozi kutuletea maendeleo na badala yake tuyatafute sote kwa pamoja kwa kukuza taasisi za kijamii, hilo naungana na wewe lakini usihusishe na imani ya watu kwa Mungu.

Ukishakuwa na imani ya mungu tayari ushakuwa na utegemezi katika kiongozi kukuletea maendeleo.

Mgodi utaanguka na kufukia wachimba madini, badala ya kutafuta chanzo na kukifanyia kazi utasema kama alivyosema Kikwete "Kazi ya mungu". Tayari ushajenga imani ya kumtegemea mungu kabla ya kufanya kitu. Mambo yaende kwa kudra tu. Sasa hapo kitakachokufanya ushindwe kumtegemea kiongozi wa duniani unayemuona wakati unamtegemea mungu usiyemuona ni kipi?

Kwa hiyo si kweli kwamba Mungu ni tatizo,

Mungu ni tatizo kwa sababu imani ya mungu inapalilia utegemezi.Kwenda kwa kudra za mungu,mambo inshallah inshallah.

Mtakuwa na serikali dhalimu, badala ya kupanga kuing'oa, mtataka kuomba dua mungu aiondoe, kumbe mamimamu na mapadri ni mapandikizi wa usalama wa taifa ndo kwanza wanaanza kuwasema nani na nani analeta chokochoko.

tatizo ni kutokuwepo kwa imani thabiti juu ya Mungu ambayo ingetuondolea uvivu,

Imani ya mungu ndo uvivu wenyewe. Ukiulizwa maswali magumu usiyojua majibu yake, badala ya kujishughulisha kuyajibu, imani ya mungu inakupa jibu rahisi la kivivu "Mungu kataka hivyo". Kwisha kazi.

Kwa nini watu wavivu wa kufikiri wasiikubali sana imani ya mungu?

Ukiikataa imani ya mungu on the other hand, huwezi kuwa mvivu, kwa sababu itabidi ukatae jibu rahisi la "Mungu kataka hivyo" na kutafuta jibu lenye kina zaidi.

wizi wa mali za umma, ubinafsi, rushwa, dhulma, na madudu yote ambayo katika vitabu vya dini vimetajwa kama dhambi.

Vitabu vya dini ni kama methali za Kiswahili.

Hapa vinakwambia "haraka haraka haina baraka" pale "ngoja ngoja huumiza matumbo" hapa "mpende adui yako" hapa vinakwambia "jino kwa jino, jicho kwa jicho" vinaji contradict. Kwa hiyo mtu mwenye kufikiri atavisoma kama ushairi wa zamani ambao hauna consistency ya kusimama katika enzi hii.
 
Back
Top Bottom