sikuwahi kudhani
WALIMWEUSI ni mwanamke, sijui kwa nini..... unisamehe kwa hilo rafiki.....
Mi naona umefanya jambo zuri sana..... hutakuja kujuta kwa hili, na nina uhakika kuna siku kaka yako atakushukuru kwa hili.
Kama upo close na wifi yako, mimi nakushauri unaweza kumwambia, ila umwambie in such a way that asione mumewe ana kosa (sijui itawezekanaje hapa! ila unaweza kumwambia kulikuwa na hii story lakini kaka kakataa, na kwamba unamsaidia yule dada huyo mtoto sababu ulikuwa unamchukulia mamake kama mdogo wako wakati mnakaa naye. uliona maisha yamekuwa magumu so unamsaidia yule dada, hata kama mtoto siyo wa kakako), ukizingatia mtoto alipatikana kabla yeye hajaolewa....
unajua kwa nini nakushauri wifi ajue? huyo ni mtoto ambaye karibia watu wengi wa familia wanalijua....
maneno yanatembea, amini usiamini, siku wifi yako atakuja tu kujua kuwa huyo ni mtoto wa kaka yako.
wifi atakuchanganya na wewe kuwa ndo wale wale, mnamchekea machoni lakini hamna lolote.
kama kakako angekuwa kakubaliana na hiyo ningekushauri umwambie kakako amwambie mkewe.
Hii ni ngumu sana, wewe ndo unamfahamu wifi yako, na huwezi kujua, wifi anaweza akalipokea positively.... siyo wamama wote hawapendi watoto wa waume zao wa kabla ya ndoa