Mtoto Mgongoni, Mwingine Tumboni, Jembe begani, Mzigo Kichwani

muhosni

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
1,108
152
Mama!

Nakuheshimu mama.

Umetoka shamba, umechoka, umembeba mdogo wangu mgongoni na ujauzito. Jembe lako hukuacha shambani, umeleta kuni na mboga za majani. Mimi ndo nimerudi shule, sijala na sielewi kiasi ulivyochoka. Mimi ni mtoto wa kiume baba kanikataza kuingia jikoni.

Mama umejitahidi kupika umenituma nikateke maji, kisha nikanunue mafuta ya kupikia koroboi moja. Hatimaye tukala. Unampenda baba mama, ukamwachia chakula.

Giza limeingia, unaogesha mtoto na mimi unaniharakisha nioge baba asije kukugombeza. Mafuta ya taa yamekwisha mama, hakuna pesa ya kununua. Moto unatusaidia mwanga.

Baba anaingia anaimba, amelewa! Anakuita kwa sauti ya ukali, unaitika kwa heshima, unatoka kwenda kumfungulia nyumba yake. Unamfunulia chakula na kumkaribisha. Anatazama chakula anahamaki "Chakula gani hiki wewe mwanamke, hata ukimpa mbwa hali?"

Maneno yanayofuata siwezi kuyarudia mama, pole sana. Baada ya kusikiliza hotuba ndefu, na baada ya baba kupitiwa na usingizi, unafunga mlango wake unakuja kwetu kulala mama.

Mara narudi nyumbani, nakuta hakuna mtu. Shangazi ananiambia mama kalazwa hospitali, "kapewa mtoto". Mara baada ya miaka kadhaa mama, ukanipatia wadogo zangu saba.

Ulipenda tusome mama, hukuwa na uwezo
Ulipenda tuwe na afya mama, hukuwa na uwezo
Ulipenda uvae vizuri mama, hukuwa na uwezo

Mtoto wa nane mama, ukaaga naye dunia. Nyerere angekuwa bado madarakani mama usingekufa kwa sababu hizo. Kukosa huduma, muuguzi hakujali.

Baada ya kifo chako mama, hadithi ni chungu zaidi na ndefu sana.

Kokote uliko mama, nakupenda sana na leo ni siku yako tukufu!
 
Nami pia ninawapa pole wa-mama wa vijijini zaidi coz yanafanana yanayowakuta. Imekaa poa sana na nakaribia kuifananisha na simulizi niliyotokea kuisoma kurasa zake tatu za mwanzo ya 'barua ndefu kama hii' kwa mpangilio wa maneno yake ulivyo. nzuri sana
 
Nyuma baba na panga na mkwaju!!this is africa wakawaka ehe waka waka.........
 
Nami pia ninawapa pole wa-mama wa vijijini zaidi coz yanafanana yanayowakuta. Imekaa poa sana na nakaribia kuifananisha na simulizi niliyotokea kuisoma kurasa zake tatu za mwanzo ya 'barua ndefu kama hii' kwa mpangilio wa maneno yake ulivyo. nzuri sana
Mgongee basi pale mahala mkuu............
 
Mkuu acha bana, hii ina urefu gani jamani??!!!!!!!!! Imetulia sana, dedication to all women who suffer for the sake of their children especially in rural areas.

Kudos kamanda.

I salute you mkuu!
 
Mkuu acha bana, hii ina urefu gani jamani??!!!!!!!!! Imetulia sana, dedication to all women who suffer for the sake of their children especially in rural areas.

Kudos kamanda.

na ikifupishwa sana inapoteza ladha, au ndiyo yupo neticafee muda haumruhusu. mi naringa na kisimu changu cha mkononi
 
Jamani tuwasaidieje hawa wanawake wa vijijini? mawazo/busara/uzoefu/utaalamu wako unahitajika please
 
Duh!! mbona kama nataka kutoka machozi?????

Mkuu nitaipata katika kitabu gani?? tupatie part II ulivyohangaika na wadogo zako 7 mpk leo upo hapo ulipo!!

i like the story!!
 
na ikifupishwa sana inapoteza ladha, au ndiyo yupo neticafee muda haumruhusu. mi naringa na kisimu changu cha mkononi

Mkuu kwa sasa natumia mtandao wa mkoloni wangu, nikitoka kazini ndo natumia simu. Kwani imekuwa fupi sana mkuu?
 
Duh!! mbona kama nataka kutoka machozi?????

Mkuu nitaipata katika kitabu gani?? tupatie part II ulivyohangaika na wadogo zako 7 mpk leo upo hapo ulipo!!

i like the story!!

asante Susy,

haipo kwenye kitabu chochote, kichwani na moyoni. Am sure hata wewe kuna namna unakumbuka mama yako alivyopata shida, katika mazingira tofauti lakini ni shida zinazotokana na kule yeye kuwa mwanamke tu
 
Mkuu kwa sasa natumia mtandao wa mkoloni wangu, nikitoka kazini ndo natumia simu. Kwani imekuwa fupi sana mkuu?

siwezi kusema kuwa ni fupi sana ila siyo refu. up to now, nimeshairejea zaidi ya mara moja kuisoma coz haichoshi
 
Mama!

Nakuheshimu mama.

Umetoka shamba, umechoka, umembeba mdogo wangu mgongoni na ujauzito. Jembe lako hukuacha shambani, umeleta kuni na mboga za majani. Mimi ndo nimerudi shule, sijala na sielewi kiasi ulivyochoka. Mimi ni mtoto wa kiume baba kanikataza kuingia jikoni.

Mama umejitahidi kupika umenituma nikateke maji, kisha nikanunue mafuta ya kupikia koroboi moja. Hatimaye tukala. Unampenda baba mama, ukamwachia chakula.

Giza limeingia, unaogesha mtoto na mimi unaniharakisha nioge baba asije kukugombeza. Mafuta ya taa yamekwisha mama, hakuna pesa ya kununua. Moto unatusaidia mwanga.

Baba anaingia anaimba, amelewa! Anakuita kwa sauti ya ukali, unaitika kwa heshima, unatoka kwenda kumfungulia nyumba yake. Unamfunulia chakula na kumkaribisha. Anatazama chakula anahamaki "Chakula gani hiki wewe mwanamke, hata ukimpa mbwa hali?"

Maneno yanayofuata siwezi kuyarudia mama, pole sana. Baada ya kusikiliza hotuba ndefu, na baada ya baba kupitiwa na usingizi, unafunga mlango wake unakuja kwetu kulala mama.

Mara narudi nyumbani, nakuta hakuna mtu. Shangazi ananiambia mama kalazwa hospitali, "kapewa mtoto". Mara baada ya miaka kadhaa mama, ukanipatia wadogo zangu saba.

Ulipenda tusome mama, hukuwa na uwezo
Ulipenda tuwe na afya mama, hukuwa na uwezo
Ulipenda uvae vizuri mama, hukuwa na uwezo

Mtoto wa nane mama, ukaaga naye dunia. Nyerere angekuwa bado madarakani mama usingekufa kwa sababu hizo. Kukosa huduma, muuguzi hakujali.

Baada ya kifo chako mama, hadithi ni chungu zaidi na ndefu sana.

Kokote uliko mama, nakupenda sana na leo ni siku yako tukufu!

nice..but mmh..hadi machozi..
 
pole kwa kupoteza mama yako mpenzi. ubarikiwe sana muhosni kwa jinsi unavyowathamini kinamama wote kwa heshima ya amamko uliyempenda. damu na nyama havikukufunulia haya ila baba yetu aliye mbinguni.

Glory to God
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom