Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,880
Ndugu Zitto,
Mimi naomba sana kueleimishwa ktk hili..
Ni sababu zipi zinazotunga huu Muafaka wa vyama viwili jinsi ya kutawala nchi zima?..
je unatokana na uchaguzi wa mwaka 2000 au 2205 na kama ndivyo... Je matokeo ya uchaguzi huo yako wapi ambayo yanahallalisha kuundwa kwa Muafaka huu.
Tatizo langu kubwa sio kufikia Muiafaka wa kisiasa kati ya CCM na CUF isipokuwa vipengele vilivyosimamiwa..
Kwa nini iundwe serikali ya Mseto - what if - Jahazi Asili au United People Demokratic (UPDP) cha Fahmi Nassoro kikishinda uchaguzi mwaka 2010 kutakuwepo na utaratibu gani..
Sina wasiwasi na Chadema kwa sababu nyie tayarc mmekwisha jenga muafaka kati yenu na CUF hivyo siwezi kuingilia zaidi isipokuwa kwa chama kama CCM< nashindwa kuelewa sababu inayounda muafaka unaohusu Mustakabali wa nchi nzima kusimamiwa na vyama viwili tu.
Na mwisho, napenda kuuliza what's wrong kuuliza wananchi kwanza? kuna tatizo gani hapa ikiwa CCM wanataka swala hili liamuliwe na wananchi badala ya vyama viwili.. Kama alivyosema JK hili ndilo tatizo hadi sasa hivi kwa nini CUF hawatakli wananchi washirikishwe hali sauti hii ikipelekwa kwa wananchi itawageuka CUF zaidi kwa kutaka kuingia mkataba kisiri...
Je, Muafaka huu una kwa jinsi wanavyotaka CUF una tofauti gani (kwa wananchi) kati yake na ile mikataba ya madini?
Ndugu Mkandara,
Suala zima la mwafaka wa kisiasa ni lazima liwe na wachezai wakuu yaani key players. Hapa ni CCM na CUF. Ndio maana katika miafaka baada ya makubaliano yanayohusu wananchi watatawaliwa namna gani, inabidi kwenda katika kubadili sheria au kubadili/kuandika katiba ya nchi. Hapa suala linakuwa kubwa zaidi ya vyama. Linakuwa ni suala la wananchi wote kabisa. Key players wanakuwa ni chachu tu na ndio maana katika sheria hakitatajwa chama cha siasa bali yatatajwa mazingira ya kisiasa.
Kwenye suala la Zanzibar, CCM wanataka wananchi waulizwe mnataka mwafaka au sio! Kimantiki hili haliwezekani, kwani wakikujibu ndio maana yake ni kuwa ni lazima ukabadili katiba ya nchi na kutunga baadha ya vifungu upya. Wakisema NO ni mbaya zaidi kwani hutakaa uwe na mwafaka hata kama ukihitajika siku za usoni. Ndio maana taratibu ni wanasiasa kuongea, wanasheria kuandaa muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba ua kuandika katiba mpya kabisa na kisha wananchi wanaulizwa mnataka katiba hii au hamtaki. Wakikataa, katiba ya zamani inatumika, wakikubali katiba mpya inatumika na hivyo unakuwa ni mwafaka wa umma na sio wa vyama.
Mwafaka wa sasa ni kufuatia hali ya kisiasa ya zanzibar toka uchaguzi wa mwaka 1995,sio uchaguzi uliopita tu. CCM wanacheza siasa na CUF kuna makosa ya kimsingi kabisa wanafanya. Kwa mfano suala hili ni lao tu na sio vyama vingine, wanakosa mawazo mbadala na kujikuta hata mapendezo ya mwafaka kuonesha picha ya wao tu (narrow picture).
Matokeo yake nchi ipo katika hatari sana wakati huu, na itakuwa hatari zaidi kwani viongozi hawajitokezi kuprovide leadership. Malumbano ya kijinga kabisa (UVCCM) ambayo hayana chembe ya utamaduni wetu wa kisiasa