Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Kumekuwa na huu mtindo wa magari ya polisi au breakdown kuziba service road asubuhi kwenye barabara ya bagamoyo ili wale wanaochepuka warudi kuunga na foleni kama wengine.
Ni kwamba wamekosa njia kabisa ya kupunguza foleni asubuhi mpaka kuamua kuziba service road? Halafu cha kuchekesha ni kwamba ni service road ya upande mmoja tu wa kulia ndio huwa inafungwa (ukiwa uelekeo wa kwenda Mwenge), huku ya upande mwingine magari yakichepuka kama kawaida! Sasa hapo wamesuluhisha nini?
Kutumia service roads wakati barabara kuu haina tatizo ni kosa, na wanahatarisha maisha ya watembea kwa miguu lakini suala la foleni asubuhi ni kichomi na utaratibu wa kuruhusu magari asubuhi ni mbaya, ndio maana madereva wanaona bora kuchepuka tu.
Trafiki/Polisi mnaweza kufanya vizuri zaidi ya hivi.
Kutumia service roads wakati barabara kuu haina tatizo ni kosa, na wanahatarisha maisha ya watembea kwa miguu lakini suala la foleni asubuhi ni kichomi na utaratibu wa kuruhusu magari asubuhi ni mbaya, ndio maana madereva wanaona bora kuchepuka tu.
Trafiki/Polisi mnaweza kufanya vizuri zaidi ya hivi.