Kindimbajuu
JF-Expert Member
- Jul 8, 2009
- 710
- 248
Ni rahisi sana kuweka hili la uaminifu mbele, kwani ndilo lafikirika ktk kichwa cha binadamu zaidi. Wasiwasi wangu ni kuwa kama tatizo halitokani na kuto kua muaminifu je akiomba na kufunga Mungu atasikia kweli? Maana muombaji atakuwa anatumia wrong platform. Binafsi kama mwanaume nimewai pata tatizo hili na liligharimu mahusiano yangu, niliitwa mwongo tu na kila lugha iliyofanana na tatizo langu. Kama si viumbe waliojaliwa hekima kutoa msaada kindambajuu nisingelikuwa naandika hapa sasa.inauma sana kuitwa malaya wakati huo umalaya huwez kuufanya. Tuwe makini tuwasikilize wenzi wetu wakiwa na matatizo. Kuwahukumu kwenye njia ya uaminifu tu si sahihi. Naamini kitu ambacho kinamchanganya sana mwanaume ktk mahusiano ni yeye kushindwa kuonyesha uanaume wake. Ndo maana hawa watu wanao uza 'to increase power of men ' hawakosi wafuasi