Elections 2010 Mtei amwonya Kikwete

CCM wana mkakati wa kuwa kila mwenye maisha ya kati (middle class) au tajiri ni FISADI. Ili baadae tuamue kutafuta suluhu kuwa mwenye nacho abakie nacho tuanze afresh. Hili linaanza kupikwa hapa hapa.

Take care, huenda hili ndo kundi la majambazi alosema HALISI.
 
William ajajibu swali aliloulizwa tangu mwanzo. Ataje mali na utajiri wa mzee Mtei alioona unamweka katika kundi la mafisadi.
Naona hakujibu badala yake amejaribu kupindisha mjadala na kuelekea kutojibu swali hilo.
Please William. Jibu hili kwanza ua kanusha statement yako.
Mzee mtei alikuwa kiongozi mwaminifu hafananishwi na hizi taka za leo hata kidogo. Maana sikuwahi kusikia vituhuma kama hivi kwake. Lakini kwa miaka ya 90 na kuja mbele tumesikia vituhuma vingi tu kwa viongozi wetu wengi. Shame.
 
anna kilango malecela aliiba fedha za Gulf Airways wakati ameajiriwa kama mhasibu wao. william malecela kabla hujamvamia edwin mtei anaza kumhoji anna ambaye mnaishi nyumba moja.
 
Felister,
Ni life uncertainty gani iliyomsibu Lowassa? He has everything and more and he still wants to grab more.
 
Felister,
Ni life uncertainty gani iliyomsibu Lowassa? He has everything and more and he still wants to grab more.

Baada ya uhuru watanzania wote tulikuwa poor either absolutely or relatively kwa kipimo cha dolar so to me we all started as poor ila society yenyewe ndo iliharibu kwa kuwamistreat watu wote waliojitolea kwa moyo kulitumikia Taifa na ku end up kutupwa na community baada ya kikomo cha utumishi wao. We now call them our heros yes they are but also are the victims of their own decision for it was them who did not creat the sustainable system which could have taken care of them after the retirement. Hata hivyo si kosa kufanya kosa but ni kosa kurudia kosa lile lile kila mara. Ndiyo maana kwa mtu anaeona mbali atajihusisha katika kujenga sustainable system itakayo take care everybody for if its not system which would take care of the individuals then the fact is; the life of an individual is shotter than that of the institutions otherwise kamba uliyoisuka mwenyewe yaweza kugeuka kuwa kitanzi chako and therefore become a victim of your own decision.
 
Baada ya uhuru watanzania wote tulikuwa poor either absolutely or relatively kwa kipimo cha dolar so to me we all started as poor ila society yenyewe ndo iliharibu kwa kuwamistreat watu wote waliojitolea kwa moyo kulitumikia Taifa na ku end up kutupwa na community baada ya kikomo cha utumishi wao. We now call them our heros yes they are but also are the victims of their own decision for it was them who did not creat the sustainable system which could have taken care of them after the retirement. Hata hivyo si kosa kufanya kosa but ni kosa kurudia kosa lile lile kila mara. Ndiyo maana kwa mtu anaeona mbali atajihusisha katika kujenga sustainable system itakayo take care everybody for if its not system which would take care of the individuals then the fact is; the life of an individual is shotter than that of the institutions otherwise kamba uliyoisuka mwenyewe yaweza kugeuka kuwa kitanzi chako and therefore become a victim of your own decision.

swali kwani NSSF si wanawakata watu kila mwezi kwani hawalipi watu pension zao au zote ndio manji kashagawana na mkullo, alafu watu wakienda wanazungushwa
embu wenye kujua NSSF ikoje watudokezee ...
 
anna kilango malecela aliiba fedha za Gulf Airways wakati ameajiriwa kama mhasibu wao. william malecela kabla hujamvamia edwin mtei anaza kumhoji anna ambaye mnaishi nyumba moja.

- Labda ungemshauri mjomba wako Mboma kwanza arudishe Kiwira, halafu uje uongelee wizi wa Mama Kilango, au?

Respect.

FMEs!
 
William ajajibu swali aliloulizwa tangu mwanzo. Ataje mali na utajiri wa mzee Mtei alioona unamweka katika kundi la mafisadi.
Naona hakujibu badala yake amejaribu kupindisha mjadala na kuelekea kutojibu swali hilo.
Please William. Jibu hili kwanza ua kanusha statement yako.
Mzee mtei alikuwa kiongozi mwaminifu hafananishwi na hizi taka za leo hata kidogo. Maana sikuwahi kusikia vituhuma kama hivi kwake. Lakini kwa miaka ya 90 na kuja mbele tumesikia vituhuma vingi tu kwa viongozi wetu wengi. Shame.

- Mkuu jitahidi kutaja jina langu na hoja nzito, swali langu vipi mbona hujalijibu juu ya mali za wizi za viongozi wa CCM? Kwa maneno yako hapo juu ni clear kwamba humjui Mtei, wanaomjua wamesema alifamnya kazi nje kama Director wa IMF, hawakusema maneno kama yako, next time kabla hujanitaja jina langu jaribu kutumia busara mkuu, na usiniulize majibu wakati unaoneakan unayo maswali.

Ahsante Mkuu.

William.
 
- Labda ungemshauri mjomba wako Mboma kwanza arudishe Kiwira, halafu uje uongelee wizi wa Mama Kilango, au?

Respect.

FMEs!

Kwi kwi kwi!!! hawa mafisadi wameua Kiwira yetu yaani hata mimi nikiwaona naweza kurusha ngumi.

Kule Kyela hakuna ajira nyingi za maana, ndugu zetu walikuwa wanaponea pale Kiwira, sasa imegeuka gofu. Kumbe Mboma naye yumo?

Afadhali mungu alimlaani kule Mbeya vijijini. kwi kwi kwi!!!
 
Kwi kwi kwi!!! hawa mafisadi wameua Kiwira yetu yaani hata mimi nikiwaona naweza kurusha ngumi.

Kule Kyela hakuna ajira nyingi za maana, ndugu zetu walikuwa wanaponea pale Kiwira, sasa imegeuka gofu. Kumbe Mboma naye yumo?

Afadhali mungu alimlaani kule Mbeya vijijini. kwi kwi kwi!!!

- Sawa sawa aje ndugu yake akanushe hapa kwamba baba yake mdogo hayumo Kiwira, halafu aeleze pale kwenye Hotel ya karibu na JFK Airport baba yake alienda kukutana na nani ile siku?

- Wewe unafikiri wananchi wa Mbeya ni wajinga kumnyima ubunge Mkuu mzima wa Majeshi? Uliwahi kusikia wapi ex-Chief Defense Force anashindwa kura za maoni tu? Tena Mbeya kule kijijini duh noma sana!

FMES!
 
Baada ya uhuru watanzania wote tulikuwa poor either absolutely or relatively kwa kipimo cha dolar so to me we all started as poor ila society yenyewe ndo iliharibu kwa kuwamistreat watu wote waliojitolea kwa moyo kulitumikia Taifa na ku end up kutupwa na community baada ya kikomo cha utumishi wao. We now call them our heros yes they are but also are the victims of their own decision for it was them who did not creat the sustainable system which could have taken care of them after the retirement. Hata hivyo si kosa kufanya kosa but ni kosa kurudia kosa lile lile kila mara. Ndiyo maana kwa mtu anaeona mbali atajihusisha katika kujenga sustainable system itakayo take care everybody for if its not system which would take care of the individuals then the fact is; the life of an individual is shotter than that of the institutions otherwise kamba uliyoisuka mwenyewe yaweza kugeuka kuwa kitanzi chako and therefore become a victim of your own decision.

Felister,
nimefurahi sana kuona post zako mbili kwenye mada hii.......keep it up!

In short......hili lishetani/lijinamizi la UFISADI tumelijenga sisi wenyewe....and the only way out ni kuondoa mizizi yake.....kubadilisha systeme ambazo zitatumia vyema resources tulizonazo kwa faida ya wote........again im impressed the way you put it...
 
Na Mussa Juma

GAVANA wa kwanza wa Benki Kuu Tanzania(BoT) na aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika utawala wa Baba wa taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Edwin Mtei amemtahadharisha Rais Jakaya Kikwete atakabiliwa na matatizo makubwa kama hatakuwa mkali na kuwachukulia hatua watendaji wake wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi Jumapili nyumbani kwake eneo la Tengeru, mkoani Arusha mwanzoni mwa wiki hii, Mtei alisema baadhi ya wasaidizi wa Kikwete watasababisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kianguke katika uchaguzi mkuu mwakani kutokana na kuchafuliwa na tuhuma mbalimbali.

Mtei alisema wasaidizi wengi wa Kikwete hawaaminiki tena katika jamii, hivyo wananchi watapiga kura za hasira ili kuing'oa CCM madarakani.

“Ni vyema Rais Kikwete akawatazama upya wasaidizi wake, kwani wengi hawamsaidii na kama ataendelea kucheka nao nchi hii inaelekea pabaya, hivyo lazima akubali kuchukua maamuzi magumu kama anataka mambo yawe mazuri,” alisema Mtei.

Alisema hali inakoelekea nchi yetu imewahi kutokea katika nchi nyingi ambako viongozi wake wameondolewa madarakani kwa kushindwa katika uchaguzi kutokana na kucheka na wasaidizi wao wazembe na wabadhilifu, badala ya kuwachukuliwa hatua kali.

Mtei ambaye pia ni muasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alitoa mfano wa serikali ya chama tawala cha KANU, nchini Kenya kuwa kilikosa mwelekeo kutokana na viongozi wake kujaa tuhuma mbalimbali chafu.

Kuhusu watalaam kukimbia nchi, alisema inachangiwa na mfumo mbaya wa malipo ya kustaafu ambao hauwiani na mishahara yao.

“Tanzania kuna wasomi wazuri, lakini wanaikimbia nchi kwa sababu mishahara yao ni midogo sana na wakistaafu hawana uhakika wa maisha mazuri, tofauti na wanasiasa,” alisema Mtei.

Alisema kuna mambo mengi ya msingi ambayo yanapaswa kufanywa na Rais Kikwete, ikiwemo kuwa na mijadala ya kitaifa itakayosaidia kutoa suluhisho kwa matatizo yanayoikumba nchi, ili kuondoa tabaka kwa Watanzania wachache wanaoneemeka na rasilimali za nchi, huku kundi kubwa likibaki katika hali ya umasikini.

Mtei alisema Mwalimu Nyerere, aliweza kuongoza vema kutokana na kuwa mkali na hakusita kuchukua hatua dhidi ya kiongozi yoyote alipopata tetesi kwamba, anahusika na ubadhilifu.

“Mwalimu alikuwa anatuita na kutueleza kwamba,Tanzania kuna watu zaidi ya milioni 20 (wakati huo) wenye uwezo wa kushika nafasi za uongozi, hivyo yoyote kati yetu kama sio msafi atatoka na aliwaondoa wengi,” alisema Mtei.

Mwanasiasa huyu mkongwe, alisema si vizuri Rais Kikwete kuwa na msaidizi ndani ya serikali au chama ambaye anatiliwa shaka na wananchi.

“Ndio maana wakati wa Nyerere, viongozi wengi walikuwa wanakimbia nchi, kwani ikibainika tu kuna dosari ni lazima mhusika atachukuliwa hatua haraka,” alisema Mtei.

Alisema ni aibu, hivi sasa unasikia kuna kiongozi ana fedha nje ya nchi zenye utata,lakini hakuna hatua zinachukuliwa; jambo ambalo halikuwahi kutokea wakati wa Nyerere.

“Wakati ule Benki Kuu ndiyo ilikuwa inahusika na uchunguzi wa fedha nje ya nchi na tulipobaini kuwa mtu fulani ana fedha nje, tulikuwa tunampa taarifa mwalimu na yeye alikuwa mkali sana na kuchukuwa hatua haraka,” alisema Mtei.

Alisema baaada ya kupitishwa Azimio la Zanzibar lililoua Azimio la Arusha, hakuna tena miiko ya uongozi na viongozi hawana woga wa kufanya biashara jambo ambalo pia ni hatari kwa taifa.

“Nampongeza Rais Kikwete kwa kubaini hili na kutoa utaratibu wa mtu kuchagua moja kati ya siasa na biashara, hili ni jambo zuri na katika nchi hizi masikini ni lazima kuwepo miiko ya aina hii,” alisema Mtei.

Akizungumzia kashfa ya ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya Kampuni ya Dowans, Mtei alisema wakati wa Nyerere jambo hili lisingewezekana hata kujadili.

“Wakati ule kama kampuni yako au shirika likibainika tu linajihusisha na rushwa katika masuala haya ya manunuzi kulikuwa na faili jeusi la makampuni na ikiingizwa humo huwezi kupewa kazi yoyote ya serikali bila kibali maalumu cha waziri wa fedha,” alisema Mtei.

Alisema kwa suala la Dowans ni wazi, kampuni hiyo ina uhusiano na Kampuni ya Richmond hivyo kuingilia katika mjadala wa kununua mitambo ambayo tayari iliwahi kutiwa doa ni jambo lisilopaswa kupewa nafasi hata ya kujadiliwa.

Akizungumza mfumo wa maslahi ya watumishi wa umma; alipendekeza kuwa Rais Kikwete aunde tume maalum ya kupitia mishahara na marupurupu yote ya watumishi wa umma.

“Hivi sasa hakuna uwiano katika malipo, kuna watu wanalipwa fedha kwa siku moja ambayo ni malipo ya mshahara wa mwezi wa mtumishi mwingine jambo ambalo lazima litazamwe,” alisema Mtei.

Alifafanua kwamba, hata mfumo wa malipo ya wastaafu unapaswa kurekebishwa ili ulingane na malipo ya wastaafu wa ngazi za juu serikalini.

“Tunapaswa kuwa na mfumo ambao utamwezesha mstaafu kuishi maisha mazuri na sio kufa baada ya kustaafu,” alisema Mtei.


huyu mzee mchango wake ni mkubwa
Tungekuwa na wazee kama hawa nchi hii ingeendelea
 
Akina Ndejembi waliojipachika heshima ya 'Wazee wa CCM' na kutumia vitisho na ubabe kutaka kuwanyima haki wanaCCM wanaotaka kugombea nafasi ya Urais 2010 eti kwa kuwa wana utamaduni wao wa kuachiana Rais wa kutoka chama chao akae madarakani kwa vipindi viwili kwa sababu 'kafanya mazuri' ukiwauliza ni mazuri yapi aliyoyafanya wayaorodhoshe, wanang'aa macho!!!!! Kuwa na makundi ndani ya CCM na kuyumba kwa chama hicho ni dalili nyingine ya uongozi duni wa Kikwete.

Bubu haya ni maneno uliyosema mwaka 2009, almost mwaka na nusu uliopita lakini ni very valid sasa. Hili swali ingekuwa vizuri tumuulize malaria sugu atujibu. Yanayofanyika sasa ni mipango ya Mkapa na Kigoda, sana sana awamu ya nne imefanya kazi ya kuyavurunda.
 
Huyu mzee asijifanye mtu wa uwiano wakati kama huu. Hiyo risala angeitoa mwaka jana au juzi ningemwelewa. Wakati huu alitakiwa kufanya kazi ya kampeni kwa chama chake ili tuje kumuenzi kama baba wa mageuzi. Inaelekea pia hafaham kuwa kipindi hiki ni cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu. Chadema for change!
 
Huyu mzee asijifanye mtu wa uwiano wakati kama huu. Hiyo risala angeitoa mwaka jana au juzi ningemwelewa. Wakati huu alitakiwa kufanya kazi ya kampeni kwa chama chake ili tuje kumuenzi kama baba wa mageuzi. Inaelekea pia hafaham kuwa kipindi hiki ni cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu. Chadema for change!
Kingi,
Acha kukurupuka. Hiyo risala ilitolewa miaka 2 iliyopita. Angalia dateline.
 
Huo ni ushauri kutoka moyoni. Alipomshauri Mwl Nyerere akubaliane na ushauri wa IMF, Nyerere alikakata na kumwambia kama ushauri wake ulikuwa wa dhati ajiuzuru.

PHP:
Ushauri wangu wa kutoka moyoni, Kikwete jitoe kwenye kinyang'anyiro cha urais
 
Hapa angalia tofauti ya hekima na busara anayoitoa Mzee Mtei, isiyokuwa na ushawishi wa kisiasa bali mapenzi ya nchi na utaifa. Je unaweza kufananisha busara zake na zile pumba zilizotolewa na wale wazee waganga njaa wakina Ndejembi?

Namsifia Nyerere, mbona yeye mwenyewe alitolewa baruti alipotoa mapendekezo yake ya kuimarisha shilingi.

Na Nyerere alimtukana na kusema anatumiwa na wamagharibi. Kama ni CV toka kwa nyerere, basi Mtei aasingepewa hata nafasi ya kuzungumza.
 
Baadaye Mwalimu aligundua ushauri wa Mtei ulikuwa sahihi. Ndio maana Mwalimu akamshauri Mwinyi akubaliane na IMF. Kama Mwalimu angeambilika wakati aliposhauriwa na Mtei, hali haingekuwa mbaya kama ilivyokuwa miaka 80 - 85.

Mwalimu hakutaka "kugeuka jiwe" wakati akingali madarakani. Lakini alitambua mapema usahihi wa ushauri wa Mtei. Ndio maana hata akaamua kumteua Mtei awe mteule wake wa kazi ya Alternate Director IMF.

Kuna siku Mwalimu atakutana na Mtei Mbinguni. Mie nadhani Mwalimu ataomba msamaha.

Hayo yote ni tisa. Kumi ni kwamba someni kitabau cha Mtei "From Goatherd to Governor". It is a must read for anyone who has an interest in the contemporary history of Tanzania.
 
hivi JK aliwahi kusoma hii makala?? au hata kumpigia simu huyu mzee,mwanauchumi mwenzake??
 
Kwa muda mrefu sikusoma/sikufungua kompyuta na kusoma yanayosemwa juu yangu binafsi. Leo ndiyo naona hii ripoti ya Asha Abdalla baada ya kuzungumza nami hapa nyumbani kwangu.

Nashukuru wanaJF wengi kwa kukubaliana nami kwamba nilikuwa mnyofu na muwazi ktk kutoa ushauri kwa Rais wangu. Nakubaliana na wale wanaodhani kwamba ni vema wazee walio na uzoefu wakachangia nao ktk mijadala.

Nikiri kwamba nimesikitishwa sana na matamshi ya wanaJF, kama William Malecela, kwamba mimi pia nilifanya mambo ya kifisadi.

Kwanza niseme kwamba mimi si tajiri. Hata katika kitabu nilichoandika na kuchapisha hivi karibuni "From Goatherd to Governor" nimeeleza jinsi nilivyoweza kununua shamba la Ogaden baada ya kujiuzulu Uwaziri wa Fedha mwishoni mwa mwaka1979. Shamba hili lenye ekari 52 tu, lilibadilishwa na nyumba yangu ya Mzinga Way, OysterBay baada ya Mkadiriaji (Valuer) kukadiria thamani ya hiyo nyumba. Hiyo nyumba niliijenga kwa mkopo toka Serikalini.

Nimeeleza pia kwamba kwa miaka minne nilikuwa Executive Director wa IMF kwa kuteuliwa na Mwalimu Nyerere; na kwamba napokea pensheni toka Shirika hilo tangu nilipotimiza miaka 55; pamoja na ya Serikali ya Tanzania kutokana na utumishi wangu kama Permanent Secretary to the Treasury nilikostaafu kutokana na kuteuliwa Gavana wa Benki Kuu Januari 1966. Tunajazia pensheni hizi kwa kulima kahawa na kufuga ng'ombe, nguruwe na kuku.


Najivunia kwamba siishi kwa kujititimua, na mke wangu pia hana makuu. Kwa hiyo tumeweza kusomesha watoto wetu waweze kujitegemea; na sasa sisi wenyewe tunaweza kuendesha maisha bila matatizo ya fedha.


Nieleze pia ni jambo la kusikitisha kwamba Watanzania tumedidimia kimaadili kiasi kwamba vijana wetu wengi, kama William , wana dhana kwamba mtu yeyote mwenye fedha ni lazima awe fisadi. Tunahitaji Mabadiliko ya kweli kuondoa dhana hii. Ni lazima tuwe na watu wanaojituma na kutoa jasho ili tupate kipato cha kuridhisha.

Fursa ya kubadili imejitokeza sasa kutokana na CHADEMA, kumteua Dr. Slaa kugombea u-Rais. Ni excitement hii ya kwamba INAWEZEKANA KULETA MABADIKO YA KWELI ifikapo Oktoba 2010 yamenifanya, kama Muasisi wa hiki chama, nikose kusoma thread hii mapema. WanaJF nawaomba radhi kwa ku-comment so late.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom