MTIKISIKO CCM: Pinda si shwari!

MTIKISIKO CCM: Pinda si shwari!

uzi wako unatuuliza sisi wachangiaji ama unatuambia?
 
Habari za uhakika nilizofikishiwa ni kwamba, waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akubaliani na yaliyotoka Dodoma katika harakati zilizofanywa kumpata mgombea urais wa CCM.

Pinda amedai kutokuridhishwa kwake na jina lake kaondolewa na kamati ya maadili huku watu aliokuwa akiwaongoza na kuwatetea kila kukicha bungeni wakipenya kwa kile alichokiita kuwa kwa utaratibu 'mbovu'

Pinda akionekana akilia kwa uchungu wakati ambapo John Magufuli alikuwa akitangazwa kama mgombea urais wa CCM mwaka 2015.

Aidha Pinda amedai kusikitishwa na jinsi ambavyo January Makamba alivyobebwa na mbeleko ya Kikwete kuingia tano bora huku akiwa na muda mfupi sana katika siasa.

Tutasikia mengi ila fukuto lililopo ndani ya CCM ni zaidi ya ujuavyo.

Mwisho tutakosa story ya ku trust +
Hata wewe!!!
 
Mwaka huu Invisible na Moderator wote mjiandae na Saver (Data base kubwa)za kutosha. Make Duuh, thread za CCM nikama gesti!!
 
Last edited by a moderator:
Porojooooooooo lakini kwa Baraza la vichaa Chadema ni issue moto. Hamnazo
 
Habari hizi za uhakika kweli???

Hizi ni porojo za kufurahiaha tu jukwaa hili. Pinda hana uthubutu wa kuihama ccm na wala hataki mikiki mikiki na vyombo vya dola.Ataendelea kufaidi mafao yake na marupurupu endelevu ya serikali hadi kufa kwake. Labda ccm ianguke na haya mafao ya maraisi makamu wao na mawaziri wakuu yapunguzwe au kusitishwa kabisa. Anayo miradi yake ya nyuki na mashamba ya matunda. Embe anauza elfu moja na mingine tusiyoijua na aliyowekeza kwa wanae n.k. Faida nyingine atakayoipata kama ataamua kujituliza na kutokihama chama chake ni kupata ile peace of mind hana cha kumfanya alie tena.
 
KANU ilipotea kwenye ramani kwa kumbeba Kenyatta ambaye hakuwa chaguo la wengi na Mwai Kibaki akaibukia upinzani na kushinda
Sema hivi Moi alilazimisha Uhuru agombee kwa tiketi ya New KANU akina Raila wakajitoa na kwenda kumuunga mkono Kibaki na Kibaki kuibuka mshindi.
 
Habari za uhakika nilizofikishiwa ni kwamba, waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akubaliani na yaliyotoka Dodoma katika harakati zilizofanywa kumpata mgombea urais wa CCM.

Pinda amedai kutokuridhishwa kwake na jina lake kaondolewa na kamati ya maadili huku watu aliokuwa akiwaongoza na kuwatetea kila kukicha bungeni wakipenya kwa kile alichokiita kuwa kwa utaratibu 'mbovu'

Pinda akionekana akilia kwa uchungu wakati ambapo John Magufuli alikuwa akitangazwa kama mgombea urais wa CCM mwaka 2015.

Aidha Pinda amedai kusikitishwa na jinsi ambavyo January Makamba alivyobebwa na mbeleko ya Kikwete kuingia tano bora huku akiwa na muda mfupi sana katika siasa.

Tutasikia mengi ila fukuto lililopo ndani ya CCM ni zaidi ya ujuavyo.

pinda ameonewa sana.jk alipaswa kumbeba pinda wamefanyakazi pamoja lakini sio makamba.ngoja tusikie pigo la lowasa
 
Back
Top Bottom