bahati30
JF-Expert Member
- Oct 15, 2012
- 1,625
- 883
Habari zanu wana JF,
Naombeni ushauri wenu katika hili lililonikuta, ni story ndefu ila in short miaka ya nyuma kipindi tukiwa tunasoma, our mom alikuwa anaishi na kabinti fulani, by that time she was 10 yrs na kiliacha shule kutokana na matatizo ya wazazi wake so kikawa home kinamsaidia mom kazi ndogondogo tu na kumpa mom kampani. Tulimchukulia kama mdogo wetu na tulimpenda sana. After two years my sis aliyekuwa anaishi DSM alijifungua so akamchukua kuishi nae ili amsaidie kazi. Kaka yetu mmoja by that time alikuwa anasoma alikuwa akiishi hapo kwa sister.
After two years binti akagundulika kuwa mjamzito na alipoulizwa nani mhusika alisema ni huyo kaka yangu ila yeye alikana kabisaaaaa!!!Binti wa watu akarudishwa kijijini na alijifungua mtoto wa kike akiwa na miaka 15. Mwaka juzi nilienda kijijini na nikabahatika kumuona huyo mtoto, honestly she resembles my brother kabisaaaaa!!! Nilimpigia na kumweleza kuhusu hilo but alisema kuwa yeye hahusiki na kama anafanana na yeye it is not his business. Huyo mtoto alikuwa anaishi maisha magumu sana imagine at the age of 12 hajaanza darasa la kwanza. ilimuomba mama yake nimchukue niishi nae na pia nimsaidie kwa vile yule kweli ni mtoto wa kaka yangu!
Kwa vile bro alishakataa hata nilipomwambia kuwa mtoto kafanana nae, sikumshirikisha uamuzi wangu niliouchukua wa kumlea huyo mtoto ila mom nilimshirikisha na hakuwa na tatizo na yeye toka zamani alishataka kumchukua ila bro alimkataza so ikabidi aheshimu uamuzi wake. Hadi sasa naishi nae na the girl is very inteligent, amini usiamini nilipompeleka shule walimpa mtihani na kugundua kuwa hakustahili kuanza drs la kwanza, wakampeleka la 3 now yupo la 5.
Last week mke wa huyo brother alikuja kwangu kunitembelea na kumuona yule mtoto, akaniuliza mtoto wa nani?Nikamjibu ni mtoto wa shemeji yangu ili kuua soo wasie gombana na mumewe. Sasa jana narudi toka job namkuta brother kwangu kafura vibaya sana na anadai mimi ninadharau kwa nini nimemchukua mtoto ambae sie wake na amedai kuwa mimi na yeye undugu wetu umeisha na akaondoka bila hata kuniaga.
Naombeni ushauri wenu katika hili mana that brother of mine ni mbabe balaa, yani ndugu wanamwogopa balaa isipokuwa mimi tu!!
Nawakilisha.
Awali ya yote nikupongeze kwa uamuzi mzuri ulioufanya. Wewe ni mmoja kati ya watu wachache ambao wangeona ipo haja ya kuchukua uamuzi kama huo. Huyo kaka yako asikuumize kichwa coz mimi kwa mtizamo wa haraka naona kma huyo bro wako ana MAPEPO na anahitaji msaada wa maombi ya haraka ili kumtoa katika hali aliyo nayo. ATAWEZAJE KUIKATAA DAMU YAKE? YEYE ALIVYOSHIRIKI HILO TENDO HAKUJUA KWAMBA KINACHOTOKEA NI NINI? AU ANASUBIRI MTOTO AKISHAKUWA MKUBWA NA MWENYE FUTURE NZURI NDIO AKUBALI KWANBA HUYO NI MWANAE? Ushauri: Endelea kumhudumia huyo mtoto na usiogope vitisho vya huyo bro wako. Kwa kuwa wewe una maisha yako binafsi wewe jikite zaidi kwenye masuala yanayokuhusu wewe mwenyewe MPOTEZEEEEEEEE......................Akili ikimkaa vizuri atarudi. Pole