Mugabe Agomea Mazungumzo Ya Kuachia Madaraka

Mugabe Agomea Mazungumzo Ya Kuachia Madaraka

Yuko kizuizini na mtu aliyemfukuza katika nafasi ya umakamu wa Rais ndo amepewa nafasi kuongoza serikali kwa muda yeye bado anagoma?
Hana jeshi sasa anaongoza nini?. Unadhani bila jeshi kuna nchi. Akikaa kizuizini tu miezi mitatu kwisha habari yake maana hakuna kilichosimama nchini.
 
Wadau
Updates from Zimbabwe,
Mugabe agomea mazungumzo ya kuachia Madaraka
Asema atabaki kuwa Rais Halali wa Zimbabwe
Kiongozi Mkuu wa Upinzani Morgan Amuomba Mugabe ajiuzulu
Mwenyekiti wa Umoja wa Africa alaani Mapinduzi ya Kijeshi Zimbabwe
Karibuni
 
Haya w ngoma bado mbichiiii, ila bora apishe tuuu mana hakuna namnaaaaa
 
Haya sasa wale wote walionibishia baada ya kuwaambia Mugabe hawezi pinduliwa waje hapa
Duh! Baadhi ya Watanzania wenzetu hii karne haiwafai kabisa, mlitakiwa muishi karne nyingi zilizopita na hivyo hivi leo watu kama Magufuli tungewasoma tu vitabuni. Tatizo ni kwamba Tanzania imebakia kama hifadhi ya watu kama wewe na kwa namna hiyo watu kama Magufuli bado wanaweza kusukumiziwa Urais hata kama uwezo, akili, busara wala hekima hawana...! Mugabe bado yuko hai kwa vile tu hakuna umuhimu wa kumshughulikia kwa namna yoyote ile...ni kumpa muda tu wa kujitafakari katika uzee wake akisubiri kipyenga.
 
Ukiachana na mihemko unagundua kuwa sio jambo rahisi kwa jeshi kuchukua nchi
 
Bado vijana wengi wa Kitanzania hawajui maana ya mapinduzi......

Sijawahi kuona mapinduzi ambayo anayepinduliwa anaombwa aache madaraka........

Mpaka muda jumuia ya kimataifa imeshindwa kuelewa nini kimefanyika Zimbabwe
 
Duh! Baadhi ya Watanzania wenzetu hii karne haiwafai kabisa, mlitakiwa muishi karne nyingi zilizopita na hivyo hivi leo watu kama Magufuli tungewasoma tu vitabuni. Tatizo ni kwamba Tanzania imebakia kama hifadhi ya watu kama wewe na kwa namna hiyo watu kama Magufuli bado wanaweza kusukumiziwa Urais hata kama uwezo, akili, busara wala hekima hawana...! Mugabe bado yuko hai kwa vile tu hakuna umuhimu wa kumshughulikia kwa namna yoyote ile...ni kumpa muda tu wa kujitafakari katika uzee wake akisubiri kipyenga.
Duh! Hii comment imebidi tu nicheke, kuna watu mnajiona bora kuliko wengine, haya lipumba cha maana ulichofanya kunzidi? Changia hoja sio kuattack personality
 
Duh! Ujui unenalo... Mugabe hana uwezo huo wala nguvu za kukataa tena. Akiwa na hekima ndogo atakabidhi Madaraka kwa makamu wake aliyemfukuza na yeye ama kwenda uhamishoni au kuomba akae kwa amani nchini (ambayo sidhani kama itawezekana kutokana na maadui aliojitengenezea ndani ya nchi). Tanzania ni option mzuri ya yeye kuja Kukaa.
Asije atatusababishia balaa aliyataka mwenyewe
 
Kaka serikali ni Ile Ile ya ZANU -PF, Na makamu wa rais anakuwa rais, mapinduzi Gani unamuomba mtu a resign mwenyewe? Ingekuwa ni mapinduzi kusingekua na upatanishi mkuu
Nani kakwambia itakuwa ni serikali ya Zanu-PF pekee !!!! Unaelewa maana ya serikali ya mseto ??? Serikali itakayojumuisha na opposition party ndio inaenda kuundwa Zimbabwe,

Muwe mnasoma mtandaoni
 
Nani kakwambia itakuwa ni serikali ya Zanu-PF pekee !!!! Unaelewa maana ya serikali ya mseto ??? Serikali itakayojumuisha na opposition party ndio inaenda kuundwa Zimbabwe,

Muwe mnasoma mtandaoni
Serikali ya mseto? Kama Ile ya Shein na Seif?
 
Kaka serikali ni Ile Ile ya ZANU -PF, Na makamu wa rais anakuwa rais, mapinduzi Gani unamuomba mtu a resign mwenyewe? Ingekuwa ni mapinduzi kusingekua na upatanishi mkuu
IMG-20171116-WA0013.jpg


Kama utakuwa umekosa akili hata hapa ndio basi tena.

Hizi ni diplomatic language tu, Mugabe alishaondolewa madarakani na yupo kizuizini.
 
View attachment 631788

Kama utakuwa umekosa akili hata hapa ndio basi tena.

Hizi ni diplomatic language tu, Mugabe alishaondolewa madarakani na yupo kizuizini.
Kuna vijitu vinajifanya vijuaji sana, kulazimishwa kuresign sio mapinduzi, haya Tony Blair alilazimishwa kuachia ngazi
 
CHEZEA WALI NAZI WA IKULU DINGI LAZIMA AKOMALIE GOLI ALAFU NA UZEE ULE LAZIMA KUNA FYUZI ZISHABUTUKA
 
Back
Top Bottom