Mume mwenza simuelewi ananitafutia jela

Mume mwenza simuelewi ananitafutia jela

Habari wadau
Naanza kuandika kisa hiki kwa maskitiko makubwa
Mwenzenu nina mke nimebahatika kuzaa nae mtoto mmoja lakini mke huyu wakati huo naanza nae mahusiano yetu nilimkuta na mtoto mmoja wa umri wa miaka 5

Kama mjuavyo nilivutiwa na bibie na sikuona uzito wa kumlea mtoto nilifurahi kujua huyu mke ni mlezi na waswahili wanasema ukipenda boga penda na ua lake

Mwezi uliokwisha aliibuka bwana mmoja asubuhi kabla ya mimi sijakwenda kwenye shughuli zangu akakaribishwa mimi nikatoka ukumbini nikamkuta huyu bwana amekaa na watoto wote wawili kwenye kochi, nikamuuliza mama watoto akanijibu nilikuwa nasubiri nikufahamishe huyu ni (baba john) si jina rasmi,nikamsalimia tukaletewa chai tukajumuika pamoja kunywa chai na maandazi tukaongea kuhusu maisha kidogo na akanieleza dhumuni la kufika hapa ni kumuangalia mwanawe ,siku zimekuwa nyingi nikawaacha mimi nikaondoka kuelekea kwenye mizunguuko yangu

Swali linalonisumbua kichwa huyu bwana alipajuaje hapa nyumbani na kwanini alikuja asubuhi hana shughuli huyu mtu, na pia hivi sasa nasikia mimi nikitoka na yeye anafika mara mbili kwa siku kuangalia mtoto na akifika anaacha mizigo anaondoka sasa juzi ndio ilikuwa kali nilikuta chupa za bia nikaambiwa nililetewa na mume mwenzangu na yeye ameshakunywa zake nikamuuliza mke akanijibu nisiwe na wasiwasi yule anampitia mwanawe na yeye ni mtu mzima hawezi kutuchanganya,lakini jamani mtu na mtuwe ni kama gari na mteremko

Ok kwa sababu ya likizo ya viroba nikajinoma bia lakini kwa shingo upande na kengele ya tahadhari ikinililia kichwani
Leo hii asubuhi mke ananiaga kuwa kuna shughuli sijui inaitwa kitchen mada kama nimekosea mta sahihisha ya mdogo wake baba john nikamkubalia lakini kwa shingo upande anasema kulingana na ratiba za shughuli atarudi kesho

Jamani mpaka kufikia hapa mimi naona mume mwenzangu ananizunguka mbuyu na sitaki afike hapa kwangu naweza kuua na nikapelekwa jela

Wadau naomba mchango wenu niache mke lakini bado nampenda au amchukue mtoto wake lakini john mwenyewe bado mdogo ili anipe amani ,nitaua mimi

assanteni nasubiri ushauri wenu
Pole sana ndugu, Nina rafiki yangu mmoja alikuwa na tatizo kama lako ila yeye babs mtoto wa mkewe amejitokeza after 15 yrs, kilichokuwa kinatokea kinakaribiana na cha kwako na nilimshauri yafuatayo:
1. Piga stop huyo mwanaume kuja kwako
2. Akitaka kumuona mtoto mchagulie siku aje amchukue akashinde nae
3. Ni vizuri pia ungejua chanzo cha kuachana kwao itakusaidia katika maamuzi yako.
4. Ongea na mkeo na umwambie ukweli kuwa hupendezwi na kinachoendelea na muulize je ingekuwa teye kwa mke mwezake anafanya hivyo angejiskiaje
Maamuzi ya mwisho ni yakwako mwenyewe sababu hayo ni maisha yako
Tafakari kwa kina na usiogope kuwa jasiri wa maamuzi
 
..Leo hii asubuhi mke ananiaga kuwa kuna shughuli sijui inaitwa kitchen mada ya mdogo wake baba john nikamkubalia lakini kwa shingo upande anasema kulingana na ratiba za shughuli atarudi kesho

Hata kama kusoma hujui, picha pia huielewi? Kubwa Jinga indeed..
 
Mpige marufuku kuja kwako Angalizo:
kiumbe anaye weza kuja utamlea ukadhan ni wa kwako kumbe ulisha zungukwa mbuyu na baba John
 
Ni shida siku jua Kama dunia hii kuna wanaume wa namna hii. Maana Mimi napataka wenye wivu hata simu unakuwa monitored
 
Sikuwa kudhan kama kwenye dunia ya sasa kuna wanaume bw*** kam ww? Duuuh huna mke hapo! Kunusuru ndoa yako mtoto aende kwa baba yake full stop. Kila mtu abebe zigo lake
 
pole sana kubwa jinga...since siku ya kwanza uliyataka mwenyewe , pambana uwezavyo unusuru ndoa yako
 
"Mwanaume kiumbe adimu kilichokaribu kutoweka duniani"
Nadhani wewe mtoa mada ni mvulana uliyeoa mapema, ungekuwa mwanaume tayari ungekuwa umeshapata majibu tayari
 
hakuna kitchen mada ya kulala hukohuko...muongo huyooo..
 
Habari wadau
Naanza kuandika kisa hiki kwa maskitiko makubwa
Mwenzenu nina mke nimebahatika kuzaa nae mtoto mmoja lakini mke huyu wakati huo naanza nae mahusiano yetu nilimkuta na mtoto mmoja wa umri wa miaka 5

Kama mjuavyo nilivutiwa na bibie na sikuona uzito wa kumlea mtoto nilifurahi kujua huyu mke ni mlezi na waswahili wanasema ukipenda boga penda na ua lake

Mwezi uliokwisha aliibuka bwana mmoja asubuhi kabla ya mimi sijakwenda kwenye shughuli zangu akakaribishwa mimi nikatoka ukumbini nikamkuta huyu bwana amekaa na watoto wote wawili kwenye kochi, nikamuuliza mama watoto akanijibu nilikuwa nasubiri nikufahamishe huyu ni (baba john) si jina rasmi,nikamsalimia tukaletewa chai tukajumuika pamoja kunywa chai na maandazi tukaongea kuhusu maisha kidogo na akanieleza dhumuni la kufika hapa ni kumuangalia mwanawe ,siku zimekuwa nyingi nikawaacha mimi nikaondoka kuelekea kwenye mizunguuko yangu

Swali linalonisumbua kichwa huyu bwana alipajuaje hapa nyumbani na kwanini alikuja asubuhi hana shughuli huyu mtu, na pia hivi sasa nasikia mimi nikitoka na yeye anafika mara mbili kwa siku kuangalia mtoto na akifika anaacha mizigo anaondoka sasa juzi ndio ilikuwa kali nilikuta chupa za bia nikaambiwa nililetewa na mume mwenzangu na yeye ameshakunywa zake nikamuuliza mke akanijibu nisiwe na wasiwasi yule anampitia mwanawe na yeye ni mtu mzima hawezi kutuchanganya,lakini jamani mtu na mtuwe ni kama gari na mteremko

Ok kwa sababu ya likizo ya viroba nikajinoma bia lakini kwa shingo upande na kengele ya tahadhari ikinililia kichwani
Leo hii asubuhi mke ananiaga kuwa kuna shughuli sijui inaitwa kitchen mada kama nimekosea mta sahihisha ya mdogo wake baba john nikamkubalia lakini kwa shingo upande anasema kulingana na ratiba za shughuli atarudi kesho

Jamani mpaka kufikia hapa mimi naona mume mwenzangu ananizunguka mbuyu na sitaki afike hapa kwangu naweza kuua na nikapelekwa jela

Wadau naomba mchango wenu niache mke lakini bado nampenda au amchukue mtoto wake lakini john mwenyewe bado mdogo ili anipe amani ,nitaua mimi

assanteni nasubiri ushauri wenu
Kumbe ulioa mke wa mtu.

We jamaa sijui niseme unaroho ngumu ya uboya sijui nsemeje.

Kwanza inaelekea huyo mkeo anakuona lofa sana ndo maana amemleta mme wake wa nyumbani kwako bila ya wewe kuwa na taarifa maana mkeo anafahamu uboya wako.

Mkeo amepigwa halichachi nyumbani kwako alafu akakupoza kwa balimi mbili na bado mkeo anampelekea zigo na kulala hukohuko.

Pole mwanaume suruali
 
Back
Top Bottom