Not true not fair assessment. Serial killers wako sehemu zote Duniani. Watu wa aina hii ni sawa na terrorists. Hawana la kupoteza na wameshajiamini wao ni watu wa kufa na kupona. Kinachoweza kulaumiwa hapa ni sababu ambayo inaonekana ni ushirikina. Kwa nini tufikie kiwango hicho? Ilikuwa Mbeya na ngozi za binadamu, Ikawa kanda ya ziwa na albino na sasa tena Njombe. Watu wakauza hata watoto, waume, wake zao albino! Kuzuiya hiyo siyo polisi tu.
Ninachoomba kwa wakati huu atakayethibitika, atiwe kitanzi. Ni aibu kwamba waliokamatwa na ngozi za binadamu au mauaji ya albino, hukumu zao hazikutangazwa sana ili kukomesha mitindo hiyo. Kinachofahamika ni kwamba kuna uhusiano na chaguzi za kisiasa. Tunapata wansiasa walio na akili mbovu kiasi hiki cha kutegemea mauaji tukliamini watatuondolea matatizo yetu ya maendeleo, Never!!!