Mtu mwenye degree anapoenda kujifunza kazi ya waliokosa Elimu ni ujumbe gani tunapata kuhusu Elimu yetu?

Ralph Tyler

JF-Expert Member
Jul 31, 2015
2,827
3,569
Nimetoka kuzungumza na mpwa wangu sasa hivi anaomba msaada wa cherehani akajifunze kushona nguo, ndio mradi aliobuni baada ya kusota miaka 2 bila ajira. Amesoma ana degree Bachelor of Arts in Community and Development Studies.

Kaniambia ameshapata mtu wa kumfundisha na mahali pa kujifunzia (baraza fulani hivi). Ninavyofahamu huyo fundi cherehani atakayekuwa anamfundisha mpwa wangu kushona ana elimu ya darasa la saba tu, jamani! Huyu fundi atapata ujumbe gani kuhusu kusomesha mtoto?

Hivi kweli ni sawa kijana asome hadi elimu ya university aishie kuja kufundishwa ushonaji na mtu wa la saba? Kulikuwa na sababu gani ya kupoteza gharama na muda wote huo, si bora tu angeenda ushonaji alipomaliza la saba, labda sasa hivi angekuwa mbali sana. Au kuna mahali tunakosea katika elimu hizi, tuna universities nyingi na courses nyingi lakini kumbe wanachohitaji watu ni ufundi cherehani tu! Tunahangaika na mambo makubwa ya gharama kubwa bure tu!

Interestingly mpwa wangu ana shauku kubwa ya kutekeleza mpango wake huu, anauchukulia serious kabisa, anaanza kesho rasmi! Namtakia kila la heri lakini kwa kweli nashangaa tu, mimi katika makuzi yangu niliona degree ni level kubwa sana, si ya kutumia kwenye cherehani. Lakini basi ndiyo imeshakuwa hivyo.

Tunakwama wapi?
 
Maisha ni kama gwaride. Ukisikia nyuma geuka ndy hiyo ya mpwa wako!

Kipindi hiki ukikumbatia hadhi ya elimu kulinganisha na kazi inayopatikana mtu afanye, kuna hati hati akaozea nyumbani.

Hapo swala siyo status ya elimu ya mpwa wako bali ni atafanyaje ili kutengeneza msingi wake wa maisha apate hela.

M-bariki huyo mpwa, acha kunungunika.
 
Nafikiri tatizo si elimu ila tatizo ni mpwa kuitumia Hiyo elimu

Elimu haikuanzishwa ili Watu waajililiwe ila ilanzishwa ili Watu waweze kutawala mazingira yao vizuri kwa uarahisi

Tunapokwama tunachukulia elimu ni kama njia ya kuajiliwa badala kuchulia kama njia ya kutufungua ufahamu wa kutawala mazingira
 
Kumbuka mpwa kakosa connection akipata connection in three or two year anakuwa na ukwasi au mali zaidi ya uyo fundi ila uyo fundu kitu kupata connection akabadili game faster kama mpwa pengine abet au ashinde tatu mzuka

Kwaiyo usimdharau mpwa ni mapito tu sema mpwa naye yupo porini sana nini si aendeshe hata boda boda afungue milango ya connection kwa kukutana na watu yani umesoma unatafuta kazi alafu unaenda kufanya kazi ya kukaa ukutani na wadau inatakiwa ajichanganye akapige hata vibarua vya ujenzi uko, au kupiga debe stand yani mixing style
 
Kasoma Art and community development, Sasa ushonaji sio Art kweli? Hapo changamoto ni hiyo kujifunza kibarazani locally but kama ameridhia mwenyewe sioni tatizo.

Kikubwa apate ujuzi wa kushona, kwa kutumia hiyo degree yake Sasa ndio ataboresha aina na mitindo ya mishono, Pia mashine za kushonea za kisasa zaidi na ofisi kubwa kama mbunifu wa mavazi badi kuwa na cloth line. Kwani kina Dickie's etc walianzaje?

Umeshindwa kumsaidia mpwa wako kwa hiyo decent job unayoiweza Wewe na bado unataka kuua ndoto yake ya kujikomboa? Jaribu kuwa na mawazo na mchango chanya kwenye mipango ya watu. Hakika baraka utaziona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapi ilipoandikwa kwamba mtu akiwa na degree lazima aajiriwe?
Wazazi wengi bado tuna mindset za kuwasomesha watoto wetu ili baadae waje waajiriwe.Ajira sasa hvi ni tatizo la dunia nzima. Hivyo kujiajiri ndiyo itasaidia kupunguza hilo tatizo. Na wakati mwingine kujiajiri hakuangalii una elimu gani na umesomea fani gani, ingawa naamini mtu aliyesoma anaweza kujiajiri na nkufanya vizuri zaidi kama atakuwa serious.

Kama huyo kijana ana passion ya kushona nguo anaweza akajiendeleza mdogo mdogo baadae akaja kuwa hata na kiwanda kidogo cha kushona nguo na hata akaajiri vijana wengine. MAISHA HAYANA FORMULA!
 
Back
Top Bottom