Mdomo wa sungura Kwa Sasa sio inshu , mtoto atarekebishwa na atakaa Vizuri.
Watoto Hawa changamoto yao kubwa Huwa ni katika lishe , na hivo basi ili Kumlinda na kumsaidia ,hakikisha Mama anajitajidi sana kumlisha Kwa angalau Mara 10 Kwa siku .
Mdomo wa sungura wenyewe kama wenyewe haihitajiki haraka kuurekebisha ila Hawa watoto wakati Fulani wanakua na Matatizo mengine Ivo ni vema umpeleke Hospital Kwa ajili ya uchunguzi zaidi .
Habari njema, Huduma za Hawa watoto ni Bure Bure Kabisa Tena Kwa TAASISI nyingine zinazotoa huduma zao ,Hadi Nauli wanakutumia.
Kuhusu Uzito mkubwa 6Kg, nadhan Kwa Tanzania ,mtoto wako amejivunjia rekodi yake,. Ni jambo la Heri mtoto kua na uzito ila wakati Fulani ni kiashiria Cha Matatizo ya ki genetic au Matatizo Kwa Mama au baadhi ya Medical conditions zinazopelekea uzito kua mkubwa ...na hivo Unawajibika Kumpelekea Mtoto Hospital Kwa uchunguzi zaidi .
Kuhusu Hosp , inategemea ni Wapi ulipo, kama upo Kanda ya Ziwa, Njoo Bugando chap !!.
Mwisho, Zingatia sana sana Lishe Kwa mtoto , Zingatia kwenda Hosp Kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa mtoto
Watoto Hawa wanakuaga na Akili Sanaa☺️☺️