Thread yako inasikitisha kwani umefananisha na kisa cha kweli kabisa ninacho kifahamu na jamaa ninayemfahamu ila yeye ni miaka sasa imepita.
Alikuwa hana kitu, akaoa na wakafanikiwa kupata watoto 4 wa kike. Bwana akaanza vitimvi, mpaka na dada yake na mahouse girl 2 na mtoto wa dadake mkewe. Wote akawa do. Dadake akachomoa ya miezi 5 kidogo iende naye.
Akamfukuza yule mke wa ndoa akavuta ndani wale mahousegirl wote 2 na kuutangaza ufalme. Ana watoto 19 leo.
Mali ilikaa kidogo lakini kaka wanasema, dua ya mnyonge husikika huko juu.
Yule mama wa house akaolewa mbali kwa mtu mwingine kumbe yeye ndo alikuwa ngekewa kwani kule amesitawi ile mbaya saa hivi. Lakini jamaa amecharara kuliko hadithi. Namjua na namwona akikat mbuga kiatu chake anatembelea ngozi ya upande mmoja. Huwezi amini kuwa ni mtu keshakuwa na maduka makubwa 29 na malori 4 ya isuzu boxbody ma pesa ya kumwaga.
Mama, tulia kwa Bwana Mungu. Atakulipia mateso yako ukiona hivi hivi. Kama una njia ya kujipatia angalao kamtaji hata wa kukaanga mandazi uza maandazi yako, na Mungu atakuinua pole pole na utafanikiwa tu. Mpende tu kwani ni mzazi mwenzio. Hao wengine woote ni wa kuja tu hivyo ni wadowezi tu wewe ndo mwenye nyumba. Baraka zake ziko kwako.