"Yo! MTV Raps" Hiyo 1988 -1990 tunaangalia kwenye VHS tapes LL Cool J anashuka kwenye Limousine ana rap "I Need Love", mambo ya X CLan, DJ Premier na Guru wa Gangstarr, Leaders of The New School wakiwa na Busta Rhymes, Digital Underground Shock G ana mu introduce dogo mmoja anaitwa Tupac Shakur, Tupac hata hajulikani hapo.
Ukute shows za Fab Five Freddy, Ed Lover, Dr. Dre wamekupangia ngoma za Wanyamwezi kutoka New York mpaka LA, umkute DJ Kid Capri ana scratch, umkute KRS-One na Scot La Rock, umkute Chubb Rock ana flow nonstop, umkute Big Daddy Kane ana flow kama hana akili nzuri, uwakute NWA wana rep West Coast, utafurahi mwenyewe hapo.
Na sisi tukachukua inspirations na DJ Kim Mgomelo wa Kim and The Boyz tukaanzisha mashindano ya Yo! Rap Bonanza Dar es salaam miaka ya mwanzo ya 1990.
Na ITV ilipoanza Tanzania ikaanzisha shooting za video za muziki wa Hip Hop na watu kama Kwanza Unit, Hard Blasterz, Sossy B, Dar Young Mob, Deeplowmatz etc kwa kufuata mfano wa MTV.
MTV imetupa memories nzuri sana.