Binadamu tunathibitisha mambo kupitia senses zetu tano ambazo wote tunazijua.
Linapokuja swala la Mungu, binafsi sijawahi kumuona, kumsikia, kumuonja, kumuhisi wala kusikia harufu yake.
Hii inanipa hitimisho kwamba Mungu ni dhana tu iliyoanzishwa na binadamu walipokosa majibu ya asili ya mambo mbalimbali. Kisha akaingizwa kwenye hadithi mbalimbali na kupewa sifa za mamlaka na zingine za kuogofya.
So naamini Mungu haexist physically ila dhana ya Mungu inaishi kwenye vichwa vya mamilioni ya watu duniani Kwa kuwa stori za Mungu zinasimuliwa toka utotoni na dhana ya Mungu imebidhaishwa na watu mbalimbali Kwa manufaa yao binafsi ya kisiasa, kiuchumi na kadhalika.