Mtarajiwa wangu simuelewi

Mtarajiwa wangu simuelewi

Kuongea au kupanga ni rahisi sana... ila linapokuja swala la utekelezaji wengi wanashikwa na kigugumizi... Alafu kama mshakaa miaka yote hiyo pamoja unadhani kuna kitu tena hapo...
 
Me si mlazimishi ni ahadi tuliyojiwekea kwann? Haivunje na yeye ndo wakwanza ( kanibikili) Mara ya mwisho kuonana Naye mwaka Jana mwez wa 7
Basi pole, ila wanaume ni kama wasaka tenda. Anapoona sehemu kuna fursa ya kupata tenda ataifukuzia kwa nguvu zote hadi aipate. Akishaipata anaifanya kwa muda then anaipiga chini.

Akishapiga mara mbili tatu anaanza kusaka tenda zingine. So lazima uyajue hayo ili usiwe unamuwaaaaza kila siku wakati mwenzio ashaanzisha project zingine.
 
Tusiwalaumu sana wanaume...hata sisi akili zetu zikisikia ndoa zinaganda,hatuwazi tena wala hatuoni kingine..Mungu atusaidie sana
Kama unampenda mtu toka moyoni mama kuja kugutuka kama hana lengo na wewe huchukua muda .... Ndo maana mimi siku hizi ni mguu ndani na mguu nje yaani ni 50/50
 
Kama unampenda mtu toka moyoni mama kuja kugutuka kama hana lengo na wewe huchukua muda .... Ndo maana mimi siku hizi ni mguu ndani na mguu nje yaani ni 50/50
Kweli kabisa siyorahisi kujua kama hana lengo na mumi kutokana na upendo nilionao kwake na nilivyo mjengea imani
 
Piga moyo konde simama usonge mama, tapeli huyo. Mapito ya kawaida kabisa ya maisha hayo shukuru kwa uhai, aliyekuchagulia Mungu yupo. Usije lazimisha matatizo mengine makubwa.
 
Pole kwa sasa unamaumivu makali na hasira moyoni. Tulia omba Mungu vuta subira. Jipe moyo jitie nguvu usimtafute tena huyo mpenzi wako. Kama una mtoto lea mwanao bila msaada wake kama hujazaa na hii utaweza iwapo utafanya kazi kwa bidii. Kasi yotote ile mradi si kujiuza au haramu ili ulee mwanao bila kumtegemea. Jipe muda walau wa mwaka mmoja au miwili kabla hujaingia mahusiano mengine. Waweza kuwa na marafiki wa kiume kwa kipindi hicho ila uwe makini wasiwe wapenzi la huwezi kuwa na rafiki wa kiume bila kuwa wapenzi basi uwe na marafiki wa kike tuu au uwe kimwenyewe mwenyewe hadi utakapokuwa tayari kuingia kwenye mahusiano mapya.
Muhimu ujipende jitunze jithamini usikubali mtu akirudishe nyuma au kukuumiza kwa mawazo hasi.
Pole sana na kila la kheri, kwa asili yetu sisi wanawake lia weeeh tena kwa nguvu hadi hasira yako iishe kisha mtoe akilini mwako na songa mbele.
Ukifanya hivi nakwambia utang'aa na kupendeza upyaa hata kama unaogea mbuni na kupata rays moyo wako uwe meupeee na mwepesi usishikilie mtu hukoo.
Kila la kheri mama.
Asante Dada yangu nitafanya hivyo
 
Piga moyo konde simama usonge mama, tapeli huyo. Mapito ya kawaida kabisa ya maisha hayo shukuru kwa uhai, aliyekuchagulia Mungu yupo. Usije lazimisha matatizo mengine makubwa.
Asante
 
Hamna ndoa tena hapo ingekua anataka kuja kwenu angeshakuja bila ata wew kumwambia apo lazma kuna mwenzako ukipata mchumba mwingne usikubal tena kukaa kwenye mahusiano mda mref ivyo mtu anakujua sana pengne ata mpenz wako kuna tabia kaziona kwako hazijampendeza labda ndo maana kakimbia
 
Ndoa..ndoa...ndoa dada zetu ni ndoa ni ndoa lakini mjue kuwa mtazamo wetu wanaume juu ya ndoa ni tofauti na wakwenu!..poleni
 
Ni ukweli usiopingika kuwa kamwe HAUWEZI KWENDA KINYUME NA MAAGIZO YA MWENYEZI MUNGU NA UKABAKI SALAMA.......mwenyezi MUNGU anapotoa makatazo kwa waja wake si katika nia ya kuwatesa waja wake bali ni katika kuwatakia mema....
Agizo la kutaka watu wasiikaribie zinaa ni katika kuuhifadhi na kuheshimu utu wa mwanadamu.....ukweli mchungu ni kwamba huyo jamaa haoni thamani yako tena ,haoni sababu kupoteza chambo kwa samaki aliyekuwa tayari anaye nchi kavu......ameshakinai na wewe haoni jipya lolote kwako......umegeuka kuwa kero kwake badala ya kuwa chem chem ya furaha kwake........haoni sababu ya kukuoa kwa kuwa kile alichokuwa akikihitaji kwenye ndoa alishakipata kwako......tena kwa muda miaka zaidi ya mitatu....kwa lugha nyepesi huyo ameshakukinai........hili ni moja kati ya masomo magumu kwako lakini huna budi kujifunza.....huna budi kuanza upya kwani kuanza upya sio ujinga.....mwanadamu mwenye hekima hujifunza kutokana na makosa yake...na ni mwanadamu mpumbavu ambaye hajifunzi kupitia makosa yake........

Na hili pia liwe funzo kwa wadada wengine walio kwenye njia kama anayopitia mtoa mada....
 
Ni ukweli usiopingika kuwa kamwe HAUWEZI KWENDA KINYUME NA MAAGIZO YA MWENYEZI MUNGU NA UKABAKI SALAMA.......mwenyezi MUNGU anapotoa makatazo kwa waja wake si katika nia ya kuwatesa waja wake bali ni katika kuwatakia mema....
Agizo la kutaka watu wasiikaribie zinaa ni katika kuuhifadhi na kuheshimu utu wa mwanadamu.....ukweli mchungu ni kwamba huyo jamaa haoni thamani yako tena ,haoni sababu kupoteza chambo kwa samaki aliyekuwa tayari anaye nchi kavu......ameshakinai na wewe haoni jipya lolote kwako......umegeuka kuwa kero kwake badala ya kuwa chem chem ya furaha kwake........haoni sababu ya kukuoa kwa kuwa kile alichokuwa akikihitaji kwenye ndoa alishakipata kwako......tena kwa muda miaka zaidi ya mitatu....kwa lugha nyepesi huyo ameshakukinai........hili ni moja kati ya masomo magumu kwako lakini huna budi kujifunza.....huna budi kuanza upya kwani kuanza upya sio ujinga.....mwanadamu mwenye hekima hujifunza kutokana na makosa yake...na ni mwanadamu mpumbavu ambaye hajifunzi kupitia makosa yake........

Na hili pia liwe funzo kwa wadada wengine walio kwenye njia kama anayopitia mtoa mada....
Nimekuelewa.....nitajifunza
 
fimbo ya mbali haiui Nyoka hii methali bado ipo?
 
Back
Top Bottom