Uwanja unabeba watu 10,000 na una mageti 8 unaweza kuniambia sababu zilizomfanya afungue geti moja pekee
Yaweza kuwa vyombo vya mafuta na pia walitarajia utaratibu wa kupanga mstari lakini watu wakavamia kila mmoja anataka awe wa kwanza. Tuliza kichwa mkuu.
Kwa hali why tusilifananishe na tukio la kibwetere la Uganda
Kibwetere alikuwa na mahubiri na mafundisho tofauti sana mkuu, ndio maana nikahoji, kuna tatizo gani kwenye hayo mafundisho ya Mwamposa in relation to the incidence? Hoja iko hapo, mihemko pembeni. Ya kibwetere hata teolojia yake haikuwa salama kwa wanadamu, sasa teolojia ya Mwamposa ina tatizo gani kiusalama? Tuache chuki binafsi.
Then umezungumzia kuhusu theology unajua elimu hii inasema nini kuhusu huu uongo wa hawa wanajiita mitume na manabii?
Mimi ni mpingaji namba moja wa teolojia. Hii ni elimu ya kum-define Mungu kwa mtazamo wa mtu ama kikundi cha watu. Huko ndiko huzaliwa viu kama statement of faith. Ni mambo haya yabteolojia yaliyoingiza imani potofu kwenye kanisa, ibada ambazo hazina sapoti ya biblia. Kumbe basi natazama Neno la Mungu zaidi kuliko kusikiliza mwana teolojia amesema nini.
Unapozungumzia mafuta mafuta kile kitu ni sacred ni kitakatifu kama kitu ni kitakatifu unaweza kukimwaga chini chini ili watu wakanyage?.....unajua tafsiri ya kukanyaga kitu ni ishara ya dharau na kukikosea kitu thamani
Ni wapi imeandikwa mafuta ni matakatifu? Mafuta yatabaki mafuta tu, ila kwa imani watu huamini kilichonenwa juu ya mafuta hayo kitawapa matokeo. Kumwaga chini? Hapa sijakuelewa mkuu, mafuta huwekwa kwenye vyombo ili watu wakanyage, miguu ikiwa sehemu ya mwili.
Nachelea kuongea sana kwa sababu mimi pia siamini katika mafuta ila najenga tu hoja kwamba watu wanamhukumu Mwamposa kwa kufuata hisia binafsi juu ya huduma yake. Hakuna sehemu kwenye biblia inaposema ukimwaga mafuta mwenye vyombo watu wakanyage ni dharau.
Alafu unatuaminisha mafuta ya upako kitu kitakatifu kinatunzwa na kama wangekuwa kweli wanaelewa wasingekikosea heshima hivi.....sababu hii ilitosha kabisa kuona huyu ni MUONGO na TAPELI
Yesu aliponya kwa mate, nadhani ungekuwepo enzi hizo ungempiga mawe. Tatizo lako unadhani Mungu anaangalia heshima za nje ambazo kimsingi ni unafiki mkubwa, Mungu anaangalia ROHO YAKO. Hili ndilo lilipelekea Mungu kuwekwa kwenye vyombo makanisani pia, akatunzwa sakaristia. Matokeo yake wengine kama kina Bulldozer wamemweka kwenye mafuta, kwa nini basi uwanyooshee kidole?
Kwa kanisa katoliki mafuta matakatifu ya Krisma yanatumika mwaka mzima yanayobaki HUZIKWA kwa heshima maana ni kitu kitakatifu
Tusitetee uongo elimu haitoshi tu kutuondolea ujinga pia itongezee maarifa
Sent from my iPhone using JamiiForums
Elimu itakupa maarifa ni kweli, lakaini maarifa ya dunia hii. Elimu ya Mungu itakupa ujuzi wa ufalme wa mbinguni. Hakuna chuo cha teolojia kina uwezo wa kufundisha hili zaidi ya mashindano ya doctrines kwamba kwa nini sisi tunaamini hivi na wao wanaamini vile.
Kumbuka tangu kale na HATA SASA Mungu alivichagua vitu vinyonge na vidhaifu ili kuviaibisha vikubwa na vyenye nguvu. Unaielewa hiyo?
Kama maprofesa wanakwenda kunywa kikombe cha babu, ama kukanyaga mafuta ya upako, yako wapi maarifa hayo unayosema? Elimu ya Mungu itabaki kuwa hivyo na ya dunia kadhalika.
Kuhusu kuzika vitu vitakatifu, Mungu wa leo hakai kwenye vitu bali akaa kwenye roho zao wamtafutao kwa bidii. Habari za ukigusa hostia utapatwa kichaa sio biblical bali ni mafundisho ya kibinadamu. Tusimshushe Mungu wetu hivyo, tumheshimu kama alivyotaka. Ndio maana leo hii hatuendi kuhiji Israeli kwa sababu hakuna tena ya kuabudu mlima huu wa ule.
Tusome biblia.
Sent from my SM-T355Y using Tapatalk