Muasisi awashukia 'wabaya' wa CHADEMA

Muasisi awashukia 'wabaya' wa CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Zitto ni msaliti, lakini chama itusaidie kuwaaminisha watanzania beyond the reasonable doubt kuwa Zitto ni msaliti na mnafiki. Huyu jamaa kama chama itamsamehe apewe onyo kali halafu asipewe nafasi ya uongozi kwenye chama.

Zitto anashindana na Kikwete kusafiri nje! Halafu eti anataka urais! Hatutaki Vasco Da Gama nchi hii

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
I'm ashamed to identify myself as a teacher in a line with you.. If that's what it takes nowadays I better quit...

There is teacher and THE TEACHER!
so who exactly r u?!

Cause all I know teachers only available in the churches! Telling lies for living!!
 
Mkuu unakosea. Mwasisi wa siasa za kilaghai ni al marhum nyerere sote tunajua hilo japo tunajifanya wabishi hatutaki kukubali. Ifike mahali tukubali kumpa marehemu sifa yake japo ni mbaya

Nyerere ni baba wa Taifa...
 
Labda mleta mada ujiulize swali; how possible is it for Mzee Mtei to elect/appoint leaders?
Kama ni kura yeye anazo ngapi? Kwa nini shutuma hizi ziletwe sasa na watu wale wale wenye uchu wa madaraka has kwa nafasi ya m/kiti Taifa?

CHADEMA sio mali ya mtu binafsi, ni taasisi na chama huru cha siasa. Mwenye sifa za uongozi afuate taratibu na sheria za chama.

Naive...
 
Angegusia mapato na matumizi akiongeza na ukomo wa madaraka cc wanachama tungemuunga mkono.

Umeshamaliza sina LA kuzingumza,CDM ambayo tunaitaka ni ya muono wa kitaifa na siyo ya mzee mtei
 
Zitto ni msaliti, lakini chama itusaidie kuwaaminisha watanzania beyond the reasonable doubt kuwa Zitto ni msaliti na mnafiki. Huyu jamaa kama chama itamsamehe apewe onyo kali halafu asipewe nafasi ya uongozi kwenye chama.

Zitto anashindana na Kikwete kusafiri nje! Halafu eti anataka urais! Hatutaki Vasco Da Gama nchi hii

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Hizi ni propaganda za vijana wanaoshinda ufipa wa boss(invisible spies)
 
Mzee mtei ninakushukuru ulianzisha CHADEMA tena kwa pesa yako ya mfukoni.
Hata hivyo ni lazima ujue kwamba Chama ulichokianzisha kwa fedha yako hakijawahi kuwa mali yako, si mali yako, na wala hakitakuja kuwa mali yako kwa sababu kinamilikiwa na Watanzania walioamua kuwa wanachama wa CHADEMA kama mimi MADELA.
Wanaotaka kuanzisha taasisi ambazo watazimiliki life time ya generation zao hawaanzishi vyama vya siasa huunda makampuni kama ya IPP, Mohamed Enterprise, Azam Mwanamboka Msae Kichwere, Fresh ya Shamba nk.

Kifupi ni kwamba mabadiliko ya kweli yenye kuleta maendeleo ndani na nje ya CHADEMA ndo kwanza yameanza.
Hii vua vua iiyoambatana na waraka imetusaidia sana na kutupa uwezo wa kujadili UFISADI ndani ya CHADEMA.

MH MBOWE na DR SLAA wana hoja nyingi za kuweka sawa.
Hafukuzwi mtu hapa, wala kukimbia chama na wala mtu awaye yote asijidanganye kwamba nafasi yake kwenye CHADEMA ndo KINGA.
Wote ni lazima tuendelee kubanana mumu humu, na ni lazima kieleweke tu. Hatuogopi wanao achia shuzi la kifo wala wale wa kucheua harufu ya yai bovu.
Kubanana kubanana tu mbavu umia mtu choka.

Heshima yako Mzee Edwin Mtei.
 
Kwa hili tu mwache akili yake iwe inaganzi ,wache akiue Chama kwa kupandikiza ma DJs ma Ma MCs
 
Hivi CDM ni mali binafsi ya mzee huyu?
Mwasisi wa Chadema Mzee Edwin Mtei ameunga mkono na kupongeza maamuzi ya Kamati Kuu Chadema kuwavua nafasi za uongozi Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo.

Akizungumza nyumbani kwake Arusha Mtei amesema kamwe Chadema haitavumilia wasaliti wanaokula njama kurudisha nyuma harakati zake.

Mwasisi huyo mwenye mvuto na heshima kubwa ndani ya Chadema amesema kamwe hawezi kupingana na maamuzi ya Kamati Kuu na kutoa wito chama kuendelea kuwafuatilia na kuwatimua mara moja wasaliti kila wanapobainika.

Source:Mwananchi.
 
I'm ashamed to identify myself as a teacher in a line with you.. If that's what it takes nowadays I better quit...

Kuna mambo ni hatari kwa uhai wa nchi ila kama hoja zinakataliwa na ubabe unatumika kuwadhibiti watu wa dini flani tufanyeje.
 
Usaliti na kuandaa waraka hata kama ingekuwa nchi wangekamatwa na kutiwa kolokoloni, hatuwasamehe, wamechunguzwa kwa miaka zaidi ya mitano.
 
Angegusia mapato na matumizi akiongeza na ukomo wa madaraka cc wanachama tungemuunga mkono.
Mkuu mbona unaota ndoto za mchana. Jamaa wanakazania usaliti kwa chama, mi sioni kwa nini wasing'ang'anie kuhusu usaliti wakati wanaona NGO imeguswa na wasipokuwa makini mfereji wa ulaji unawezakwisha, maana umeshashtukiwa
 
Msaliti hatutakaa naye MZEE hongera kwa kuunga mkono, aende kwa wanaomtuma kazi hiyo
 
Asante Mzee taifa la Tz limeshaangamia kabisa
Ufisadi unatisha kila kona
Huyu mkoloni mweusi ametunyonya hadi mwisho
wananchi wa nchi hii hawafaidi matunda tuliojaliwa na mwenyezi Mungu katika nchi hii
Mabilion ya pesa zimefichwa Swiss, tembo wanawawa, madawa ya kulevya, nchi imewekwa rehani huko China
Wachina wanafanya hata biashara za umachinga wananchi wamebaki wazururaji
Watz tuamke tujitambue la sivyo tumekwisha
Maisha yamepanda balaa huduma mbovu, wao wanaenda kutibiwa nje sisi tunakufaAmk
eni watz njooni tuungane tupate uhuru wetu

Na hivi karibuni watapandisha tena bei ya umeme. Sijui wanataka tukaishi wapi? Hapa tukiendelea na tabia hii ya kuongea tu bila kuchukua hatua tumekwisha
 
Mzee Mtei anajua anachosema. Kujenga chama imara ni pamoja na kuwakomalia wanaokisaliti hata kama watu hao ni maarufu kiasi gani. Kilichoua ccm ni kuoneana haya inapofika kwa vigogo wenye majina. Mtu anayekaa kwenye chama kama kirusi ni hatari. Ni lazima "antivirus" ya chama ifanye kazi yake vilivyo kama cdm kinataka kudumu kuwa chama imara. Zito alionekana tangu mwanzo kuwa na nia ya kutaka madaraka hata kwa gharama ya umoja wa chama.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom