Muhongo atoroka!

Muhongo atoroka!

Anaogopa kuwekwa lupango keko maana jamaa hawaeleweki

OvA
 
kufanya nn sasa hata ubunge nahisi ataukacha kama yuleeee aliye sema anaachana na siasa uchwara
 
Yeye shida yake ni uwaziri, na ndio kitu kilichomfanya aache kazi huko South Africa (kama sijakosea) na kuja nchini ili apewe Wizara. Ubunge sio ishu kwake, ndio maana akiondolewa kwenye uwaziri, anaondoka bungeni. Na kama unavyomjua Muhongo alivyo na "jeuri ya elimu".
 
  • Hii habari ni kweli au ni kutaka tu kuuza gazeti?
  • Sitashangaa gazeti hili likijikuta linatakiwa kumuomba radhi Muhongo
Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, hajaonekana bungeni jijini Dodoma bila ruhusa ya Spika tangu uteuzi wake katika baraza la mawaziri utenguliwe wiki tano zilizopita.

Mei 24, mwaka huu, Rais John Magufuli alitengua uteuzi wa Prof. Muhongo katika baraza la mawaziri, ikiwa muda mfupi baada ya kukabidhiwa ripoti ya kamati ya kwanza ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu (Makinikia).

Hata hivyo, uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa mtaalamu huyo wa Jiolojia wa kimataifa hakuwapo bungeni wakati uteuzi wake wa uwaziri ukitenguliwa, huku taarifa zikidai alirudi nyumbani kwao, Musoma mkoani Mara, kuhudhuria mazishi ya dada yake.

Simu ya Prof. Muhongo iliita bila kupokewa alipotafutwa na Nipashe kwa siku tofauti, ikiwamo jana, kuzungumza sababu za utoro bungeni.

Kutokana na kutoonekana bungeni kwa Prof. Muhongo, Nipashe jana ilizungumza na Katibu wa Bunge kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Dk. Thomas Kashililah, ambaye alisema ofisi yake haina taarifa za Mbunge huyo wa Musoma Vijijini (CCM) jambo ambalo ni kinyume cha utaratibu.

Kiongozi huyo wa Bunge pia alisema ofisi yake haijui aliko tangu alipoachishwa nafasi ya uwaziri mwishoni mwa mwezi uliopita.

Dk. Kashililah aliongeza kuwa kwa kawaida mbunge anapokuwa na udhuru, humwandikia Spika kumwelezea hatakuwa bungeni kwa muda fulani na ofisi ya Katibu wa Bunge hupewa nakala.

"Sijapata nakala yoyote ya udhuru wa Profesa Muhongo na wala sijui alipo tangu siku ile", alisema Dk. Kashililah.


Katibu wa Bunge huyo alisema hii ni mara ya pili kwa Muhongo kuondoka bungeni kwa muda mrefu bila ya ruhusa kwani hata alipomwandikia barua ya kujiuzulu Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete, hakuhudhuria Bunge kwa muda mrefu.

Prof. Muhongo alijiuzulu nafasi ya Waziri wa Nishati na Madini Januari 24, 2015 kwa shinikizo la Bunge, kutokana na taarifa ya Kamati moja ya chombo hicho juu ya kashfa ya uchotwaji fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.


Chanzo: Nipashe
  • New-Doc-2017-06-22_17-686x950.jpg
hawawezi chukuliwa hatua [*]nipashe ni chombo kikubwa cha habari [*]wamejiridhisha kutafuta ukweli ndiyomaana wamechapisha habari hii [*]katibu wa bunge amekiri kutoonekana kwa muhongo bungeni tena bila taarifa.
 
  • Hii habari ni kweli au ni kutaka tu kuuza gazeti?
  • Sitashangaa gazeti hili likijikuta linatakiwa kumuomba radhi Muhongo
Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, hajaonekana bungeni jijini Dodoma bila ruhusa ya Spika tangu uteuzi wake katika baraza la mawaziri utenguliwe wiki tano zilizopita.

Mei 24, mwaka huu, Rais John Magufuli alitengua uteuzi wa Prof. Muhongo katika baraza la mawaziri, ikiwa muda mfupi baada ya kukabidhiwa ripoti ya kamati ya kwanza ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu (Makinikia).

Hata hivyo, uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa mtaalamu huyo wa Jiolojia wa kimataifa hakuwapo bungeni wakati uteuzi wake wa uwaziri ukitenguliwa, huku taarifa zikidai alirudi nyumbani kwao, Musoma mkoani Mara, kuhudhuria mazishi ya dada yake.

Simu ya Prof. Muhongo iliita bila kupokewa alipotafutwa na Nipashe kwa siku tofauti, ikiwamo jana, kuzungumza sababu za utoro bungeni.

Kutokana na kutoonekana bungeni kwa Prof. Muhongo, Nipashe jana ilizungumza na Katibu wa Bunge kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Dk. Thomas Kashililah, ambaye alisema ofisi yake haina taarifa za Mbunge huyo wa Musoma Vijijini (CCM) jambo ambalo ni kinyume cha utaratibu.

Kiongozi huyo wa Bunge pia alisema ofisi yake haijui aliko tangu alipoachishwa nafasi ya uwaziri mwishoni mwa mwezi uliopita.

Dk. Kashililah aliongeza kuwa kwa kawaida mbunge anapokuwa na udhuru, humwandikia Spika kumwelezea hatakuwa bungeni kwa muda fulani na ofisi ya Katibu wa Bunge hupewa nakala.

"Sijapata nakala yoyote ya udhuru wa Profesa Muhongo na wala sijui alipo tangu siku ile", alisema Dk. Kashililah.


Katibu wa Bunge huyo alisema hii ni mara ya pili kwa Muhongo kuondoka bungeni kwa muda mrefu bila ya ruhusa kwani hata alipomwandikia barua ya kujiuzulu Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete, hakuhudhuria Bunge kwa muda mrefu.

Prof. Muhongo alijiuzulu nafasi ya Waziri wa Nishati na Madini Januari 24, 2015 kwa shinikizo la Bunge, kutokana na taarifa ya Kamati moja ya chombo hicho juu ya kashfa ya uchotwaji fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.


Chanzo: Nipashe
  • New-Doc-2017-06-22_17-686x950.jpg
Hiki ni kiburi na dharau kwa Bunge.Lakinii,kwani Bunge halina sheria za kuweza kumwajibisha.Itakuwa ajabu sana kama halina.Huku ni kukosea wananchi wa Jimbo lake haki yao ya msingi ya kuwakilishwa.Awajibishwe.
 
Muhongo anajuta kurudi nchini angejua.......lakini ninge ange.....ni majuto mjukuuu!!!
Angepata wapi shamba lingine LA bibi? Hawezi kujuta hata kidogo! Sema kwa sasa inaelekea limepata mwenyewe! Ila watangulizi walijivunia sana na sasa wameachwa "wapumzike"!
 
Katika nduki maana asije akarukishwa kichurachura hapo kisutu......

OvA
 
Huyu jamaa husema nchi itatikisika akiachishwa uwaziri
 
Muhongo anajuta kurudi nchini angejua.......lakini ninge ange.....ni majuto mjukuuu!!!


Kwani Muhongo alikuwa nani huko nje ya nchi?

Muhongo hawezi kujuta kurudi nchini, hapa nyumbani alipata the best job he could ever dream of getting anywhere else in the world. Waziri na mbunge. Sio rahisi kwa mhamiaji kupata kazi nje huko yenye hadhi, malipo, na ma perks kama ya Mbunge Waziri wa Afrika. Na ukiipata itakuwa ina ma perfomance stress mpaka utatolewa!

Kama hampajui ughaibuni na jinsi wazungu wanavyomchulia mtu mweusi waulizeni diaspora wawaambie ni mtaalam gani Mtanzania huko nje ana kazi maalum ambayo wazungu wanamsujudia kwayo?

Eti ajutae kurudi.
 
Back
Top Bottom