Muhimbili kuanza kutibu Wanaume wenye matiti

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
1698050033487.png

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) - Mlongazila, imesema huduma ya kupunguza uzito na upasuaji rekebishi zinazotarajiwa kufanyika hospitalini huko, zitahusisha pia wanaume wenye maumbile kama matiti.

Mkuu wa Idara ya Upasuaji MNH-Mloganzila, Dk. Eric Muhumba, alibainisha hayo na kueleza kuwa huduma hizo kama alivyoeleza awali, zitatolewa kwa siku mbili kuanzia Oktoba 27 mwaka huu.

"Huduma hii ya kupunguza uzito ni kwa jinsi zote mbili kwa kuwa kumekuwa na minong’ono kwamba, mbona mmependelea wanawake. Huduma itafanyika kwa watu wote wenye uzito mkubwa," alisema.

"Tumeona wanaume kwa bahati mbaya inatokea miili yao wanakuwa kama wana matiti badala ya kifua cha kiume, nao watafanyiwa upasuaji rekebishi katika siku hizi mbili," alisema.

Bingwa huyo aliwatoa hofu Watanzania kwa kuwaeleza kuwa, upasuaji huo ni salama na ni sawa na upasuaji mwingine unaofanywa hospitalini huko.
 
Plastic surgery zinakuja kwa kasi,

Ila kwa wanaume wenye matiti waende tu aisee, haiwi poa kuwa nayo
 
kuna jamaa mmoja aliendaga jeshini mafunzo ya ajira kabisa akakaa miezi miwili akarudishwa,alivyorudi akanambia eti ameambiwa yupo unfit sababu ana hayo matiti...
nikaona nisimuhoji sana maswali
Miez miwili ndan ya kozi , manyonyo hayajaisha....

Labd huyo ni complete homon imbalance
 
Manyonyo ya hivyo ukipiga push-up kila sku asubuh na jioni yanapotea ndani ya miezi mitatu tu.
Uko sahihi, mimi naona hapa inawahusu wale ambao wana unene wa kurithi, lakini unakuta mtu ana unene wa kula mi chipsi, pombe na nyama, kajiachia kawa mnene kizembe, sidhani kama ni wote wa kufanyia operesheni, wengine kama wakitoa uvivu wao, mazoezi yanaweza kurudisha miili yao ikawa vizuri...
 
Back
Top Bottom