Ndio maana nakupenda mjukuu, sema tu hujui!Babu mjukuu wako nipo vizuri kicwani ukiachana na zile mada zangu zingine🤪
🤔🤔
Subiri kwanza nitarudi acha nifikilie hili swali fupi ila jibu lake linataka utulivu
Karibu babu England 1 wengine 0 😀😀
Ukimpa mtu muda wako, umempa sehemu ya maisha yako ambayo haitarudi tena ❤️Muda ni nini hasa?🤔
Kwa wengi wetu, muda ni kipimo kinachotuonyesha sasa ni saa ngapi, ni asubuhi, mchana au usiku
Tunautambua kwa kuangalia saa, simu au hata mwendo wa jua
Lakini je, muda ni saa tu?
Mara nyingi tunasikia maneno kama
Tumia muda wako vizuri
Usichezee muda wako
Muda ni mali
Muda ukipita haurudi tena
Muda utasema
Hapo ndipo ninapojiuliza, muda ni nini hasa?
Je, ni sekunde, dakika na saa zinazopita?
Au ni nafasi tunayopewa kuishi, kupenda, kujifunza na kutimiza ndoto zetu?
Umewahi kunyimwa muda na mtu uliyekuwa unamhitaji?
Mimi niliwahi kumpenda mtu
Na nilivyo nikipenda mtu hua ni huyo huyo siwezani na stress za wapenzi wengi so hua nategemea vingi kutoka kwake kwa sababu nakua sina sehemu nyingine ya kuvipata
Kila nilipomuonesha nime m miss ghafla nilipokea SmS
Imethibitishwa umepokea kiasi fulani kutoka kwa fulani
Kisha ananiambia S, kanunue wine unywe
Kitu ambacho si kibaya ila sikua naitaji pesa yake tu nilimtaka yeye pia
Sasa sielewi labda nilikua nazidisha sana kumuitaji mpaka akachoka au la🤔
Nilifurahi kwa sababu alikuwa ananijali kwa namna yake
Lakini ukweli ni kwamba sikuwa nahitaji pesa pekee
Nilikuwa mpweke.
Nilitamani anipe muda wake
Kila nikisema Babe, I miss you
Badala ya mazungumzo marefu au muda wa kuwa pamoja, nilipokea tena pesa
Sio kwamba sikuthamini pesa (hapana)
Lakini wakati mwingine mtu hahitaji zawadi, anahitaji uwepo wako Anahitaji muda wako
Anahitaji kusikilizwa
Ndipo nikagundua kuwa kuna vitu ambavyo pesa haviwezi kununua, na kimojawapo ni muda wa mtu
Na si katika mapenzi tu
Kuna watu hunyimwa muda wa kujieleza
Kuna watu hunyimwa muda wa kuonyesha vipaji vyao
Kuna watu hunyimwa muda wa kusikilizwa
Kuna watu hunyimwa hata muda wa kuponya majeraha yao
Kuna watu hupoteza fursa mbali mbali kwa sababu walinyimwa mda
Basi, muda ni nini?
Unaelewa nini ukisikia neno mda?
Kwangu, muda ni maisha yenyewe
Kwa sababu kila kitu kinahitaji muda
kupenda, kusamehe, kukua, kupona, kufanikiwa na hata kuondoka
Na ndiyo maana tunasema
Muda ni mali, lakini zaidi ya mali, muda ni maisha
Ukimpa mtu muda wako, umempa sehemu ya maisha yako ambayo haitarudi tena ❤️⏳
ShesRise_1 🖐
Sasa mimi kipingi hicho ndio naanza chekecheaKwanini mahi ndio ingekufaa ?
Kipindi hicho mwaka 2009
Nilikua hata sijavunja ungo
Wakati unatuma hii nilikua nimelala😅Lala uko 😒
Shukrani kaka nina mengi natamani tuongee please ukipata mda tufanye ka mdahalo nijiokotee maarifakati ya vitu nimetumia muda mwingi kuvisoma ni muda wenyewe, hapa nimeanzia zama za mawe hadi digital age, mifumo yote ya kalenda nimepitia mpaka zile siku 11 zilizopotea zilizoleta kizaazaaa, mifumo yote ya saa na technologies zote za saa mpaka cesium-133 atom na atomic clock,
International Meridian Conference in Washington na zero longitude kupita Greenwich bila time haya yote yasinge kuwepo, kitendo cha ku link time na positioning systems hapa ndo nikaanza kuamini time and space are two side of the coin na huwezi kivitofautisha, hapa ndo hayo mambo ya kupoteza muda, hakunipa muda, yote ni kuchanganya space na time ambayo ni kitu kimoja space-time
sikuishia hapo, nikaenda traditional astronomy mpaka precisely observation maana bila muda kosingetokea kitu, Kepler's planetary motions mpaka principia mathematica, nikaachana na classical physics mpaka quantum physics, relativity and time travel, hakuna kitu kimenipotezea muda kama theoretical physics hapa nili base kwenye haya mambo ya muda.
Hili suala la muda ni mada ndefu sana na ni very interesting, sekunde moja ni kubwa sana ukitaka kujua ukubwa wa sekunde fanya software development halafu function zako ziwe zina excute for 2 seconds wakati inatakiwa less than 20ms
Watu wengi hawajui hata kwanini siku ina masaa 24 wakati tunaweza tukaamua tu siku nzima iwe ni saa moja? hawajui kwanini masaa 24 ndo optimum choice. wazee kwenye muda hapa kuna madesa mengi kuliko vitu vyote ulivyosoma shule.
Mimi nikiwa na muda basi nadili na huohuo muda maana kunamambo mengi bado nataka kuyajua kuhusu muda
Hii song itakua ina sisimua🥰Ukimpa mtu muda wako, umempa sehemu ya maisha yako ambayo haitarudi tena ❤️View attachment 3610166
HayaaSasa mimi kipingi hicho ndio naanza chekechea
Nakupenda pia babuNdio maana nakupenda mjukuu, sema tu hujui!
SawaTafisiri ya muda ni nafasi tuliyopewa na Mungu ili tuwe karibu naye zaidi kabla ya utimilifu wa nyakati
Shukrani🥰Umedadavua vyema .
Asantee swetie🥰Upo vizuri sana,
Hakika!Basi, muda ni nini?
Unaelewa nini ukisikia neno mda?
Kwangu, muda ni maisha yenyewe
Kwa sababu kila kitu kinahitaji muda
kupenda, kusamehe, kukua, kupona, kufanikiwa na hata kuondoka
Na ndiyo maana tunasema
Muda ni mali, lakini zaidi ya mali, muda ni maisha
Ukimpa mtu muda wako, umempa sehemu ya maisha yako ambayo haitarudi tena ❤️⏳
Yes🤝Hakika!
Bado sijaona!!Nakupenda pia babu
Hii song itakua ina sisimua🥰
Nifanye nini ili uone 😅Bado sijaona!!
Hiyo ni assignment yako.Nifanye nini ili uone 😅