MTIKISIKO CCM: Pinda si shwari!

MTIKISIKO CCM: Pinda si shwari!

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,282
Reaction score
38,876
Habari za uhakika nilizofikishiwa ni kwamba, waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akubaliani na yaliyotoka Dodoma katika harakati zilizofanywa kumpata mgombea urais wa CCM.

Pinda amedai kutokuridhishwa kwake na jina lake kaondolewa na kamati ya maadili huku watu aliokuwa akiwaongoza na kuwatetea kila kukicha bungeni wakipenya kwa kile alichokiita kuwa kwa utaratibu 'mbovu'

Pinda akionekana akilia kwa uchungu wakati ambapo John Magufuli alikuwa akitangazwa kama mgombea urais wa CCM mwaka 2015.

Aidha Pinda amedai kusikitishwa na jinsi ambavyo January Makamba alivyobebwa na mbeleko ya Kikwete kuingia tano bora huku akiwa na muda mfupi sana katika siasa.

Tutasikia mengi ila fukuto lililopo ndani ya CCM ni zaidi ya ujuavyo.
 
KANU ilipotea kwenye ramani kwa kumbeba Kenyatta ambaye hakuwa chaguo la wengi na Mwai Kibaki akaibukia upinzani na kushinda
 
Kwa maana hiyo Pinda anaungana na Sophia Simba, Nchimbi, na Kimbisa = Team Lowassa?
 
Utetezi wake wa Bungeni ndio kigezo muhimu cha kukatwa - badala ya maslahi ya nchi yeye alishikilia maslahi ya chama.
 
Pinda keshanogewa na power....anashindwa imagine life without power now
 
Mbona waliokatwa ni wengi?..mBona hawasemi?..naamini kwa vyovyote vile lazima angepatikana mmoja tu kupeperusha bendera ya CCM...ni vyema kukubali matokeo na kusonga mbele.
 
Habari za uhakika nilizofikishiwa ni kwamba, waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akubaliani na yaliyotoka Dodoma katika harakati zilizofanywa kumpata mgombea urais wa CCM.

Pinda amedai kutokuridhishwa kwake na jina lake kaondolewa na kamati ya maadili huku watu aliokuwa akiwaongoza na kuwatetea kila kukicha bungeni wakipenya kwa kile alichokiita kuwa kwa utaratibu 'mbovu'

Pinda akionekana akilia kwa uchungu wakati ambapo John Magufuli alikuwa akitangazwa kama mgombea urais wa CCM mwaka 2015.

Aidha Pinda amedai kusikitishwa na jinsi ambavyo January Makamba alivyobebwa na mbeleko ya Kikwete kuingia tano bora huku akiwa na muda mfupi sana katika siasa.

Tutasikia mengi ila fukuto lililopo ndani ya CCM ni zaidi ya ujuavyo.

Mchakato ule ulikuwa mbofumbofu kabisa!

Kila wakati nimekuwa nikisema kwamba, ubora wa wanasiasa wetu uko chini ya kiwango. Hata mtu aliyekuwa Waziri mkuu hakujua kwamba miaka yote aliteteta uozo na haikuwa sahihi? Hajui hiyo ilikuwa ni kinyume cha maadili? Sasa akikatwa kwa kigezo cha maadili analalama kweli?

TZ, this hopeless country!
 
Amesahau kauli zake za kibabe bunge kusema wananchi wapigwe tu.Nayo kamati ya maadili ilichoshwa na uroho wake wa madaraka ikaamuru akatwe tu maana wajumbe walichoka
 
Ingawa wengi wataendelea kumsema vibaya lakini Mzee Kingunge aliongea mambo ya msingi sana ambayo CCM inatakiwa kuyafanyia kazi
 
Aliye leta hii mada ni muongo. Jina la pinda halikukatwa. Liliondolewa kwenye mchakato baada ya maridhiano.

Hawezi kulalamika kwa sababu hakuondolewa kwa vigezo bali kwa maridhiano kutokana na mazingira halusi.
 
Back
Top Bottom