Mfano:kuna mwanamke umempenda na unamtaka,kila kukicha ww unampigia simu na mara zote unapomtafuta yeye huwa yuko nyumbani,ukiacha mida ya kazi(hata ukisema umtegee umpigie usiku sana atapokea na mtaongea vizuri tu na anakwambia kabisa kuwa yuko nyumbani)sasa swali langu ni kuwa mwanaume anapokutana na mwanamke wa namna hii,anafurahia au anamshangaa kuwa kwanini hajichanganyi?.
jamaa alishindwa nini kuwa wazi kwamba asingeweza kuendelea na uhusiano na huyo dada kutokana na situation aliyomkuta nayo... kusepa kimyakimya ni kuonyesha kwamba huna balls za ku-face reality head-on
Watu wanatofautiana,na si kila mtu anaweza kuwa na guts za kusema kila kitu kilichoko moyoni mwake. Ndiyo maana kuna watu wanajua sana kupepesa mdomo wakati wengine wanongea kwa vitendo. Kila njia ina madhara yake!
Babu DC!!
Vipi tena wewe? Au wewe ndiye Candy?
Babu DC!!
Ila sikujua kama kuwa mtalikiwa ni hasara.
Nimepokea ombi maalum toka kwa mama chanja wangu mtarajiwa ,anasema kuna mtu kamwomba ushauri,katika hili naye anaomba mchango wenu.
Ni hivi:
Kuna mdada mmoja (tumwite Cindy), Cindy aliolewa na akaachika.Alipata watoto wawili kwenye ndoa yake na anaishi mwenyewe na wanae.Majuzi kuna baba mmoja aliingia kwenye ofisi ya dada yake Cindy (tumwite Brenda) na hapo ofisini huyo baba aliona picha ya Cindy na akamtunuku. Alijitahidi kuomba contact za Cindy lakini Brenda akawa anakataa.Jamaa king'ang'anizi pamoja na Cindy kumwambia dada yake asitoe contact zake lakini tokana na presha yajamaa mwisho Brenda alimpa jama namba ya Cindy.Zikanza simu na sms zisizoisha mpaka Cindy akakubali akutane na jamaa.Wakakutana,wakala,wakanywa,in the process Cindy akamweleza jama ukweli kuwa yeye ni divorcee with two kids.Kuanzia siku hiyo hajamsikia wala kumwona jamaa tena.
Cindy anajiuliza hivi jamaa kakimbia kisa ana watoto? Au kisa ni u divorcee?apparently dada yake kumbe hakumweleza jamaa kuwa cindy aliwahi kuolewa na ana watoto.
Hivi wanaume mnakerwa kuwa na mwanamke mwenye watoto/divorcee,kwa nini?
huyo mwanamme sie kabisa,yani kusikia ana watoto unatoka mbio loh mungu asinikutanishe na kiumbe kama hiko..
Dark City,
nimegundua mambo ni magumu kuliko nilivyofikiri.
Ila huyo nampongeza mwanamme huyo kuondoka mapema kabla madhara makubwa hayajafanyika.
Huyu Cindy naye pole zake naona alijipa matumaini makubwa mapema mno.
Ila sikujua kama kuwa mtalikiwa ni hasara.
Huyo mwanaume ****, vipi utamwingia mtu bila kufanya fact findings?
Ni vigumu kusema moja kwa moja kwa sababu binadamu tunatofautiana. Kuna watu wanapenda mwanamke au mwanamume ambaye hajichanganyi kabisa. Hata hivyo kuna watu wanachukia tabia ya kutojichanganya.
Binafsi napenda mtu ambaye yuko katikati..siyo chakaramu sana wala mother house wa kukaa jikoni 24/7!
Babu DC!!!
Hoja ipi tena kamanda,
Tumeshakueleza kuwa huyo dogo (mwanamume) kichwani ni mzima sana...
Lingine ni jipi?
Babu DC!!
kama aligonga mzigo halafu akaingia mitini kwa style hii atakuwa amemuumiza sana huyo dada.... why leave her guessing nini chaweza kuwa cause ya kukimbia kwake?
Samahani sana kwa wale ambao hawatapenda comment hii,....hata hivyo huwa nalisema hili mara nyingi!
Mwanamke mwenye watoto anatakiwa kutafuta mwanamume ambaye ana watoto kama yeye. Ni kosa kubwa kwa mwanamume kujidanganya na kumwoa mwanamke mwenye mtoto/watoto.
Nayasema haya kutokana na uzoefu na wala siyo kwa nia mbaya ya kuwanyanyapaa dada zetu. Ndiyo maana huwa nawashauri wajukuu zangu kwamba, kama inawezekana, mtu asizae kabla ya ndoa!
Samahani tena kwa post hii,
Babu DC!!
Naomba nikufahamishe kuwa kitendo cha kuwa mtalaka ni kizito...afadhali hata kuwa mjane....Kila mtu unayekutana naye lazima ajiulize kwanza; kwa nini alishindwa kudumu katika mahusiano yake ya awali....?
Na kwa mtu ambaye anaongozwa na akili zake zote (siyo tamaa ya ngono), hataweza kuamini kwamba mhusika hana kosa au mchango wowote katika kuvunjika kwa mahusiano yake ya awali! Na mhusika mara nyingi atakuwa na hisia kwamba labda anaonekana mkorofi/mkosefu, kiasi cha kusababisha mahusiano yake ya awali kuvunjika. Hili linafanya mchakato wa kujenga uhusiano mpya uwe mgumu sana kwa pande zote mbili, labda kama wahusika wamekaa kimaslahi zaidi!
Babu DC!!