Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Umeniuliza inakuwaje Mungu si hai akaumba Kitu kisicho hai. Nimekujibu kwa kukuambia Ameumba Vitu vingi Visivyo na Uhai pia na Vilivyo na Uhai

Mawe/Michanga/Dhahabu hayana uhai ila kayaumba. Kwa Mantiki yako ili jiwe liumbwe Mungu angetakiwa asiwe hai ili aliumbe hilo jiwe.

Unaposema Mungu yu Hai Maana Yake Umemuweka Kama Kiumbe ulivyo wewe wakati Hayupo hivyo. Vilivyo na Uhai na Kuumbwa Hufa
So kwa akili yako wakati anaumba hivi vyote alikuwa Hai au amekufa?
 
Pole sana ndugu, maadam umeamua kuanza safari ya kumjua Mungu atakusaidia uendelee kumwelewa zaidi. Safari ndio umeianza lakini weka akili yako wazi kupokea michango ya wadau upate uelewa zaidi.

1. Mungu alimwumba mtu kwa mfano wake. (Udongo jumlisha pumzi ya Mungu).
2. Mungu aliumba mbingu na nchi na vyote viijazavyo.

Inawezekana vipi kisicho na uhai kiumbe vilivyo na uhai.

Mungu akasema......na ikawa. Kabla ya kusema nini kinatangulia. Ni kuwaza au mawazo. Kwahiyo mawazo (niite consciuosness kwa kizungu cha Uingereza) ndiyo kiini cha uhai. Leo wewe ukipoteza consciousness umekwisha.

Endelea kujifunza ndugu. Mungu yu hai na anaishi milele.
Haya umeyatoa wapi?
 
Mungu ni nini/nani? Je nawezaje kuuhisi uwepo (presence) yake?

Viumbe wa Mungu wote Wanamtegemea Mungu.

1. Unakula Chakula Kutoa katika Ardhi yake
2. Unapumua

Kama Unataka kuhisi uwepo wake Basi huwezi maana Yeye hana Mwili kama Ulionao wewe. Hisia za Kushika na Kuona Zinatoka Katika mfumo wako wa Fahamu ulio KATIKA mwili wako.
 
Ninatamani kuandika ila naona kama nitapoteza muda huyu jamaa anabeep mahali ambapo hata wewe ukisahau yeye hasaau kamwe atakuja kukulipa sawa na uzi huu tena umeujua ukweli ila umechelewa
 
Kumekuwa na Dhana POTOFU na Dhana Hii imewaharibia sana Akili watu wa madhehebu. Unakutana na Mtu anakuambia, Mungu wangu yu Hai

Kitu kilicho hai ni kiumbe tu. Mwenye Enzi Mungu yupo nje kabisa na Vinavyoishi, yeye aliviumba Viwe vinaishi na akaviweka Katika Sayari mbalimbali vikae huko

Yeye hakai na Viumbe vyake wala Hasaidiani mambo yake na Viumbe vyake alivyoviumba.

Kwahiyo ni makosa makubwa kumfananisha Mwenye Enzi Mungu na Uhai wa Viumbe vyake na kusema Eti Yeye yu Hai, kumpatia Sifa za Viumbe (anakaa, anasema, anatuma malaika, anatamaa, ana wivu n.k n.k ni Makosa na Upotofu mkubwa sana unaoendelea huko Wanakoabudu

Mmeambukizwa Imani za Viumbe waovu na Wenye dhambi (Mashetani, Malaika, Wachawi n.k) Na mnapokuwa mnamwabudu Mungu huyo mnamfananisha na Nyie mlivyo. Mnampa Sifa za Nyie mlivyo(uhai, tamaa, wivu, Utakaji wa vitu). Mungu hana Sifa za Ubinadamu wala sifa za kiumbe chake chochote kile


ASANTENI
Ila kuna uwezekano pia miungu ilikuwepo na ikaumba binadamu. Ila kwa bahati mbaya kama ambavyo iliweza kuwepo ikawa haipo tena sasa kwa njia zilizo nje ya uelewa wa binadamu, miungu imetoweka. Hayupo hata Mungu mmoja tena🙏🏿🤔
 
Viumbe wa Mungu wote Wanamtegemea Mungu.

1. Unakula Chakula Kutoa katika Ardhi yake
2. Unapumua

Kama Unataka kuhisi uwepo wake Basi huwezi maana Yeye hana Mwili kama Ulionao wewe. Hisia za Kushika na Kuona Zinatoka Katika mfumo wako wa Fahamu ulio KATIKA mwili wako.
Tatizo lako unadhani huo mwili wako ndiyo wewe. Utakesha unamtafuta Mungu na hautamwona kamwe.
 
Mwanadamu kumuwaza Mungu hutaweza kumpatia picha mwisho unaweza ukajikuta unakufuru tu.

MWENYEZI MUNGU YU HAI MILELE DAIMA.
Sasa ndugu yangu Mbona Wewe ushasema YU Hai Milele. Sasa si ushampatia Picha ambayo hata Ukiambiwa useme ana Uhai Gani hutoweza. Kitu kilicho HAI kina Kufa na Kina Mwisho wake kama Wewe binadamu ulivyo hai mana Yake Utakufa.

Sasa Hawa Viumbe waliowapotosha wamewaambia Pia Mungu Yu Hai yaani Wanajifananisha na Yeye. Ndio maana Wanampa sifa walizonazo. Utasikia Mungu wangu anaishi milele na milele kitu kinachoishi hakiwezi ishi Milele kitakuwa ndio mana ya Kuishi. Ukisema unaishi maana Yake unamuda mwili wako utazeeka na Kufa


Hivi ulishwahi kujiuliza hizi mbingu zimewezaje kuwa juu yetu pasi na kuwekewa nguzo yoyote ile unayoiona?

Ni nani anaezishikilia hizi mbingu zisitufunike tulio chini yake?

Wewe nani kakuambia hayo!? Nani kakuambia Mbingu ipo juu yako. Au hujui kwamba Hata Mbingu umeumbwa ni kiumbe na Itakufa Muda wake ukifika


Vp huyo anaezishikilia akisinzia sisi tuliochini yake tutakuwa katika hali gani?

Ukishajiuliza swali hili ndio utajua kuwa MUNGU yupo hai au amekufa!

Ndugu yangu Tipstipstor nani kakuambia Kuwa Mbingu zimeshikwa na Mtu. Au Pia wewe ni muumini wa Malaika mlinzi wangu. Kwamba Unaamini kwamba Kuna malaika yupo anakulinda. Hakuna Aliyeshikilia Mbingu wala Nini. Kila Kiumbe kimeumbwa na Kuweka Mahali kilipo kwa Muda wake na Ikifikia Hatua kitakufa na Kupotea hata Dunia Hii ina Muda Wake itapotea Na Wewe pia Una Muda Wako ukifika utazeeka Na Kufa

Nimeshajiuliza Na Nikuambie Mungu Hana Uhai wala Hajafa maana Vinavyokufa ni Viumbe pekee. Yeye Yupo Alipo na Hana Mwanzo wala Mwisho na Wala Hana Umbo unalofikiria wewe wala Binadamu yeyote maana hakuna Aliyewahi muona
 
Mungu ni dhana/imani.
Imani hii ni tofauti na imani nyingine, hii ina uraibu kama wa kilevi au madawa ya kulevya...mtu akishaonja kuacha ni ngumu sana!
Kam ilivyo kwa mlevi wa pombe kwamba ukitaka kukosana naye mwaga pombe yake, hivyo hivyo kwa mlevi wa imani ya mungu ukitoka mtoane macho gusa mungu wake.

Kwenye hii imani/nadharia, watu wametofautiana kutegemea na mwenye kuamini amejengaje imani yake.

Wengine wanasema, Mungu ni UPENDO tu inatosha.
 
Ninatamani kuandika ila naona kama nitapoteza muda huyu jamaa anabeep mahali ambapo hata wewe ukisahau yeye hasaau kamwe atakuja kukulipa sawa na uzi huu tena umeujua ukweli ila umechelewa
Mungu hana chuki na Viumbe wake wenye Chuki ni wewe na Mimi. Na Majini na MASHETANI na malaika ambao ndio wanakuambia Mungu anachuki na ukimjadili anakuadhibu, usipompa Sadaka anakuadhibu, usipompa Zaka anakuadhibu

Mungu Hayupo kama Wewe unavyo chukulia na Alivyoandikwa kwenye Vitabu
 
Mungu hana chuki na Viumbe wake wenye Chuki ni wewe na Mimi. Na Majini na MASHETANI na malaika ambao ndio wanakuambia Mungu anachuki na ukimjadili anakuadhibu, usipompa Sadaka anakuadhibu, usipompa Zaka anakuadhibu

Mungu Hayupo kama Wewe unavyo chukulia na Alivyoandikwa kwenye Vitabu
UNAPOTEA
 
Unapoamini jambo lolote imani yako inakuunganisha na jambo hilo na muda huo unaanza kuona matokeo yake. Imani inaamsha na kuaksi mazingira, hali halisi na mipango yote inayoshabihiana na imani yako. Yote yanatokea kwa kadri au ukubwa wa imini yako kwani unashughulika na roho.

Hii ni karakana yako ambapo ulimwengu wako utauona katika mwelekeo wa imani uliyonayo na kila kitu kitatokea kama unavyoamini.

Watu wawili wanaweza kwenda kwa Mungu, mganga au mchawi wakafanikiwa au mmoja asifanikiwe mwingine akafanikiwa. Kwanini? IMANI......kubwa au ndogo.

Ukiamini uchawi utauona, ukiamini Mungu utamwona. Ukipanda bangi utaotesha na kuvuna bangi wakati huo ukipanda mahindi eneo hilo hilo utaotesha na kuvuna mahindi.

Imani yako itakufaa
 
Wewe ni Binadamu una uhai ila Unatengeneza magari na Vitu visivyo na Uhai kama Wewe. Muujiza wa Mungu umetenda hayo Yote umeumba

MALAIKA, MAJINI, MASHETANI, n.k nao wameumbwa kama Wewe na Hawaonekani na Hata Mchawi anakuja Kwako anachukua Vitu na Kukuwangia Ila Humuoni jiulize kwanza Hayo kabla Hujauliza muujiza wa Mungu umetendaje Haya Yote

Labda kama Huamini kama Huyo huyo aliyemuumba Malaika ndio kamuumba Jini na Wewe binadamu

Na pia Ujiulize kiliumbaje Mawe na Miamba Ambayo haina Uhai pia
Hayo mambo ya uchawi kwasasa kushadadia naona sawa na kushadadia uwezo mdogo wa kuchanganua na kutafakari changamoto mbalimbali za kimaisha.
 
Unapoamini jambo lolote imani yako inakuunganisha na jambo hilo na muda huo unaanza kuona matokeo yake. Imani inaamsha na kuaksi mazingira, hali halisi na mipango yote inayoshabihiana na imani yako. Yote yanatokea kwa kadri au ukubwa wa imini yako kwani unashughulika na roho.

Hii ni karakana yako ambapo ulimwengu wako utauona katika mwelekeo wa imani uliyonayo na kila kitu kitatokea kama unavyoamini.

Watu wawili wanaweza kwenda kwa Mungu, mganga au mchawi wakafanikiwa au mmoja asifanikiwe mwingine akafanikiwa. Kwanini? IMANI......kubwa au ndogo.

Ukiamini uchawi utauona, ukiamini Mungu utamwona. Ukipanda bangi utaotesha na kuvuna bangi wakati huo ukipanda mahindi eneo hilo hilo utaotesha na kuvuna mahindi.

Imani yako itakufaa
Kama imani ya mtu ina nguvu kiasi hiki Mungu wa nini sasa.
 
Ila kuna uwezekano pia miungu ilikuwepo na ikaumba binadamu. Ila kwa bahati mbaya kama ambavyo iliweza kuwepo ikawa haipo tena sasa kwa njia zilizo nje ya uelewa wa binadamu, miungu imetoweka. Hayupo hata Mungu mmoja tena
Kila Kiumbe kilichoumbwa na Mungu kilipewa mahali pa kukaa na Uwezo wa akili. Kutokana viumbe kupenda Kutawala mfano mzuri ni Ukoo wa Majini (shetwani ), malaika, elians na wengine upotoshaji ndipo unapoanza

Na hata Binadamu sasa tunataka kwenda Sayari zingine. Hao viumbe wengine wao walishakuja duniani muda mrefu na wakatupotosha na kuleta Teknolojia zao huku(kumbuka kuna Mambo yapo Duniani wanasayansi hawana Majibu yametokea wapi na Yamejengwa na Nani)

Viumbe hawa ndio wameleta mpaka hzii dini za upotoshaji zilizopo leo hii ambazo ndizo zinakuambia Mungu anataka Hiki na Ukimnyima anakulaani

Ndio hawa hawa wanawatokea manabii walioandikwa kwenye vitabu wanamwambia wasome kwa jina la Mola wao. Ndio hawa hawa wanakuja kwa njia ya Moto kuwaka kwenye Kichaka na Kuwaambia wavue viatu ni sehemu takatifu
 
Kila Kiumbe kilichoumbwa na Mungu kilipewa mahali pa kukaa na Uwezo wa akili. Kutokana viumbe kupenda Kutawala mfano mzuri ni Ukoo wa Majini (shetwani ), malaika, elians na wengine upotoshaji ndipo unapoanza

Na hata Binadamu sasa tunataka kwenda Sayari zingine. Hao viumbe wengine wao walishakuja duniani muda mrefu na wakatupotosha na kuleta Teknolojia zao huku(kumbuka kuna Mambo yapo Duniani wanasayansi hawana Majibu yametokea wapi na Yamejengwa na Nani)

Viumbe hawa ndio wameleta mpaka hzii dini za upotoshaji zilizopo leo hii ambazo ndizo zinakuambia Mungu anataka Hiki na Ukimnyima anakulaani

Ndio hawa hawa wanawatokea manabii walioandikwa kwenye vitabu wanamwambia wasome kwa jina la Mola wao. Ndio hawa hawa wanakuja kwa njia ya Moto kuwaka kwenye Kichaka na Kuwaambia wavue viatu ni sehemu takatifu
Mungu ni nani/nini?.
 
Babu zetu walio ishi na kufa kabla ya hivi vitabu havijaja,walimjua Mungu ?
Wakijua au wasijue wewe inakuhusu nini na imani au wokovu wako?

Let the dead bury their dead. Acha wafu wazikane wao kwa wao. Sio kazi yako kujua walikula nini walichamba na nini wakati karatasi laini za kuchambia hazikuwepo.

Wakati wako ni sasa unaposoma andiko hili wala sio dakika moja ilopita.

Usiniulize habar za babu yako aliishije. Ukitaka kijua aliishije katambike kaburini kwake na sijui hata kama ana muda wa kukusikiliza kwani hatujui huko alipo anafanya nini na wala yeye sidhani hata kama anajua wewe unaishije leo.

Huwa sijadili habari habari za wafu kuwa waliishije.
 
Back
Top Bottom