JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Akiongea mara baada ya mafunzo hayo Februari 20, 2024 katika chuo cha Ufundi Arusha kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini Naibu kamishna wa Polisi DCP Ramadhani Ng’anzi amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wakaguzi wa magari ili kwendana mifumo ya kiksasa na magari ya kisasa yanayoingia nchini.
Kwa upande wake Mkuu wa idara ya Uhandisi Magari kutoka chuo cha ufundi Arusha Injiania David Mtunguja amesema chuo hicho ni miongoni mwa vyuo bora Afrika katika idara ya uandishi magari ambapo amebainisha kuwa endapo wakaguzi wa magari watasoma katika chuo hicho watapata maarifa mazuri na bora katika utendaji wa kazi zao.
Nae Mkurungenzi wa udhibiti Usafiri wa Barabara kutoka Latra Bw. Johansen Kahatano amesema chuo cha ufundi Arusha kimejipanga vizuri katika maswala ya usalama barabarani huku akisema chuo hicho kinashirikiana na mamlaka ya udhibiti usafiri Ardhini (LATRA) katika kuboresha mifumo ya utambulisho ya njiani za mabasi hapa nchini.
Mkuu wa chuo cha ufundi Arusha Dkt. Musa Chacha amesema kuwa wataendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuwajengea uwezo wakaguzi wa magari ili kuwa na ufanisi katika ukaguzi magari hapa nchini huku akimshukuru Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini kwa kuridhia wakaguzi hao kupata mafunzo chuo hapo.