Mtwara kimenuka: Mabomu ya machozi yarindima!

Mtwara kimenuka: Mabomu ya machozi yarindima!

Hali mijini hapa ni tete! Mabomu yanarindima mjini hapa kuwatawanya wananchi wanaojiandaa na mkutano mkubwa unaotarajiwa kufanyika mjini hapa kuhusu suala zima la gesi.

Chanzo cha mabomu hayo kupingwa ni baada ya umeme kukatika/kukatwa eneo panapotarajiwa kufanyika mkutano huo uwanja wa mashujaa mjini hapa na baada ya kuona hivyo wananchi wakaamua kuandamana kuelekea Tanesco kujua chanzo cha tatizo hilo la umeme na hali hiyo kupelekea polisi kuanza kuvurumisha mabomu ya machozi.

Ifahamike kwamba kumekuwa na mvua kubwa mjini hapa toka usiku wa leo ambayo inaweza ikawa chanzo cha kukatika kwa umeme huo (huu ni mtazamo wangu) ingawa inaweza ikawa hujuma pia.

Eneo nilipo umeme upo hali hii ya sintofahamu imepelekea huduma muhimu za kijamii kama maduka na soko kufungwa.

Eee, yan hapa mpaka kieleweke ,wanaMtwara big up' run hiyo ki2 mpaka 2one kua rasilimali zetu zinatumika kwa manufaa na sio ujanja ujanja tu hapa.
 
Hapa hakuna ushabiki, tunasimama katika ukweli, Tabora ipo choka huku madini yanatoka wilayani Nzega . Wanao nufaika wengine. Mtwara waki ruhusu itoke kule watakua kama Geita mali kibao inatoka pale ila njaa tupu
hivi tutashabikia mambo haya hata lini?
 
Dingswayo, Unafuraaaaahi,kama vila unangojea picha za Van Dame na Rambo sio? Hizo ni picha za watanzania wakijeruhiwa na pengine nao kujeruhi au kuua na kuuana sio sinema! huo ushabiki wenu unaponza wananchi. Na usifikiri wanaokaa kusini wote ni wamakonde usisahau hilo watakapowaona watu wasio wa Kusini ni kikwazo watawashambulia nini kitafuatia?
Ralphryder, sifurahii hata kidogo watu wakiumia na kuteseka, ndio maana niko mstari wa mbele kuona kuwa Mtwara na sehemu za kusini wanapata maendeleo yanayostahili. Maana ya kutaka picha si kuziangalia tu, pale kuweza kuzisambaza ikiwezekana duniani kote kuonyesha jinsi harakati za wana Mtwara zinavyozuiwa kwa kutumia nguvu za dola.

Na kwa taarifa yako nimeshawahi kuishi na kufanya kazi mkoa wa Mtwara miaka ya 1978 mpaka 1980, nimezunguka sehemu nyingi za mikoa ya Mtwara na Lindi na kutembelea vijiji vingi. Ni kutokana na hilo ndio maana nawaelewa watu wa kusini wanachokitaka.
 
Wenzao wa Arusha walillala usiku kucha na mvua...Hiyo ni haki yao/Gesi ni ya kwao. Wanamtwara piganieni haki yenu..
 
katika kujikomboa inahitaji kujitolea na kuwa tayar kwa kila linalotokea hata kama ni kifo poa tu.wanamtwara mimi kwetu kuko shwari mno nahapa ninasubiri idadi ya watakaokufa kwa kupigwa na vitu vilivyo na ncha kali.nasubiri tarifa hyo ndani ya tbc.
 
Mkutano unaendelea everything iz perfect... Pipo kutoka kilakona wamejongea,hawajali mvua wala nini..those above who thinks "ni upepo tu" they should think again..its a movement, pepoles movement! Wameitwa wabunge wote wa mtwara wa vyama vyote,waje wapokee maoni ya wananchi na wawe wawakilishi kwa mujibu wa kazi yao...asiyefika si mbunge wa mtwara kuanzia leo hii!
 
Hapa hakuna ushabiki, tunasimama katika ukweli, Tabora ipo choka huku madini yanatoka wilayani Nzega . Wanao nufaika wengine. Mtwara waki ruhusu itoke kule watakua kama Geita mali kibao inatoka pale ila njaa tupu
mkuu kuna mtu kakuzuia kufanya uwekezaji wa madini?
 
Wana mtwara msikubali kruhusu gas itoke maana laana ya umaskini wa kutupwa itawaandama! Msikubali kulubuniwa kuwa mtanufaika baada ya bomba kupelekwa dar!

Hakika mkikubali kwa hili mtasahaulika kama mlikuwa chanzo cha gas! Dar itaendelea kupendeza na watu watakula pesa kama kawaida yao!
 
Mpaka Magamba yakituachia Nchi yetu...........!!!!!!!
tanzania ni yetu sote chai ililimwa iringa ikainufaisha mpaka mtwara kahawa illimwa kagera na klm ikainufaisha mpaka lindi na ruvuma lazima tujenge umoja wa kitaifa acha
 
Back
Top Bottom