Mulugo: Division Five haipo na sifuri ipo palepale

Mulugo: Division Five haipo na sifuri ipo palepale

Mulugo siku hizi anashinda JF kasoma maoni yenu kajua hapa na soon wataitwa dakika 45 au kipima joto kaona hapana mapema .Kaanza kusoma alama za nyakati si mjinga kivile .
 
Nyie wana siasa wa wizara ya Elimu acheni bwana kuwachanganya watoto wetu hata kama watoto wenu hawasomi kwenye shule zetu za kata. Ongeeni kama wasomi kwani naona hata profesa mzima anataka kushindwa na mwenyekiti wangu wa mtaa darasa la saba la zamani katika kufanya maamuzi.
 
Mabata wadogo wadogo wanaogelea kaktika shamba zuri la elimu la Tanzania. Ni nchi pekee ambayo huwezi kutofautisha profesa na aliyeishia darasa la nne. Tunamsubiria Pinda na yeye aropoke lake. Tuendelee kusubiri tuone Alhamisi akitwangwa swali kuhusu hilo atajibu nn?

Hivi hii ndo "BIG RESULTS NOW nini Mkuu" watoto wanaanza mitihani chenga na danadana zimeshaanza .....Usijali tutaunda tume ya kuchunguza ..... na hapa usije ukashangaa baada ya matokeo kilaza mwingine akasema watoto walifeli kwasababu ya kuathirika kisaikolojia na Amri ya Mulugo ya kuondoa ofa ya Mchome kufutilia mbali division Zero ili watoto wakiwa shuleni waserebuke tu......Haya mambo unaweza ukayaona Tanzania tu...
 
MACCM yameamua kuchakachua mfumo wetu wa elimu!
 
Hivi hii ndo "BIG RESULTS NOW nini Mkuu" watoto wanaanza mitihani chenga na danadana zimeshaanza .....Usijali tutaunda tume ya kuchunguza ..... na hapa usije ukashangaa baada ya matokeo kilaza mwingine akasema watoto walifeli kwasababu ya kuathirika kisaikolojia na Amri ya Mulugo ya kuondoa ofa ya Mchome kufutilia mbali division Zero ili watoto wakiwa shuleni waserebuke tu......Haya mambo unaweza ukayaona Tanzania tu...
Sitashangaa sana maana ndio mfumo tulioamua kuufuata. Big result now ilitaka kutuaminisha kuwa wanafunzi wote wamefauli maana hakuna zero.Profesa huyo aliamua kuita press na kutoa hayo aliyotoa bila kumuhusiha waziri. chaajabu hii wizara sijawahi msikia sana Dr. Kawambwa ila mara nyingi yuko Mulugo. Lets see. ila nashukuru katangaza asubuhi wanafunzi wakiwa washawahi shuleni.
 
Hujui kuwa ufaulu wa sasa ulitayarishwa zamannniiiiii. Hao wenye kusomea madawati ya mawe kama vigoda walie tu. Subiri uone matokeo ktk ligi hii ST.... , GT NA KATA.
 
Leo nimetumiwa sms inasema waingereza wanazindua iphone 5s huku watanzania nao wanaend na technologia kwa kuzindua division 5.!!
 
Mabata wadogo wadogo wanaogelea kaktika shamba zuri la elimu la Tanzania. Ni nchi pekee ambayo huwezi kutofautisha profesa na aliyeishia darasa la nne. Tunamsubiria Pinda na yeye aropoke lake. Tuendelee kusubiri tuone Alhamisi akitwangwa swali kuhusu hilo atajibu nn?

Ataigiza tu,hachelewi kulia yule. Yaani hii nchi full majuha.
 
Na haiwezekani ww unasumbuka miaka yote hii kupandishwa daraja ukiwa upo palepale daraja C,nipe jina lako nikirudi ofisini nitahakikisha daraja lako la mshahara linapanda mpaka A.
Ha haa haaa haaaa...! Mkuu umenikumbusha hii,nimecheka sana! Jamaa aliongea akiamini daraja A ni kubwa kuliko C. Aaah,mulugooooooo.....!!
 
Me nashukuru Mungu ameongea wakati wanafunzi wakiwa tayari wapo shule! Angeongea jana,ki-saikolojia ingewaathiri saana.

wangeongea tu baada ya mitihani, huku mtaani vijana wanajipa matumaini ile ngumu wanajua lazima mwisho wa siku cheti kipo hata kama amepata 19 kila somo
 
Mawaziri wa JK ni wa matamko tu sio ufanisi. Maskin nchi yangu.
 
nothingtosay.jpg
 
Huyo mulugo yeye kila anapoongea lazma atoe ushuzi!,hivi huwaga hajiandai?,au hana mawasiliano na wenzie?
 
anataka ajisafishe kivyake baada ya kusemwa sn wakati ss ndo anatujengea mazingira ya kumdadisi zaidi
 
naangalia tbc 1 hapa,naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi philipo mulugo,amekanusha maneno ya mchome ya kuongeza daraja la 5 na kusema daraja hilo halipo na sifuri ipo pale pale.

Source; tbc 1
kauli ya kilaza. Sishangai hata kidogo.
 
Ingawa kwa hilo nakubaliana naye, kama binadamu anaitwa Mulugo ametoa maoni yake sina la kusema. Hivi pamoja na kufoji kote huko Mulugo ado Naibu Waziri? JK, huyu mtu ana kazi nyingine ipi kitaifa au ni mganga? Mnataka afanye lipi ndipo umuondoe?

Tanzania ni muungano wa Tanganyika na visiwa vya Zimbabwe..... Ya mulugo tumwachie Mulugo na JK.
 
Back
Top Bottom