BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,825
- 287,847
Muafaka: JK sasa mambo mazito
2008-05-14 16:09:08
Na Usu-Emma Sindila, Buguruni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bwana Jakaya Kikwete sasa amewekwa kwenye mtihani mgumu kufuatia chama cha upinzani cha CUF, kuapa kwamba, kamwe hakitarudi kwenye meza ya mazungumzo.
Kinachofanya mambo yawe mazito kwa kiongozi huyo wa nchi, ni chama hicho kumbwagia sakata hilo zito JK na kukataa kata kata kuendelea kulijadili kama vyama.
Katibu Mwenza wa CUF, Bw. Ismail Jussa Ladhu, kurudi kwenye meza ya mazungumzo na CCM ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi.
Bw. Ladhu ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Makao Mkuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni, amesema kwa sasa mtu pekee anayeweza kuokoa jahazi
hilo ni rais Kikwete.
``Tukubali, tusikubali rais Kikwete ndiye mwenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, na hatuwezi kurudi katika meza ya mazungumzo tena, kwa kuwa ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi wetu,`` akasisitiza.
Amesema bado nafasi ipo na kwamba kama JK atakaoonyesha nia ya kutaka kuzungumza nao, watampa nafasi na ushirikiano unaotakiwa.
Licha ya chama hicho kumwachia jukumu hilo zito rais Kikwete, kimetaka suala hilo lisichezewe shere kwani ni zito na linahusu mustakabali wa taifa.
Amesema kwa hatua iliyofikiwa sasa, ni budi suala hilo likashughulikiwa kama yalivyoshughulikiwa masuala ya Kenya, Comoro na la sasa la Zimbabwe.
Bw. Ladhu amesema njia pekee za kuweza kufikia makubaliano katika mazungumzo hayo ya muafaka, ni kwa CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo ya vyama vyote viwili na endapo Halmashauri Kuu ya CCM imeyakubali kimsingi, basi wakubali kutia saini na utekelezaji uanze mara moja.
Amesema njia nyingine ni kwa Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka kuitisha mkutano wa pamoja kati yake na wadau wakuu wa masuala hayo ya Zanzibar, ambao ni Rais Amani Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad kujadili na kukubaliana juu ya mapendekezo yaliyotolewa na NEC.
Chama hicho kimewaomba wanachama wake wa Zanzibar
na Bara kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki.
SOURCE: Alasiri
2008-05-14 16:09:08
Na Usu-Emma Sindila, Buguruni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bwana Jakaya Kikwete sasa amewekwa kwenye mtihani mgumu kufuatia chama cha upinzani cha CUF, kuapa kwamba, kamwe hakitarudi kwenye meza ya mazungumzo.
Kinachofanya mambo yawe mazito kwa kiongozi huyo wa nchi, ni chama hicho kumbwagia sakata hilo zito JK na kukataa kata kata kuendelea kulijadili kama vyama.
Katibu Mwenza wa CUF, Bw. Ismail Jussa Ladhu, kurudi kwenye meza ya mazungumzo na CCM ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi.
Bw. Ladhu ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Makao Mkuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni, amesema kwa sasa mtu pekee anayeweza kuokoa jahazi
hilo ni rais Kikwete.
``Tukubali, tusikubali rais Kikwete ndiye mwenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, na hatuwezi kurudi katika meza ya mazungumzo tena, kwa kuwa ni kupoteza wakati na kuwahadaa wananchi wetu,`` akasisitiza.
Amesema bado nafasi ipo na kwamba kama JK atakaoonyesha nia ya kutaka kuzungumza nao, watampa nafasi na ushirikiano unaotakiwa.
Licha ya chama hicho kumwachia jukumu hilo zito rais Kikwete, kimetaka suala hilo lisichezewe shere kwani ni zito na linahusu mustakabali wa taifa.
Amesema kwa hatua iliyofikiwa sasa, ni budi suala hilo likashughulikiwa kama yalivyoshughulikiwa masuala ya Kenya, Comoro na la sasa la Zimbabwe.
Bw. Ladhu amesema njia pekee za kuweza kufikia makubaliano katika mazungumzo hayo ya muafaka, ni kwa CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo ya vyama vyote viwili na endapo Halmashauri Kuu ya CCM imeyakubali kimsingi, basi wakubali kutia saini na utekelezaji uanze mara moja.
Amesema njia nyingine ni kwa Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka kuitisha mkutano wa pamoja kati yake na wadau wakuu wa masuala hayo ya Zanzibar, ambao ni Rais Amani Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad kujadili na kukubaliana juu ya mapendekezo yaliyotolewa na NEC.
Chama hicho kimewaomba wanachama wake wa Zanzibar
na Bara kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki.
SOURCE: Alasiri