Naomba msaada wenu mume wangu anacheat nifanyeje? mbaya zaidi na watu ambao wengine kawatambulisha kwangu,na ilikia hatua nilipokwenda jifungua alileta mpaka ndani nikiuliza tatizo nini hasemi sms kila siku godnight bby love u ukiuliza sina mana ya mapenzi nisaidieni wana jf nianye nini ?nami nianze cheat kama yeye au nifanye nini?
Dada kisa chako kinanisikitisha, najiona mimi kama wewe, japokuwa mimi ni mwanaume, lakini nakushauri ifuatavyo:
- Hebu jaribu kurudi nyuma katika historia ya maisha yako wewe na mume wako. Je, kabla ya kuoana, kulikuwa na maandalizi YA KUTOSHA kwa jini ya kuishi kama wanandoa? Je, maandalizi hayo yalifanyika chini ya msingi wa kidini au wa kimila? Hujaeleza kama wewe ni Mkristo au Muislam. Kila dini ina taratibu na misingi yake ya jinsi ya kuishi katika ndoa. Utazame, je, kulikuwa na maandalizi ya kutosha?
- Ninasema hivi kwa kuwa wengi wetu, sisi vijana wa leol, TUNAKURUPUKA na kuingia ndani ya ndoa huku tukiwa HATUJAFANYA MAANDALIZI ya aina yoyote yale ya jinsi ya kuishi katika ndoa. Ukweli ni kwamba, wanaume na wanawake wengi siku hizi wanaingia kwenye ndoa na kuendelea kuishi KANA KWAMBA bado hawako kwenye ndoa. Sijui imekuwa FASHENI au kitu gani. Mtu unaoa/unaolewa ili mradi tu uitwe Mr. au Mrs. Fulani, umevaa pete, basi, umependeza, lakini HUJUI MAANA YAKE!
- Hapo ndipo chanzo cha mtu kutoka nje ya ndoa kinapoanzia. Bwana yeye anajiendeshea maisha yake kana kwamba hana mke nyumbani. Anaenda huku na huko, anabadilisha wanawake kama mashati. Kinachomrudisha nyumbani, akitubu, mkia kaufyata nyuma, ubabe wote umeisha ni nini? UKIMWI! Keshaukwaa! Labda tena KISHAMWAMBUKIZA mke wake bila hata kujua. Anamwona mke wake kama kimada, lakini aliye ndani ya nyumba. Kwa hiyo hawezi kumtofautisha na yule wa nje. Wote sawa! Hapa, hata ile HOFU YA MUNGU haipo tena. Kama ingekuwa apo, ile amri ya "Usizini" isingevunjwa kabisa.
- Najua maneno haya ninayokuambia ni MAGUMU na YANATIA UCHUNGU, lakini ukweli lazima usemwe. Hakuna kufichaficha hapa. Tunaficha nini? Lengo letu ni kutafuta MARIDHIANO kati yako wewe na mume wako, umekuja kutuuliza UFANYE NINI? Sasa sisi tunakuambia... tuseme MIMI ninakuambia, kwanza ANZA KUJICHUNGUZA wewe mwenyewe.
- Hebu jiulize: Ni mara ngapi ulimwandalia mume wako chakula mezani? Ni mara ngapi uliandaa maji ya kuoga na kumwita mume wako, mkaingia wote bafuni, mkaoga pamoja?
- Jiulize: Ni mara ngapi ulimwambia mume wako: Nakupenda _______ (fulani). Nakupenda honey. Nakupenda switi!
- Jiulize: Ni mara ngapi ulimpokea mume wako aliporudi nyumbani akitoka kazini, na kumwambia: Pole mume wangu kwa kazi nyingi.
- Sasa jiulize: Ni mara ngapi yote haya, na mengine ambayo sijakuuliza, mume wako alikuwa anakufanyia, na labda wewe hukuyatilia maanani, kwa kuyaona "old fashioned"?
- Kumbuka, misingi ya kidini (kwa waumini wa Kikristo) ilihuishwa na tamaduni za makabila mbali mbali, baada ya tafiti mbali mbali kufanyika kuhusu uhuishaji huo wa mila na desturi, ili kuzioanisha na jinsi Kanisa la Kikristo linavyofanya kazi yake hapa nchini, HASWA kwa wanandoa. Kwa hiyo, yale ambayo vijana wa sasa wanayaona "ya kizamani", ni misingi ambayo wazazi wetu waliitumia ili kuishi kwa amani na maridhiano. Hakukuwa na ubaguzi wa nani "mkubwa" au "mdogo" ndani ya nyumba. Wote walikuwa sawa, walielewana, waliridhiana. Hakukuwa na ubabe.
- Utakuta siku hizi, binti anatoka kwenye familia yenye UWEZO, kwa hiyo anajua: Wikiendi naenda kwa Mama. Anasahau maana halisi ya "kuwa mwili mmoja" na mume wake. Naye mume kwa kuwa anampenda, anashindwa kumzuia, lakini anaumia moyoni. Anabaki mpweke. Mke anaenda kwa mama yake, kuanzia Ijumaa anarudi Jumapili. Mume anabaki na "beki tatu" nyumbani, unatarajia nini kitokee? Sasa hapo Shetani anaanza kazi yale. Baada ya "kutosheka" kwa "beki tatu" anaanza kutoka nje kabisa ya ndoa. Keshaisaliti, lakini Shetani keshamteka, akili haipo kwenye "network" yake. Hapo mawazo yote ni: Mie si naonekana -----? Mie si naonekana sina lolote? Yeye si anaona wazazi wake ni bora zaidi kuliko mimi? Haya, ngoja mie nikajirushe na washkaji, tukasake madem. Potelea mbali! Kufa kwaja!
- Safi sana! Shetani keshafanya kazi yake! Keshawamaliza WOTE!
Sasa dada, unaona kinachotokea hapo? Mie nimekupa "nusu" tu ya mkanda. Wewe hujatueleza kinagaubaga kinachoendelea ndani mwako. Lakini cha kwanza kabisa, BAADA YA KUTAFAKARI, ninakuomba ufanye hivi:
- Kwa IMANI YAKO, sali sana. Muombe Mungu akupe moyo wa uvumilivu na upendo. Sali sana!
- Kwenye sala zako MUOMBEE MUNGU amrejeshe MUME WAKO kwako, kwani Mungu ndiye aliyekupa mume huyo. Yaonekana bado wampenda, kwa hiyi huna budi kukumbuka kwamba UNAMPENDA na huna mwingine zaidi yake.
- Kauli yako ya kwamba kwa kuwa yeye amecheat na wewe ucheat IFUTE KABISA. Ok, amecheat, sawa, na wengine kawaleta hadi ndani. SAMEHE NA SAHAU. Fanya kwamba jambo hilo HALIJATOKEA, kwamba ni Shetani ndiye amempitia. Shetani ni ADUI WA KILA MWANADAM, kwa hiyo kila atubuye na kuungama dhambi zake husamehewa na kufutiwa dhambi hizo.
- Tafuta muda, weka mazingira, mwambie mumeo unataka mtoke outing. Toka naye outing, sijui kama bado unalea, lakini kama unaweza, hebu nendeni outing mara moja au mbili, fanya utoke naye outing hata kila wikiendi, kwa mwezi mmoja, kisha tazama nini itakuwa reaction yake.
- Pengine wewe ULIKUWA BUSY na kazi, hukupanga muda wa kufurahi na mumeo? Au labda yeye? Sijui. Wajua wewe. Jaribu kujikumbusha, mlivyokuwa wapenzi mlikuwa mnafanya nini? LAKINI USISAHAU KUOMBA NA KUSALI KILA SIKU! OMBA SANA! SALI SANA.
Mimi natarajia kwamba, maombi yako yatamrejesha mume wako nyumbani, na kama wewe ni Mkristo, basi, itakuwa HARAKA SANA. Kwa sasa uko naye, lakini Shetani ameshamteka, tena KAMTEKA SANA, ndio maana anadiriki hata kuwaleta hao vimada, wezi, nyumbani. La sivyo ANGEMUOGOPA MUNGU. Unahitaji sana kufanya maamuzi magumu: Uamue, ndoa imekushinda, uondoke.... sijui utaenda wapi, maana sioni utakapokwenda na sidhani utakuwa na maisha mazuri, kwani utakuwa umevunja ndoa ILIYOFUNGWA NA MUNGU! Kwa hiyo nakushauri, vumilia, kwa busara utakazopewa na Yesu Mwokozi, HAKIKA utafanikiwa. Nakutakia mafanikio mema ili ndoa yako idumu. Kumbuka: Kwa Mungu, HAKUNA linaloshindikana!
Nitakukumbuka kwenye Sala Zangu.
Ubarikiwe sana!
Amina!