kijanamtanashati
JF-Expert Member
- Aug 22, 2014
- 516
- 890
Nakumbuka mimi nilipokuwa na umri 6-13 nilikuwa mkorofi natukana sana watu sichagui mkubwa au mdogo, nilikuwa na matusi hatari na kupenda kurushia watu mawe, pale mtaani wakawa wanamwita mama yangu 'mama mawe'. Hadi watu wazima wakawa waniogopa kwa matusi. Mtu akinichokoza mbona ataisoma namba yeye na familia yake, nakusanya mawe mengi halafu naenda kurusha juu ya bati na mlangoni kwao basi huko ndani zinatoka sauti 'wee mama mawe mwao ameanza mkataze mwanao'.
Nyumbani kulikuwa na shamba la mipapai basi majirani wakija kuomba mapapai kama mama hayupo wakinikuta mimi wanagairi hata kuomba. Au wakimkuta mdogo wangu na yeye anawaambia muombeni kaka, basi wanagairi utasikia 'mtoto ana matusi yule unatafuta kuporomoshewa matusi'. Kuna kipindi mpaka wazazi wa pale mtaani waliwakataza watoto zao wasicheze na mimi. Ila baadae nilibadilika baada ya kumaliza shule ya msingi nikawa mtoto wa kawaida mpaka watu wakawa wanashangaa.
Sasa hivi nina mtoto wa kiume miaka 5, kila siku naletewa kesi zake amevunja vitu vya watu kwa mawe. Ugomvi wake wa mawe akichokozwa anaporomosha mawe. Aliwahi kuvunja kioo cha gari cha watu nikaletewa kesi ilinibidi nilipe. Amevunja vioo nyumbani kwa majirani mara tatu na jana amempasua mtoto wa jirani kichwani kwa jiwe mpaka ikabidi tumpeleke hospitali. Mama ake anampiga sana lakini hasikii, anapigwa leo kipigo cha mbwa mwito kesho anarudia tena kurusha mawe akichokozwa. Mimi pia nimeshampiga mara kadhaa, nimemtishia kumpeleka polisi lakini wapi. Ukimuliza kwanini unapiga watu mawe anajibu 'wenyewe wananichokoza'. Mama yake anadai tumpeleke bording labda atabadilika lakini mimi sikubaliani na wazo hili, mtoto wa miaka 5 bado mdogo sana kukaa mbali na wazazi. Halafu watoto huko bording wanaharibika sana hasa hawa wa kiume. Wakuu nisaidieni nifanye ili huyu mtoto aache hii tabia maana huko anakoelekea anaweza kuja kuua mtu kwa mawe.
Nyumbani kulikuwa na shamba la mipapai basi majirani wakija kuomba mapapai kama mama hayupo wakinikuta mimi wanagairi hata kuomba. Au wakimkuta mdogo wangu na yeye anawaambia muombeni kaka, basi wanagairi utasikia 'mtoto ana matusi yule unatafuta kuporomoshewa matusi'. Kuna kipindi mpaka wazazi wa pale mtaani waliwakataza watoto zao wasicheze na mimi. Ila baadae nilibadilika baada ya kumaliza shule ya msingi nikawa mtoto wa kawaida mpaka watu wakawa wanashangaa.
Sasa hivi nina mtoto wa kiume miaka 5, kila siku naletewa kesi zake amevunja vitu vya watu kwa mawe. Ugomvi wake wa mawe akichokozwa anaporomosha mawe. Aliwahi kuvunja kioo cha gari cha watu nikaletewa kesi ilinibidi nilipe. Amevunja vioo nyumbani kwa majirani mara tatu na jana amempasua mtoto wa jirani kichwani kwa jiwe mpaka ikabidi tumpeleke hospitali. Mama ake anampiga sana lakini hasikii, anapigwa leo kipigo cha mbwa mwito kesho anarudia tena kurusha mawe akichokozwa. Mimi pia nimeshampiga mara kadhaa, nimemtishia kumpeleka polisi lakini wapi. Ukimuliza kwanini unapiga watu mawe anajibu 'wenyewe wananichokoza'. Mama yake anadai tumpeleke bording labda atabadilika lakini mimi sikubaliani na wazo hili, mtoto wa miaka 5 bado mdogo sana kukaa mbali na wazazi. Halafu watoto huko bording wanaharibika sana hasa hawa wa kiume. Wakuu nisaidieni nifanye ili huyu mtoto aache hii tabia maana huko anakoelekea anaweza kuja kuua mtu kwa mawe.