MTV: Mwisho wa enzi

MTV: Mwisho wa enzi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,869
Reaction score
828,401
Mtandao maarufu wa Muziki Duniani, MTV unajiandaa kufunga Chaneli zake za mwisho za kimataifa za video za muziki Desemba 31 mwaka huu hatua inayohitimisha rasmi enzi ya zaidi ya miaka 40 ya ushawishi mkubwa katika utamaduni wa vijana na tasnia ya burudani.

MTV, iliyoanzishwa mwaka 1981, ilikuwa zaidi ya kituo cha televisheni. Ilikuwa kitovu cha mitindo, muziki na utambulisho wa kizazi kizima, ikizindua Wasanii wakubwa duniani na kuunda lugha ya pamoja ya kitamaduni kupitia video za muziki.

Sababu kuu iliyotajwa na kampuni ni mabadiliko makubwa ya tabia za watazamaji. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hadhira imeacha kutazama muziki kupitia televisheni na kuhamia majukwaa ya kidijitali kama YouTube, TikTok, Instagram pamoja na huduma za streaming zinazoendeshwa na algoriti.

Wataalamu wa masoko wanaona hatua hiyo kama kielelezo muhimu cha mabadiliko ya soko la kisasa.

Ingawa MTV ilikuwa chapa yenye urithi mkubwa, ilishindwa kubadilika kwa kasi inayolingana na mabadiliko ya namna watu wanavyogundua na kutumia maudhui ya muziki.

Kwa muda mrefu, MTV ilitegemea mfumo wa televisheni ya kawaida (linear TV), wakati hadhira yake—hasa vijana—ilihamia kwenye maudhui mafupi, yanayopatikana kwa simu na yanayodhibitiwa na mtumiaji mwenyewe.

Hatua hii inaacha somo muhimu kwa biashara na chapa nyingine: umuhimu wa chapa hauko kwenye jukwaa unalotumia, bali kwenye thamani unayotoa kwa hadhira yako. Majukwaa hubadilika, lakini tabia za watumiaji ndizo zinazoamua mshindi sokoni.

Wachambuzi wanasema kufungwa kwa chaneli za muziki za MTV hakumaanishi mwisho wa chapa hiyo kabisa, bali ni ishara ya mwisho wa enzi ya televisheni kama njia kuu ya ugunduzi wa muziki kwa vijana.

1766711316720.jpg
 
BET nayo wanafuata kwa Afrika na baadhi ya sehemu za Ulaya
Wamiliki wa MTV na BET ni Paramount ambayo inaenda kununuliwa na Netflix
Content zao zitapatikana huko
Channel nyingine za CNN, Discovery, TNT, Cartoon Network nazo zinafuata
DSTv wametangaza kuzifunga kuanzia 1 January
 
BET nayo wanafuata kwa Afrika na baadhi ya sehemu za Ulaya
Wamiliki wa MTV na BET ni Paramount ambayo inaenda kununuliwa na Netflix
Content zao zitapatikana huko
Channel nyingine za CNN, Discovery, TNT, Cartoon Network nazo zinafuata
Hata kina CNN, DW, BBC nk wasipoendana na kasi ya mabadiliko watatundika viatu muda si mrefu
 
BET nayo wanafuata kwa Afrika na baadhi ya sehemu za Ulaya
Wamiliki wa MTV na BET ni Paramount ambayo inaenda kununuliwa na Netflix
Content zao zitapatikana huko
Channel nyingine za CNN, Discovery, TNT, Cartoon Network nazo zinafuata
DSTv wametangaza kuzifunga kuanzia 1 January
MTV Base ni chapa ya runinga ya muziki, ambayo kihistoria iliangazia hip-hop, R&B, na muziki wa Kiafrika, na chaneli tofauti barani Afrika (inayoishia Desemba 31, 2025), Uingereza na Ireland (iliyofungwa 2022), na Ufaransa, inayojulikana kwa kuonyesha sauti za kisasa na kimataifa, kuorodhesha vibao, na kuadhimisha utamaduni wa Kiafrika. Toleo la Kiafrika limekuwa na nguvu kubwa katika ulingo wa muziki wa bara hili lakini linatazamiwa kusitisha matangazo mwishoni mwa 2025 kama mkakati wa mabadiliko makubwa.
1200px-MTV_Base_Africa_(2021).svg.png
 
"Yo! MTV Raps" Hiyo 1988 -1990 tunaangalia kwenye VHS tapes LL Cool J anashuka kwenye Limousine ana rap "I Need Love", mambo ya X CLan, DJ Premier na Guru wa Gangstarr, Leaders of The New School wakiwa na Busta Rhymes, Digital Underground Shock G ana mu introduce dogo mmoja anaitwa Tupac Shakur, Tupac hata hajulikani hapo.

Ukute shows za Fab Five Freddy, Ed Lover, Dr. Dre wamekupangia ngoma za Wanyamwezi kutoka New York mpaka LA, umkute DJ Kid Capri ana scratch, umkute KRS-One na Scot La Rock, umkute Chubb Rock ana flow nonstop, umkute Big Daddy Kane ana flow kama hana akili nzuri, uwakute NWA wana rep West Coast, utafurahi mwenyewe hapo.

Na sisi tukachukua inspirations na DJ Kim Mgomelo wa Kim and The Boyz tukaanzisha mashindano ya Yo! Rap Bonanza Dar es salaam miaka ya mwanzo ya 1990.

Na ITV ilipoanza Tanzania ikaanzisha shooting za video za muziki wa Hip Hop na watu kama Kwanza Unit, Hard Blasterz, Sossy B, Dar Young Mob, Deeplowmatz etc kwa kufuata mfano wa MTV.

MTV imetupa memories nzuri sana.
 
Nina miaka zaidi ya 20 sijaangalia MTV.

Nilikuwa hata sijui kama bado ipo.

Nadhani MTV ilianza kupoteza umaarufu na ushawishi wake kwenye miaka ya mwisho ya 90.

Na ujio wa BET’s 106 & Park ulisaidia kuififisha hiyo MTV.

Hata hivyo, MTV ina mchango mkubwa sana katika Hip-Hop.

Ted Demme ndo aliyeanzisha Yo! MTV Raps.

Ed Lover na Dr. Dre wakaipaisha Yo! MTV Raps.

Hip-Hop ndo iliyoipa chati MTV.

Hopefully kabla hawajafunga kabisa virago vyao watafanya tamasha kama alivyofanya Arsenio Hall….kuwakusanya wasanii wengi wa kipindi hicho na kufanya bonge la tamasha la kufunga stesheni.
 
Nina miaka zaidi ya 20 sijaangalia MTV.

Nilikuwa hata sijui kama bado ipo.

Nadhani MTV ilianza kupoteza umaarufu na ushawishi wake kwenye miaka ya mwisho ya 90.

Na ujio wa BET’s 106 & Park ulisaidia kuififisha hiyo MTV.

Hata hivyo, MTV ina mchango mkubwa sana katika Hip-Hop.

Ted Demme ndo aliyeanzisha Yo! MTV Raps.

Ed Lover na Dr. Dre wakaipaisha Yo! MTV Raps.

Hip-Hop ndo iliyoipa chati MTV.

Hopefully kabla hawajafunga kabisa virago vyao watafanya tamasha kama alivyofanya Arsenio Hall….kuwakusanya wasanii wengi wa kipindi hicho na kufanya bonge la tamasha la kufunga stesheni.
MTV na BET are not completely shutting down
Wanaondoa tu ile non stop music wanabaki na reality shows na entertainment nyingine
Inapunguza channel zake baadhi ya maeneo duniani
US na Canada bado itaonekana
Content nyingi za music watu wanapata kupitia Spotify, Tik Tok na You Tube
Wanahamia Paramount + baada ya merger/acquisition ya Skydance Media
 
MTV na BET are not completely shutting down
Wanaondoa tu ile non stop music wanabaki na reality shows na entertainment nyingine
Inapunguza channel zake baadhi ya maeneo duniani
US na Canada bado itaonekana
Content nyingi za music watu wanapata kupitia Spotify, Tik Tok na You Tube
Wanahamia Paramount + baada ya merger/acquisition ya Skydance Media
Kwani BET na MTV bado walikuwa wanaonyesha music videos?

Nilishaacha kuangalia hizo chaneli zamani sana.

Hata subscription ya cable na satellite sina.
 
Back
Top Bottom