Dr Matola PhD
Platinum Member
- Oct 18, 2010
- 61,564
- 109,103
Labda nikupe somo dogo ambalo huenda unalijuwa au kwa bahati mbaya hujui.Bado vijana wengi wa Kitanzania hawajui maana ya mapinduzi......
Sijawahi kuona mapinduzi ambayo anayepinduliwa anaombwa aache madaraka........
Mpaka muda jumuia ya kimataifa imeshindwa kuelewa nini kimefanyika Zimbabwe
Tanzania tukiwa ndani ya mfumo wa chama kimoja tulikuwa na mkoa wa majeshi na wanajeshi wote walikuwa ni wanachama wa ccm.
Halikadharika mpaka leo jeshi la Zimbabwe ni wanachama wa ZANU-PF na ukumbuke Mugabe ni Comrade mwenzao pamoja na mapungufu yake wanamtunzia heshima ndogo aliyobaki nayo.
Ni lazima uelewe jeshi la Zimbabwe halikuingilia mgogoro wa Zimbabwe kama nchi, bali jeshi limeingilia mgogoro wa chama chao na yule makamu wa Rais aliyefukuzwa na Mugabe ni Comrade mwenzao ni veteran wa kupigania uhuru jina lake maarufu walimwita Mamba.
Unapoangalia kinachoendelea Zimbabwe usifananishe na nchi nyingine, wale wanajeshi hawakuwajali wananchi wa Zimbabwe kwa sababu Mugabe ni kitambo tu anazinguwa tu, ila kilichofanywa na jeshi ni kukilinda chama chao cha Mapinduzi cha ZANU-PF.
Nadhani utakuwa umepata mwangaza sasa ni kwa nini Tanzania wanajeshi walipewa option anayetaka jeshi abaki jeshini na anayetaka ccm abaki ccm.
Ndio kina Makamba, Komba, Kinana, Kikwete, Nnauye,Chilligati,Mkuchika na wengineo wakaamuwa kubaki ccm na kuacha jeshi.
Leo Magufuli anarudia makosa hayahaya kuwajaza wanajeshi serikalini kuna kitu bado hakielewi vizuri.