Mtarajiwa wangu simuelewi

Mtarajiwa wangu simuelewi

Pole sana huyo ameshabadili mawazo kama hakuwa akikudanganya tuu na kukupotezea muda ili akutumie fanya maamuzi yako anza maisha mengine kabisa utampata wa kwako kikweli
 
Pole kwa sasa unamaumivu makali na hasira moyoni. Tulia omba Mungu vuta subira. Jipe moyo jitie nguvu usimtafute tena huyo mpenzi wako. Kama una mtoto lea mwanao bila msaada wake kama hujazaa na hii utaweza iwapo utafanya kazi kwa bidii. Kasi yotote ile mradi si kujiuza au haramu ili ulee mwanao bila kumtegemea. Jipe muda walau wa mwaka mmoja au miwili kabla hujaingia mahusiano mengine. Waweza kuwa na marafiki wa kiume kwa kipindi hicho ila uwe makini wasiwe wapenzi la huwezi kuwa na rafiki wa kiume bila kuwa wapenzi basi uwe na marafiki wa kike tuu au uwe kimwenyewe mwenyewe hadi utakapokuwa tayari kuingia kwenye mahusiano mapya.
Muhimu ujipende jitunze jithamini usikubali mtu akirudishe nyuma au kukuumiza kwa mawazo hasi.
Pole sana na kila la kheri, kwa asili yetu sisi wanawake lia weeeh tena kwa nguvu hadi hasira yako iishe kisha mtoe akilini mwako na songa mbele.
Ukifanya hivi nakwambia utang'aa na kupendeza upyaa hata kama unaogea mbuni na kupata rays moyo wako uwe meupeee na mwepesi usishikilie mtu hukoo.
Kila la kheri mama.
 
Hapo we jiongeze tu maana kama akisikia sauti yako hata ukimpigia kwa simu na simu nyingine anakata hapo huna lako. Huhitaji akili ya ziada kuamua
 
Me si mlazimishi ni ahadi tuliyojiwekea kwann? Haivunje na yeye ndo wakwanza ( kanibikili) Mara ya mwisho kuonana Naye mwaka Jana mwez wa 7
Unataka akuoe kwasababu kakubikiri, kwasababu mliahidiana au kwasababu anakupenda (mnapendana)?
 
Ushaachwa kiaina...........ukipata bahati ya mwisho kutoka kwa mwingine usiache oooohh
 
Kwahiyo unamlazimisha hata kama kaahirisha?

Ni kawaida kubadili mawazo sio lazima akuoe hata kama anakuona we ni jipu. Suala la kuoana ni la milele, kwanini alazimishe? Tafta wengine ambao hawajaoa kama mimi
Hahah,muwahi pm sasa umpooze ..kamata fursa
 
Ndoa ni nzuri sana kama utaipatia
Ndoa ni mbaya sana kama utaikosea
Mahusiano ya muda mrefu si mazuri
Ingia kwenye mahusiano kwa sababu maalumu iwe kuoa au kuolewa na si vinginevyo
Hayo mahusiano hayatakiwi kuzidi mwaka mmoja kisa mnataka juana
Uchumba ni pale mnapotambulishana kwenu na baada ya hapo ndani ya miezi sita muwe mmeoana
Tatizo mnaweka kambi mnoooo
 
Back
Top Bottom