propagandist
Member
- Aug 12, 2011
- 93
- 9
TV hii imekuwa ni kawaida yake katika kuonesha na kuripoti habari za chama cha wanainchi CUF imekuwa ni kawaida kutoa picha ambazo lengo lake ni kuwakatisha tamaa wafuasi na wanachama wa CUF Kwa kupiga picha za pembeni kabisa ya mkutano sehemu yenye umati wa watu huwa hawapeleki Camera, imefanyika hivyo mkutano wa CUF wa Arusha na baadaye TV hiyo ikaja kuumbuliwa na Mlimani TV kwa kuonesha umati uliofurika uwanjani na kufuatiwa na magazeti, mf. mzuri gazeti la Fahamu mwanainchi. Leo tena wamerudia yale yale kwa kupeleka Camera sehemu ya viongozi, tunashindwa kutambua vitendo hivyo wanavyokifanyia chama cha CUF ni kwa faida ya nani? au kwa faida ya chama gani? kama mnaona hamtaki kuonesha habari za cuf kwa ufasaha kwa nini mnapata tabu kwenda kwenye mikutano yao tafuteni habari zingine. CUF ipo ndani ya mioyo ya wana CUF hamtaweza kuiua au kuidhofisha mtakufa nyie CUF itabaki.